FT: Simba 0-3 Raja Casablanca | CAF Champions League | Estadio Benjamin Mkapa | 18.02.2023
Enzi za marais toka Zanzibar lazima tufungwe tu.

Hata wakitoa bilioni kama motisha.
 
Mama kawaponza wameingia na tamaa ya million tano + kauli ya Raisi , wakasahau uhalisia wa game
 
Ni ngumu sana kufanya usajili wa wachezaji aina ya sawadogo na ukataka upate matokeo kama wenzako, Sisi tunaoangalia mpira na kuuelewa kiufundi tulikuwa tunajua ni ngumu sana kwa kikosi hiki cha simba kutoboa kimataifa, unapoona timu imewekeza kwenye ushirikina badala ya kufanya usajili ujue kinachofata ni majanga, Simba hii ata hapa ilipofika imejitahidi kwa aina ya wachezaji walionao, Hili nililiona tokea mechi za mwanzo dhidi ya zile timu dhaifu, Bata big bullet na De agosto , tulipokuwa tunasema simba imetinga makundi baada ya kukutana na timu dhaifu tulikuwa tunaona kwa jicho la 3 mambo mengi ya kiufundi, Kibaya zaidi kiwango walichoonyesha walipocheza na Horoya ambayo sio timu ya kutisha ni ya kawaida lakini walipata shida ata kuifunga kigoli kimoja pamoja na kupata nafasi, Na mashabiki wao uwa wanajua kushupaza shingo wakiamini wana kikosi bora kama misimu 2 iliyopita, Unapotaja kwa mkapa atoki mtu pia unaangalia kipindi kile ulikuwa na wachezaji wa aina gani na sasa hivi una wachezaji wa aina gani, Unaweza ukaroga uwanja mwezi mzima na kupigwa ukapigwa vile vile kama auna quality ys wachezaji, Niwatakie usiku mwema mashabiki wa simba kunyweni angalau castle lite moja mpate angalau usingizi leo
 
20230218_205938.jpg
 
Hiyo penati hata sijaiona nilikuwa katika harakati za kutoka uwanjani

Ila nilichojifunza mashabiki inabidi tubadilike sana

Wakati natoka nje hapa kwenye hizi ngazi uwanjani nimestuka na kelele za watu waliokuwa wanamkinbiza mtu wakimuita mwiz

Alikuwa ni dogo tu maskini watu wamemzinga wamepiga kipigo kikali watu wakijua ni mwizi

Lakini mwisho wa siku kumbe dogo alikuwa anashangilia penati ya Raja

Wamemuumiza sana dogo anavuja damu hata nguvu ya kusimama amekosa

Dear friends timu yako kama haichezi kwa Mkapa sio sehemu salama wewe kwenda ukifikiri utakuwa huru kushangilia wapinzani wako wakifungwa kama ukiwa mtaani au humu jukwaani
Wanageuza furaha kuwa vita. Very stupid
 
Back
Top Bottom