Hakika wanaume mna akili za ajabu sana. Kwanini mkipata pesa mnabadilika sana?


Nimekuelewa mpenzi, yaani nilimbeba sana alipokuwa akilitia kipindi kizito cha kufutwa kazi na kuugua ila sasa ameona haitoshi ameamua kutangaza ndoa kabisa kwa mwanamke mwingine ambaye hata hakuwa nae wakati wa matatizo.

Nimejutia muda niliopoteza nae kanipotezea muda wangu mno, uwii naumia mimi [emoji24]
 
Pole sana mama ila ndio maisha, wanaume tunatofautiana sana calibre! Mie siwezi acha mtu ambaye amekuwa namimi nikiwa juani ila too bad wapo watu ambao wanaweza.

Kitu ambacho nataka confirm kwako ni kuwa uliishi vipi nae wakati hana. Unajua kuvumilia mwanaume ni jambo moja na tabia uliokuwa nayo wakati unamvumilia ni jambo la pili ambalo huwa linakuwa overlooked vibaya mno.
 
Pole, chukulia haikuwa fungu lako...Yuko wa kwako anakusubiri somewhere, kumbuka dunia ina watu karibia bilioni 6, it's not worth it kukalilia kajitu kamoja....kaache kaende.
Dedication song umeachwa, kubali
 
Hata sisi wazazi wanatusonesha hafu matunda mnayafaidi ninyi
 
Kabisa shosti, hivi unaweza uza asset zaidi ya milioni mia ukatumia pesa yote kufanyia starehe kweli bila kukumbuka mtu aliyekufadhili wakati ulipokuwa na shida, nimehuzunika sana kwa kweli pesa wanafaidi wanawake wengine oopss [emoji25][emoji24]
Kinachokuuma ni yeye kukuacha, au kinachokuuma ni kuwa unashindwa kuzifaidi pesa zake, baada ya we kueKeza pesa zako Kwake ukitegemea we utakuja zifaidi mbele, sasa hayo sio mapenzi, ni biashara tena ya utumwa

Ni sawa mm nimsomeshe dada halafu baadae akiolewa kwingine, nilalamike kuwa nimemsomesha halafu kaniacha, sasa huo si itakua utumwa, kiuhalisia natakiwa nilalamike kua nimeachwa Priscallia
 
Tuwe realistic, hapa Tanzania wanaume wenye hela nyingi wako wangapi? Bongo tuko million 60, tuseme million 30 ni wanaume, sasa utakuta wanaume wanaopata Tsh million 2 kwa mwezi, hawafiki Wanaume million 1 Tanzania nzima, wanawake mko million 30 sasa equation unaibalance vipi hapo cariha
 
Na ndio maana mimi nimemwambia, usitake kutendewa wema, wakati wewe mwenyewe una roho mbaya, na tabia chafu chafu nyingi.

Wanaume huwa tunawastahi tu then baada ya Muda tunachapa lapa.
 
Equation ita balance kwa mimi kutafta hela yangu na sio ku support ndoto za mwingine Ili anipende
 
Mshukuru Mungu kwa kila jambo huyo hakukupenda toka moyoni alikupendea status flani ya mtelezo wa Ganda la ndizi, Sasa mambo yamenyooka anaenda kwa ampendaye, what I have noticed ukiwa mwema kwa mwanaume ukamsaidia sana, mwisho huishia pabaya hujiona wao sio wanaume kamili na huenda kutafta mpya asiye jua hustle zake wale naye vizuri, but I'm sure after a while atakurudia tu kwako
 
Si mnasemaga titafte hela jamani! Tabu ya kuzipata ndio kama hivyo kila demu full shobo
Mimi nitasaidia mwanaume ka ninavosaidia yoyote mwenye shida, bila ku expect anioe, sijui anipende hapana kwa kweli, wadada wengi sikuhizi vile wataka ndoa huwahonga wanaume na kuanza kufanya vitu vya maendeleo pamoja akiamini ni mume, kumbe mwanaume kafata mserereko wa kiulaini
 
Dah umenikumbusha mwaka juzi yule kima Mungu ampige laana nilikuwa natoa nauli ya kwenda kutafuta kazi,kula juu yangu alivyopata kazi nyoko yule alinipiga na kitu kizito siku amini ila namshukuru amenifunza kuwa kauzu zaidi ya dagaa😬😬
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…