Hivi Mungu alikosa njia nyingine ya kufikisha ujumbe tofauti na Vitabu?

Hivi Mungu alikosa njia nyingine ya kufikisha ujumbe tofauti na Vitabu?

Sasa nilichotaka ujibu si umeshajibu!!, umedai Mungu atumie malaika, atuongezeee akili ya kujua maneno yake nk, si ndio!!, mbona ulikuwa unaogopa kutoa majibu??!, bila shaka ulijua kuwa njia zako zingekuwa dhaifu sana kuliko njia ya Mungu, na ni dhaifu mno.
Ukifuatilia hapo sijakujibu wewe, nimemjibu mtu mwingine.
Na wewe nilikuwa sitaki kukujibu kwakuwa nilijua tu kwa mahaba yako ya kumtetea mungu kila njia utakuwa unaikataa. Na mimi sitaki majadiliano yaende huko kuanza kujadili njia zangu maana hazitabadilisha kitu.

Point yangu ni kwamba hata kama mimi binafsi sina njia bora haimaanishi Mungu nayeye hawezi kuipata au ameshindwa.

Na kama ameikosa au ameshindwa kupata njia bora zaidi basi tukubaliane kuwa hawezi kila kitu.
.
 
Mkuu em soma post ya kwanza nimeeleza failures za hii njia ya maandishi.

Kitendo tu cha kuwepo madhehebu kibao yanayosoma maandishi yaleyale na kupishana uelewa ni failure ya hiyo njia.

Alikosa njia ambayo binadamu wote duniani wataelewa anataka nini na anatakaje bila kutofautiana?

Sasa wasabato wanaamini usipotunza jumamosi hauendi mbinguni, walokole wanasema siku yoyote tu ni sabato.
Je kama Mungu mwenyewe alikuwa upande wa wasabato? Ina maana siku ya kiama hawa walokole wanaenda motoni kwa kukosea kuelewa maandiko yake?

Mifano ni mingi mno.


Ndio maana nimekuuliza wewe ni dini gani??, yawezekana wewe ni atheist !!, nikijua dini yako ndipo ninaweza kukujibu vyema juu ya kasoro za hizo njia mbadala unazopendekeza, kwasababu hujui kusudi la mtu kuumbwa.
 
Ndio maana nimekuuliza wewe ni dini gani??, yawezekana wewe ni atheist !!, nikijua dini yako ndipo ninaweza kukujibu vyema juu ya kasoro za hizo njia mbadala unazopendekeza, kwasababu hujui kusudi la mtu kuumbwa.
Hizi njia zangu mbadala nimezifikiria tu ndani ya dakika 2, huu mjadala wa kuanza kuzijadili na kutafuta mapungufu yake ni kupoteza tu muda na kuchengesha lengo la huu uzi.

Maana Mungu ameishi miaka Milele kabla ya kuiumba dunia kwahyo alikuwa na Muda wa kutosha wa kufikiria njia mbadala kuliko mimi.

Alikosa?
Maana hii aliyoitumia ni wazi kabisa ina mapungufu.
 
Ukifuatilia hapo sijakujibu wewe, nimemjibu mtu mwingine.
Na wewe nilikuwa sitaki kukujibu kwakuwa nilijua tu kwa mahaba yako ya kumtetea mungu kila njia utakuwa unaikataa. Na mimi sitaki majadiliano yaende huko kuanza kujadili njia zangu maana hazitabadilisha kitu.

Point yangu ni kwamba hata kama mimi binafsi sina njia bora haimaanishi Mungu nayeye hawezi kuipata au ameshindwa.

Na kama ameikosa au ameshindwa kupata njia bora zaidi basi tukubaliane kuwa hawezi kila kitu.
.


Nani kakuambia kuwa Mungu anaweza kila kitu??, Mungu hawezi kuiba, hawezi kusema uongo, hawezi kudhulumu, hawezi kunyima haki ya mtu nk, Mungu HAWEZI kutenda mambo yote mabaya.

Ni hivi; Mungu amepanga na hakuna wa kupangua, amepanga kumuumba mtu na hatimaye huyo mtu aende akhera baada ya kufariki dunia na kufuliwa huko akhera, huko akhera kuna moto na pepo, katika moto wataingizwa wakosefu ili dhambi zao zichomwe na zikiisha ndipo wataingia peponi, ili mtu aingie peponi ni lazima afanye jitihada ya kushika mafundisho ya manabii (general case), mafundisho hayo ndio mengine yamehifadhiwa katika mfumo wa vitabu ili mtu asome na kuelewa Mungu anataka nini, kumekuwepo na mikorogano mingi katika kila dini juu ya hayo mafundisho hii inatokana na uelewa wa binadamu kuwa tofauti kwa kujua hilo ndipo Mungu kupitia dini ya kiisilamu akamtuma nabii mfuasi ili aje kufundisha dini sahihi ya Uisilamu, Uisilamu ulianzishwa na mtukufu mtume Muhammad (saw) na nabii wake Mfuasi ni Hadhrat mirza Ghulam Ahmad (as) nabii aliyeahidiwa kufika kuwaleta watu wa dini zote chini ya bendera ya Uisilamu, huyo nabii Mfuasi ndiye aliyeanzisha kwa amri ya Mungu jumuiyya ya Waisilamu wa Ahmadiyya duniani, Jumuiya hii imekuja kuvunja makundi ya dini zote duniani na kuwa kundi moja, hivyo ili kuondoa mtafaruku na miss understanding za mafundisho ya kidini hakuna haja ya kuja malaika wala Mungu kumuongezea mtu akili nk, kwani akili alizonazo binadamu Mungu mwenyewe ndiye kampa na anajua zinamtosha ili kujua neno lake.

Sasa ili umjue Mungu na mafundidho yake sahihi yasiyo na mkanganyiko ingia katika jumuiya ya Waisilamu wa Ahmadiyya .
 
Mans knowledge is limited. What we don't is beyond our knowledge.

Kuna baadhi ya mambo huwa tunapoteza muda na nguvu kuyahoji.

Tambua hakuna mwanadamu anaefahamu uwezo au utashi wa Mungu Kwamba kwanini alifanya kile na kwanini hakufanya hiki.

Vitabu vya dini hasa Biblia vimejaribu kumuelezea Mungu lakini ile ni "summary" tu ya machache kuhusu.Vitabu vya dini sio mwisho wa kila kitu kumuhusu Mungu.

Mungu ni zaidi ya tunavyodhani na tulivyofundishwa. Km kikiandikwa kitabu kumuelezea Mungu basi h kitabu hicho kitakuwa hakina mwisho na hakuna mwanadamu atakaeweza kukimaliza kukisoma.
POINT.
 
Wewe ndio umefeli sio Mungu

Kuna binadamu walifundishwa Kumjua Mungu kupitia mahubiri ya manabii na miujiza sio vitabu na bado walifeli

Binadamu umepewa akili ili uitumie hiyo akili kumjua Mungu wa kweli hayo mengine ya kutafuta chakula na kujenga nyuma hata Ndege wanayafanya
Kwahyo njia pekee zilizopo ni manabii, miujiza na vitabu?
Mungu amekosa njia nyingine ambayo haitafeli?

Mbona hesabu haifeli?
Ulishakutana na watu wanaobishana 1+1? Yani wengine waseme ni mbili wengine ni 3??

Lakini ni kawaida kukuta watu wanabishana maandiko.
 
Nani kakuambia kuwa Mungu anaweza kila kitu??, Mungu hawezi kuiba, hawezi kusema uongo, hawezi kudhulumu, hawezi kunyima haki ya mtu nk, Mungu HAWEZI kutenda mambo yote mabaya.

Ni hivi; Mungu amepanga na hakuna wa kupangua, amepanga kumuumba mtu na hatimaye huyo mtu aende akhera baada ya kufariki dunia na kufuliwa huko akhera, huko akhera kuna moto na pepo, katika moto wataingizwa wakosefu ili dhambi zao zichomwe na zikiisha ndipo wataingia peponi, ili mtu aingie peponi ni lazima afanye jitihada ya kushika mafundisho ya manabii (general case), mafundisho hayo ndio mengine yamehifadhiwa katika mfumo wa vitabu ili mtu asome na kuelewa Mungu anataka nini, kumekuwepo na mikorogano mingi katika kila dini juu ya hayo mafundisho hii inatokana na uelewa wa binadamu kuwa tofauti kwa kujua hilo ndipo Mungu kupitia dini ya kiisilamu akamtuma nabii mfuasi ili aje kufundisha dini sahihi ya Uisilamu, Uisilamu ulianzishwa na mtukufu mtume Muhammad (saw) na nabii wake Mfuasi ni Hadhrat mirza Ghulam Ahmad (as) nabii aliyeahidiwa kufika kuwaleta watu wa dini zote chini ya bendera ya Uisilamu, huyo nabii Mfuasi ndiye aliyeanzisha kwa amri ya Mungu jumuiyya ya Waisilamu wa Ahmadiyya duniani, Jumuiya hii imekuja kuvunja makundi ya dini zote duniani na kuwa kundi moja, hivyo ili kuondoa mtafaruku na miss understanding za mafundisho ya kidini hakuna haja ya kuja malaika wala Mungu kumuongezea mtu akili nk, kwani akili alizonazo binadamu Mungu mwenyewe ndiye kampa na anajua zinamtosha ili kujua neno lake.

Sasa ili umjue Mungu na mafundidho yake sahihi yasiyo na mkanganyiko ingia katika jumuiya ya Waisilamu wa Ahmadiyya .
Okay kumbe uwezo wa Mungu ni limited..ina maana kuna mambo hawezi na inawezekana hata hilo jambo la kutafuta njia bora alishindwa...Sawa.

Tuje kwenye point yako...kwa maelezo yako, nilivyokuelewa ni kuwa Mungu alikosea mwanzo kuleta maandiko yake, Watu kutokana na uwezo wao wa kuelewa wakapotoka na kukatokea makundi meengi yenye mafundisho tofauti tofauti.... Sasa Mungu akashtuka kuwa hali ni mbaya akaamua alete nabii mwingine tena mwenye maelezo mengine tena? (Maana Sidhani kama kuna dhehebu/dini nyingine iliyokuwepo yenye mafundisho sawa 100% na Ahmadiya)

Kwahyo watu wote kabla ya huyo Ghulam walikosea kutafsiri mafundisho ya Mungu.
Mungu akashtuka alipofeli ndio akamleta Ghulam arekebishe si ndio?

kutokana na Maelezo yako tunaweza kuconclude kuwa.
A:
1.Mungu alikosea/Mungu hukosea
2.Mungu hujirekebisha baada ya kukosea
3.Kama Mungu anakosea inamaana hakujua kama anachofanya kitakosanisha na kutenganisha watu, (Angejua asingeleta mafundisho yeyote angemleta tu Ghulam tokea Mwanzo)..Kwahyo Mungu hajui kila kitu
4.Kama hajui kila kitu ina maana hana uwezo wa kila kitu

Sasa kama Hana uwezo wa kila kitu na hajui kila kitu, kwanini hata tunamuita Mungu?
B:
Bado njia aliyotumia kurekebisha amefeli maana wewe unasema Ghulam ndio mwisho wa reli, Wasabato wanasema Ellen Gm white ndio mwisho wa reli, Wasunni wanasema Muhamad ndio mwisho wa reli, Waroma husema Papa ndio mwisho wa reli, Wafuasi wake husema Mwamposa ndio mwisho wa reli..


Kwahyo bado tatizo liko palepale, Ghulam hajasaidia, ila ameongezea tatizo maana nayeye ameongeza kundi lingine tena..Na sasa waahmadiya wanauliwa na wasunni huko middle east.

Inamaana Mungu ameshindwa kufikiria njia bora kuliko hawa manabii na vitabu itakayofanya binadamu wote duniani waamini kitu kimoja?
 
Okay kumbe uwezo wa Mungu ni limited..ina maana kuna mambo hawezi na inawezekana hata hilo jambo la kutafuta njia bora alishindwa...Sawa.

Tuje kwenye point yako...kwa maelezo yako, nilivyokuelewa ni kuwa Mungu alikosea mwanzo kuleta maandiko yake, Watu kutokana na uwezo wao wa kuelewa wakapotoka na kukatokea makundi meengi yenye mafundisho tofauti tofauti.... Sasa Mungu akashtuka kuwa hali ni mbaya akaamua alete nabii mwingine tena mwenye maelezo mengine tena? (Maana Sidhani kama kuna dhehebu/dini nyingine iliyokuwepo yenye mafundisho sawa 100% na Ahmadiya)

Kwahyo watu wote kabla ya huyo Ghulam walikosea kutafsiri mafundisho ya Mungu.
Mungu akashtuka alipofeli ndio akamleta Ghulam arekebishe si ndio?

kutokana na Maelezo yako tunaweza kuconclude kuwa.
A:
1.Mungu alikosea/Mungu hukosea
2.Mungu hujirekebisha baada ya kukosea
3.Kama Mungu anakosea inamaana hakujua kama anachofanya kitakosanisha na kutenganisha watu, (Angejua asingeleta mafundisho yeyote angemleta tu Ghulam tokea Mwanzo)..Kwahyo Mungu hajui kila kitu
4.Kama hajui kila kitu ina maana hana uwezo wa kila kitu

Sasa kama Hana uwezo wa kila kitu na hajui kila kitu, kwanini hata tunamuita Mungu?
B:
Bado njia aliyotumia kurekebisha amefeli maana wewe unasema Ghulam ndio mwisho wa reli, Wasabato wanasema Ellen Gm white ndio mwisho wa reli, Wasunni wanasema Muhamad ndio mwisho wa reli, Waroma husema Papa ndio mwisho wa reli, Wafuasi wake husema Mwamposa ndio mwisho wa reli..


Kwahyo bado tatizo liko palepale, Ghulam hajasaidia, ila ameongezea tatizo maana nayeye ameongeza kundi lingine tena..Na sasa waahmadiya wanauliwa na wasunni huko middle east.

Inamaana Mungu ameshindwa kufikiria njia bora kuliko hawa manabii na vitabu itakayofanya binadamu wote duniani waamini kitu kimoja?


Mungu anaweza kila kitu kinachoendana na kanuni na sifa zake njema, mfano Mungu hawezi kunifanya mimi nikawa wewe na vice versa au Mungu hawezi kumfufua mtu aliyekufa kwani akifanya hivyo atakuwa kafanya kinyume na kanuni/sheria zake na hivyo kuwa Mungu kigeugeu. Mungu hawezi kufanya mambo yatakayoharibu sifa zake njema akifanya hivyo yeye anakuwa sio Mungu, ili hadhi na heshima yake ibaki inabidi mambo yote mabaya asiweze kuyafanya, Mungu hawezi kumuumba Mungu mwingine wafanane katika sifa nk, hiyo ndio maana ya Mungu kutokuweza kufanya Kila kitu, katika mambo mema Yeye anaweza kila kitu.

Katika mada: Ndio maana kabla sijaanza kukujibu nilikuuliza wewe ni dini gani?? au huna dini??, ningejua wewe ni dini gani nadhani ningalikuwa na njia sahihi ya kukujibu vinginevyo tutazunguka hadi kukuche.
 
Nani kakuambia kuwa Mungu anaweza kila kitu??, Mungu hawezi kuiba, hawezi kusema uongo, hawezi kudhulumu, hawezi kunyima haki ya mtu nk, Mungu HAWEZI kutenda mambo yote mabaya.

Ni hivi; Mungu amepanga na hakuna wa kupangua, amepanga kumuumba mtu na hatimaye huyo mtu aende akhera baada ya kufariki dunia na kufuliwa huko akhera, huko akhera kuna moto na pepo, katika moto wataingizwa wakosefu ili dhambi zao zichomwe na zikiisha ndipo wataingia peponi, ili mtu aingie peponi ni lazima afanye jitihada ya kushika mafundisho ya manabii (general case), mafundisho hayo ndio mengine yamehifadhiwa katika mfumo wa vitabu ili mtu asome na kuelewa Mungu anataka nini, kumekuwepo na mikorogano mingi katika kila dini juu ya hayo mafundisho hii inatokana na uelewa wa binadamu kuwa tofauti kwa kujua hilo ndipo Mungu kupitia dini ya kiisilamu akamtuma nabii mfuasi ili aje kufundisha dini sahihi ya Uisilamu, Uisilamu ulianzishwa na mtukufu mtume Muhammad (saw) na nabii wake Mfuasi ni Hadhrat mirza Ghulam Ahmad (as) nabii aliyeahidiwa kufika kuwaleta watu wa dini zote chini ya bendera ya Uisilamu, huyo nabii Mfuasi ndiye aliyeanzisha kwa amri ya Mungu jumuiyya ya Waisilamu wa Ahmadiyya duniani, Jumuiya hii imekuja kuvunja makundi ya dini zote duniani na kuwa kundi moja, hivyo ili kuondoa mtafaruku na miss understanding za mafundisho ya kidini hakuna haja ya kuja malaika wala Mungu kumuongezea mtu akili nk, kwani akili alizonazo binadamu Mungu mwenyewe ndiye kampa na anajua zinamtosha ili kujua neno lake.

Sasa ili umjue Mungu na mafundidho yake sahihi yasiyo na mkanganyiko ingia katika jumuiya ya Waisilamu wa Ahmadiyya .
Kaka Akhi , Nurain Eturgrul Kazakh destroyer ufafanuzi please hasa huku mwisho ahmadiya hata dm uzi wawatu usijebadili maanamaana
 
Hata kabla ya vitabu mwenyezi Mungu aliwatuma mitume wake moja kwa moja kwa umma kuwapa maamrisho na makatazo.mfano watu wa musa kwa firauni/ farao, nuhu kwa watu wake na bado walikataa nimemtaja Musa na watu ambao walioneshwa dhahiri ukubwa wa Mungu kwa bahari kuoasuka.na njia kufanyika lkn bado walikataa, unadhabi njia gani ingekua bora?
Bro Kazakh destroyer Naomba nikumbushe ile aya ambao wanadamu waliambiwa hata wangeletewa malaika bado wangemkataa kama wanavympinga mtume pbuh
 
1. Malaika wawe visible...si huwa wanasema kila mtu ana malaika wake?
Sasa kila malaika anakuwa visible anakuwa anakufundisha Mambo ya Mungu kila saa ukiuliza.
Inakuwa haina haja ya kwenda kanisa hili au lile kupotoshwa na mwanadamu mwenzako maana utakuwa unapata directly from the source.

2.Aongeze uelewa wa binadamu ili wawe wanaelewa maandiko yake kama alivyokusudia ili kuepusha madhehebu kibao na mitafaruku.

3. Awabandike binadamu mafundisho yake akilini mwao, yani unazaliwa ukipata ufahamu tu automatically unakuwa unajua kila kitu kuhusu Mungu anataka nini, ila inakuwa choice yako tu..kunakuwa hakuna haja ya kwenda kusoma sehemu au kufundishana matangopori.
4.Nk. Nk.......

Anything is possible actually, yeye si Mungu bana.
Yani kuna infinite possibilities.
Binafsi nimekuelewa sana mkuu.
 
Okay kumbe uwezo wa Mungu ni limited..ina maana kuna mambo hawezi na inawezekana hata hilo jambo la kutafuta njia bora alishindwa...Sawa.

Tuje kwenye point yako...kwa maelezo yako, nilivyokuelewa ni kuwa Mungu alikosea mwanzo kuleta maandiko yake, Watu kutokana na uwezo wao wa kuelewa wakapotoka na kukatokea makundi meengi yenye mafundisho tofauti tofauti.... Sasa Mungu akashtuka kuwa hali ni mbaya akaamua alete nabii mwingine tena mwenye maelezo mengine tena? (Maana Sidhani kama kuna dhehebu/dini nyingine iliyokuwepo yenye mafundisho sawa 100% na Ahmadiya)

Kwahyo watu wote kabla ya huyo Ghulam walikosea kutafsiri mafundisho ya Mungu.
Mungu akashtuka alipofeli ndio akamleta Ghulam arekebishe si ndio?

kutokana na Maelezo yako tunaweza kuconclude kuwa.
A:
1.Mungu alikosea/Mungu hukosea
2.Mungu hujirekebisha baada ya kukosea
3.Kama Mungu anakosea inamaana hakujua kama anachofanya kitakosanisha na kutenganisha watu, (Angejua asingeleta mafundisho yeyote angemleta tu Ghulam tokea Mwanzo)..Kwahyo Mungu hajui kila kitu
4.Kama hajui kila kitu ina maana hana uwezo wa kila kitu

Sasa kama Hana uwezo wa kila kitu na hajui kila kitu, kwanini hata tunamuita Mungu?
B:
Bado njia aliyotumia kurekebisha amefeli maana wewe unasema Ghulam ndio mwisho wa reli, Wasabato wanasema Ellen Gm white ndio mwisho wa reli, Wasunni wanasema Muhamad ndio mwisho wa reli, Waroma husema Papa ndio mwisho wa reli, Wafuasi wake husema Mwamposa ndio mwisho wa reli..


Kwahyo bado tatizo liko palepale, Ghulam hajasaidia, ila ameongezea tatizo maana nayeye ameongeza kundi lingine tena..Na sasa waahmadiya wanauliwa na wasunni huko middle east.

Inamaana Mungu ameshindwa kufikiria njia bora kuliko hawa manabii na vitabu itakayofanya binadamu wote duniani waamini kitu kimoja?
Hakuna kitu kimeleta muongozo kwa binadam Ni watu wenyewe wamejitungia tu hivyo habari za kitu kinaitwa Mungu Ni uongo mtupu
 
Kwahyo njia pekee zilizopo ni manabii, miujiza na vitabu?
Mungu amekosa njia nyingine ambayo haitafeli?

Mbona hesabu haifeli?
Ulishakutana na watu wanaobishana 1+1? Yani wengine waseme ni mbili wengine ni 3??

Lakini ni kawaida kukuta watu wanabishana maandiko.
Kwa hiyo wewe unasema njia ya manabii, miujiza na vitabu zimefeli kwasababu hizo njia hazijakuwezesha wewe Kumjua Mungu wa kweli na dini ya kweli?

Jibu ni kwamba hazijafeli ila wewe ndio unajifelisha mwenyewe kwa kutotaka kuutafuta ukweli

Akili aliyokupa Mungu inawezo wa kukufanya wewe ujue ukweli kupitia hizo njia na ndio maana matahira na wanakufa wakiwa Bado watoto hawataenda jahanam

Ila wewe mtu mzima mwenye akili timamu usipotumia akili yako Kuujua ukweli Hadi siku inaingia kaburini jua jahanam inakusubiri
 
Mungu anaweza kila kitu kinachoendana na kanuni na sifa zake njema, mfano Mungu hawezi kunifanya mimi nikawa wewe na vice versa au Mungu hawezi kumfufua mtu aliyekufa kwani akifanya hivyo atakuwa kafanya kinyume na kanuni/sheria zake na hivyo kuwa Mungu kigeugeu. Mungu hawezi kufanya mambo yatakayoharibu sifa zake njema akifanya hivyo yeye anakuwa sio Mungu, ili hadhi na heshima yake ibaki inabidi mambo yote mabaya asiweze kuyafanya, Mungu hawezi kumuumba Mungu mwingine wafanane katika sifa nk, hiyo ndio maana ya Mungu kutokuweza kufanya Kila kitu, katika mambo mema Yeye anaweza kila kitu.

Katika mada: Ndio maana kabla sijaanza kukujibu nilikuuliza wewe ni dini gani?? au huna dini??, ningejua wewe ni dini gani nadhani ningalikuwa na njia sahihi ya kukujibu vinginevyo tutazunguka hadi kukuche.
It seems wewe una visheria vyako ulivyomuwekea Mungu....congrats.

Lakini Huoni kitendo cha Mungu kuleta maandiko yaliyochanganya watu na kupelekea wengine kuuana kwa vita za kidini kwa maelfu sio jambo jema?
Jambo jema ni angetumia mbinu kufikisha ujumbe ambayo haitatutenganisha binadamu.
Kwahyo kuleta hiyo mbinu bora sio jambo baya kama wewe unavyotaka kulipaint.

infact kutoleta hiyo mbinu kwenyewe ni jambo baya analofanya.
 
Hata kabla ya vitabu mwenyezi Mungu aliwatuma mitume wake moja kwa moja kwa umma kuwapa maamrisho na makatazo.mfano watu wa musa kwa firauni/ farao, nuhu kwa watu wake na bado walikataa nimemtaja Musa na watu ambao walioneshwa dhahiri ukubwa wa Mungu kwa bahari kuoasuka.na njia kufanyika lkn bado walikataa, unadhabi njia gani ingekua bora?
Bro Kazakh destroyer Naomba nikumbushe ile aya ambao wanadamu waliambiwa hata wangeletewa malaika bado wangemkataa kama wanavympinga mtume pbuh
Ishu sio kwa watu walioamua wenyewe kukataa,,watu wa kukataa watakuwepo na sio kesi.

Kesi ipo kwa wale walioamua kukubali sasa ila wamefata mafundisho yaliyo kinyume na mpango wa Mungu kwasababu hawakuelewa vizuri maandiko...au walifata mafundisho ya watu wengine ambao hawakuelewa maandiko
Mfano: Quran ni moja lakini utakuta kuna shule tofauti tofauti za kiislam zinabishana kuhusu aya ile ile moja kwenye Quran.
Utakuta wasunni,waahmadiya,washiya wanabishania aya zilezile za Quran.
Mf. Ukiuliza Mungu yuko wapi,unaweza kupata majibu zaidi ya 6 na wote wanatoa majibu yao kwenye kitabu kimoja.

sasa hapa ndio hoja ilipo...Kwa kutumia maandiko na kwasababu binadamyu wanatofautiana uelewa, maandiko yaleyale yameleta makundi mngi yanayopingana.
sasa Mungu kwanini alitumia hii njia huku akijua viumbe wake ni dhaifu?Kwanini asingetafuta njia bora kufikisha ujumbe wake ili kuepusha yote haya??

Ona sasa hata huwezi kujua dini ipi ni sahihi,Maana kila dini au kila dhehebu linasema lenyewe ndiyo sahihi na yote yanatofautiana na yapo maelfu kwa maelfu
 
Ahmadia wanakoroga Mambo sana
Hahaah,wewe unasema wao wanakoroga, Wao wanasema wako sahihi Wasunni ndio wanakoroga.

Lakini wote wanasoma Quran ileile.
kuna makundi ya kidini yanayopishana mafundisho zaidiya 50,000 (Kwa hizi Abrahamic religion)
Sasa Tuassume hapo ni kundi moja tu ndio lipo sahihi lets say Wasunni tu,,,inamaana kuna makundi 49,000 yenye mabillioni ya watu yamepotoka.

Sasa hapa ndio hoja yangu ilipo, Hii njia ya vitabu inapotosha sana watu..Kwanini Mungu aliitumia??
Alikosa njia bora zaidi?
 
Kwa hiyo wewe unasema njia ya manabii, miujiza na vitabu zimefeli kwasababu hizo njia hazijakuwezesha wewe Kumjua Mungu wa kweli na dini ya kweli?

Jibu ni kwamba hazijafeli ila wewe ndio unajifelisha mwenyewe kwa kutotaka kuutafuta ukweli

Akili aliyokupa Mungu inawezo wa kukufanya wewe ujue ukweli kupitia hizo njia na ndio maana matahira na wanakufa wakiwa Bado watoto hawataenda jahanam

Ila wewe mtu mzima mwenye akili timamu usipotumia akili yako Kuujua ukweli Hadi siku inaingia kaburini jua jahanam inakusubiri
Wapo maelfu ya watu wanaotumia akili zao kwa moyo wote kuutafuta ukweli na wengine wanaishia kuwa Mapadri,wengine wanasema ukweli ni kuitunza sabato,wengine wanasema Uislam ndio ukweli pekee nk. nk.

Sasa kwsababu wote mafundisho yao yanapingana kwa namna moja au nyingine, wote hawawezi kuwa sawa.

kuna makundi ya kidini yanayopishana mafundisho zaidi ya 50,000 (Kwa hizi Abrahamic religion)
Sasa Tuassume hapo ni kundi moja tu ndio lipo sahihi lets say Waislam wa kisunni tu,,,inamaana kuna makundi 49,000 yenye mabillioni ya watu yamepotoka.

Sasa hapa ndio hoja yangu ilipo, Hii njia ya vitabu inapotosha sana watu..Kwanini Mungu aliitumia??
Alikosa njia bora zaidi?
 
Hahaah,wewe unasema wao wanakoroga, Wao wanasema wako sahihi Wasunni ndio wanakoroga.

Lakini wote wanasoma Quran ileile.
kuna makundi ya kidini yanayopishana mafundisho zaidiya 50,000 (Kwa hizi Abrahamic religion)
Sasa Tuassume hapo ni kundi moja tu ndio lipo sahihi lets say Wasunni tu,,,inamaana kuna makundi 49,000 yenye mabillioni ya watu yamepotoka.

Sasa hapa ndio hoja yangu ilipo, Hii njia ya vitabu inapotosha sana watu..Kwanini Mungu aliitumia??
Alikosa njia bora zaidi?
Uislamu umebainisha njia moja TU Ambayo Ni Quran na Sunnah ..mwenye kupita nje ya mafundisho hayo anapewa nasaha iliyonjema asipotaka kufuata juu yake...
 
Back
Top Bottom