Hivi Mungu alikosa njia nyingine ya kufikisha ujumbe tofauti na Vitabu?

Hivi Mungu alikosa njia nyingine ya kufikisha ujumbe tofauti na Vitabu?

Hahaah,wewe unasema wao wanakoroga, Wao wanasema wako sahihi Wasunni ndio wanakoroga.

Lakini wote wanasoma Quran ileile.
kuna makundi ya kidini yanayopishana mafundisho zaidiya 50,000 (Kwa hizi Abrahamic religion)
Sasa Tuassume hapo ni kundi moja tu ndio lipo sahihi lets say Wasunni tu,,,inamaana kuna makundi 49,000 yenye mabillioni ya watu yamepotoka.

Sasa hapa ndio hoja yangu ilipo, Hii njia ya vitabu inapotosha sana watu..Kwanini Mungu aliitumia??
Alikosa njia bora zaidi?
Mkuu sizani kama kweli ni Mungu alileta hivyo vtabu , ukivisoma tu utajua vina eggo na majivuno ya kibinadamu kabsa havina umuhimu wowote kama mtu utajitambua
 
Uislamu umebainisha njia moja TU Ambayo Ni Quran na Sunnah ..mwenye kupita nje ya mafundisho hayo anapewa nasaha iliyonjema asipotaka kufuata juu yake...
Humo humo kwenye usilam kuna mkundi mengi yamejitokeza, ila main ni Wasunni na washia.
Tusiende mbali koote....tuanzie humohumo kwenye wasunni kuna makundi kama ma4 yamejitokeza yenye mafundisho tofauti tofauti
Kuna Hanafi,Maliki,Sha'afi,Hanbali
Hawa wote wasunni ila wanatofautiana kwenye kutafsiri Quran na maagizo ya sunnah
Mfano kwenye kuswali
Maliki wanaswali mikono ikiwa pembeni
Hanafi wanaume wanaswali ikiwa chini ya kitovu na wanawake ikiwa kifuani
Sha'afi wanasema Bismillah kwa sauti,wengine hawasemi
Hanafi wanasema ni wajibu mwanamke kufunika mikono,miguu,uso
Maliki na Sha'afi wanasema mwanamke anaruhusiwa kuachia uso,miguu na mikono wazi akiswali
Hanbali wao wanasema mwanamke haruhusiwi kuachia wazi sehemu yoyote kasoro uso wazi kipindi anaswali
Nk. nk.
Na hizo ni tofauti tu kwenye kuswali,lakini ukifuatilia utakuta wanatofautiana karibia kila sekta.

Hapo bado hatujaja kwa makundi mengine kama ahmadiya,ibadi,wasufi nk.

Sasa tuchukulie Ni dhambi mwanamke kuswali huku umeachia uso wazi..Basi inamaana kuna kundi kubwa la wasunni wasiofunika uso wanamchukiza Mungu kila wakiswali.

Haya yote wanatoa kwenye Quran na Sunna humohumo...
Sasa huoni kuwa Mungu hii njia ya maandishi inachanganya sana watu na njia mbovu sana aliyotumia kufikisha ujumbe wake?
 
Mkuu sizani kama kweli ni Mungu alileta hivyo vtabu , ukivisoma tu utajua vina eggo na majivuno ya kibinadamu kabsa havina umuhimu wowote kama mtu utajitambua
Kama hakuvileta sawa atleast itamake sense..lakini kama ni kweli alivileta anaonekana ni dhaifu sana maana kifasihi tunasema Fanani ameshindwa kufikisha ujumbe aliokusudia kwa hadhira yake.
 
Our GOD is God of varieties.
Duniani kuna dini+madhehebu zaidi ya elfu 40(na kila dini inadai yenyewe ndio ipo sawa kuliko zingine).
Kitakachokufikisha mbinguni sio diniyako bali ni your personal relationship with GOD
Dini ndio relionship kati ya watu na Mungu.
Msabato kuitunza Jumamosi na kumkumbuka Mungu hiyo siku ndio personal relationship yake na Mungu.
Muislam kwenda Hijja pia ni personal relationship yake na Mungu wake Allah.

Sasa Kama Mungu anataka bunadamu wote personally ikifika Jumamosi waache kazi zote na kumkumbuka kama wasabato wanavyosema..huoni tayari kuna mkanganyiko hapo??

Mlokole anaona personally kunena kwa lugha na kugalagala umejawa roho mtakatifu ndio njia pekee binadamu anaweza kuwa na mahusiano ya kweli na Mungu. Muislam anasema kunena kwa lugha ni aina fulani ya uchizi.
 
Humo humo kwenye usilam kuna mkundi mengi yamejitokeza, ila main ni Wasunni na washia.
Tusiende mbali koote....tuanzie humohumo kwenye wasunni kuna makundi kama ma4 yamejitokeza yenye mafundisho tofauti tofauti
Kuna Hanafi,Maliki,Sha'afi,Hanbali
Hawa wote wasunni ila wanatofautiana kwenye kutafsiri Quran na maagizo ya sunnah
Mfano kwenye kuswali
Maliki wanaswali mikono ikiwa pembeni
Hanafi wanaume wanaswali ikiwa chini ya kitovu na wanawake ikiwa kifuani
Sha'afi wanasema Bismillah kwa sauti,wengine hawasemi
Hanafi wanasema ni wajibu mwanamke kufunika mikono,miguu,uso
Maliki na Sha'afi wanasema mwanamke anaruhusiwa kuachia uso,miguu na mikono wazi akiswali
Hanbali wao wanasema mwanamke haruhusiwi kuachia wazi sehemu yoyote kasoro uso wazi kipindi anaswali
Nk. nk.
Na hizo ni tofauti tu kwenye kuswali,lakini ukifuatilia utakuta wanatofautiana karibia kila sekta.

Hapo bado hatujaja kwa makundi mengine kama ahmadiya,ibadi,wasufi nk.

Sasa tuchukulie Ni dhambi mwanamke kuswali huku umeachia uso wazi..Basi inamaana kuna kundi kubwa la wasunni wasiofunika uso wanamchukiza Mungu kila wakiswali.

Haya yote wanatoa kwenye Quran na Sunna humohumo...
Sasa huoni kuwa Mungu hii njia ya maandishi inachanganya sana watu na njia mbovu sana aliyotumia kufikisha ujumbe wake?
Kuna Jambo wengi hamlielewi....kuhitilafiana vs kufarikiana ...kuhitilafiana Ni kitendo Cha kuwa na maoni tofauti ktk dini na yote Ni katka jitihada za kuifuata dini....Jambo hili halitutoi katka itikadi sahihi ya ahl sunna na lilikuwepo hata Zama za mtume.....

Kufarikiana Ni kitendo Cha kupishana Hadi kupelekea uadui katika dini ,,Jambo hili limekatazwa kisheria katika uislamu..


Hivyo Mimi nikihitilafiana na ndugu yangu Bado wote tunakuwa ahl sunna...Ndio maana hao ahl Elm uliowataja hapo unakuta Imam Maliki aliswali kwa iman hambal na imam hambal naye aliswali kwa imam Maliki lkn Kuna sehemu walipishana ktk baadhi ya mambo...


Kuhusu Ahmadia,mashia na ibadh na mapote wengine hao Ni katika watu waovu ..


Kudai utume unaendelea Ni ukafiri,,kuwatukana baadhi ya maswahaba wa mtume ni ukafiri...
 
Dini ndio relionship kati ya watu na Mungu.
Msabato kuitunza Jumamosi na kumkumbuka Mungu hiyo siku ndio personal relationship yake na Mungu.
Muislam kwenda Hijja pia ni personal relationship yake na Mungu wake Allah.

Sasa Kama Mungu anataka bunadamu wote personally ikifika Jumamosi waache kazi zote na kumkumbuka kama wasabato wanavyosema..huoni tayari kuna mkanganyiko hapo??

Mlokole anaona personally kunena kwa lugha na kugalagala umejawa roho mtakatifu ndio njia pekee binadamu anaweza kuwa na mahusiano ya kweli na Mungu. Muislam anasema kunena kwa lugha ni aina fulani ya uchizi.
Personal relationship ni uhusiano wako binafsi na Mungu hicho unachoelezea ni uhusiano na mfumo wa dini yako.

Kwa kuongezea tu siku ya mwisho ya hukumu kila mtu(personally) atahukumiwa kulingana na uhusiano wake binafsi na Mungu katika maisha yake duniani hakutakua na kigezo cha dini .Wokovu ni suala binafsi sio la kijumuiya
 
Dini ndio relionship kati ya watu na Mungu.
Msabato kuitunza Jumamosi na kumkumbuka Mungu hiyo siku ndio personal relationship yake na Mungu.
Muislam kwenda Hijja pia ni personal relationship yake na Mungu wake Allah.

Sasa Kama Mungu anataka bunadamu wote personally ikifika Jumamosi waache kazi zote na kumkumbuka kama wasabato wanavyosema..huoni tayari kuna mkanganyiko hapo??

Mlokole anaona personally kunena kwa lugha na kugalagala umejawa roho mtakatifu ndio njia pekee binadamu anaweza kuwa na mahusiano ya kweli na Mungu. Muislam anasema kunena kwa lugha ni aina fulani ya uchizi.
Mungu hana shida na dini+dhehebu unalotoka Mungu anashida na moyo wako(personal relationship with GOD)
 
Mungu hana shida na dini+dhehebu unalotoka Mungu anashida na moyo wako(personal relationship with GOD)
Hebu tumia fikra ndogo tu serikali imeweka taratibu wananchi tufuate,,,ukiviolate taratibu utashtakiwa mahakamani then utaulizwa kwann hukufuata ...hii akili ndogo...

Sasa iweje Mungu akuumbe halafu akuache tu Bila kukupa Muongozo ,,je ukikosea atakurekebisha na nn...

Jibu ndio hili hapa ,,Kwamba Ni kweli tumembwa na tumewekewa Muongozo na maonyo hii kutokana na ukweli kuwa binadamu anakitu kinaitwa UTASHI...Kama asingewekewa njia ya kufuata Basi Uovu ungekuwa wa hali ya juu kuliko ufikiriavyo....

Quran Ni Muongozo wenye maonyo,maelekezo na suluhisho juu ya maisha ya binadamu
 
Personal relationship ni uhusiano wako binafsi na Mungu hicho unachoelezea ni uhusiano na mfumo wa dini yako.

Kwa kuongezea tu siku ya mwisho ya hukumu kila mtu(personally) atahukumiwa kulingana na uhusiano wake binafsi na Mungu katika maisha yake duniani hakutakua na kigezo cha dini .Wokovu ni suala binafsi sio la kijumuiya
Okay personal relationship na Mungu ipoje?Toa mfano.

Then kama ni hivyo basi hivi vitabu kumbe sio vya Mungu? Maana ndo vimeleta dini.
 
Kwanini asingetumia njia bora zaidi kufikisha ujumbe wake? Au hajui hiyo njia? Au hana huo uwezo?
ndugu usikengeuke kwa maneno yako ya dharau, kama ni hoja ungeitoa then ukaacha kutoa dhihaka yako humu. Mungu alitumia manabii wa kale kufikisha ujumbe kwa wanadamu, baada ya kuona hiyo njia si njema sana ndipo akatoa nafsi yake ikazaliwa Duniani kama mwanadamu ili ujumbe wa neno lake ufike kwetu live.

Yesu Kristo alikuwa ni Mungu katika nafsi ya Mungu mwana, alifundisha na akatimiza tabiri zote za manabii wa kale.
 
Neno la Mungu haliongozwi na tafsiri binafsi za kibinadamu bali huongozwa na mafunuo ya roho.
Okay, Mbona sasa Roho anafunulia watu mambo tofauti tofauti yanayopingana?Mpaka sasa kuna madhehebu zaidi ya 50, 000?
Ellen G white anasema alifunuliwa kuwa Usiposali Jumamosi utaenda Motoni, Walokole wanafunuliwa kuwa kusali ni siku yoyote.
Mwamposa anafunuliwa tofauti, Gwajima tofauti.

Na kama Ni hivyo, kwanini sasa roho asingefunulia binadamu wote kitu kimoja? Wakawa na dini moja?
 
ndugu usikengeuke kwa maneno yako ya dharau, kama ni hoja ungeitoa then ukaacha kutoa dhihaka yako humu. Mungu alitumia manabii wa kale kufikisha ujumbe kwa wanadamu, baada ya kuona hiyo njia si njema sana ndipo akatoa nafsi yake ikazaliwa Duniani kama mwanadamu ili ujumbe wa neno lake ufike kwetu live.

Yesu Kristo alikuwa ni Mungu katika nafsi ya Mungu mwana, alifundisha na akatimiza tabiri zote za manabii wa kale.
Mkuu kuna sehemu nimeonesha dharau?
Au kuuliza swali na kwenyewe ni dharau?

Yesu alikuja akaondoka, (Labda angeendelea kuishi Milele hapa duniani) kwahyo sisi tusingefaidika lolote kwa kuja kwake...ila sasa wewe na mimi tulisikia habari zake kupitia Mathayo, Luka na Marko tumetofautiana, Wewe umekuwa Mlokole mimi nimekuwa msabato.
 
Okay, Mbona sasa Roho anafunulia watu mambo tofauti tofauti yanayopingana?Mpaka sasa kuna madhehebu zaidi ya 50, 000?
Ellen G white anasema alifunuliwa kuwa Usiposali Jumamosi utaenda Motoni, Walokole wanafunuliwa kuwa kusali ni siku yoyote.
Mwamposa anafunuliwa tofauti, Gwajima tofauti.

Na kama Ni hivyo, kwanini sasa roho asingefunulia binadamu wote kitu kimoja? Wakawa na dini moja?
Ndio ujue hayo sio mafunuo ya Roho. Yesu Kristo hakuja kuanzisha dini, bali wanadamu walijaribu kutumia mafundisho yake kuanzisha dini. Dini ni mpango wa wanadamu kumwelezea Mungu ndio maana kuna tofauti ya mitazamo. Yesu Kristo alikuja kumfunua Baba kwa neno lake, kisha alitupatia Roho ambaye hutukumbusha na kutufundisha yote yatupasayo. Hizo diploma na digrii za theolojia hazina uhusiano na Roho Mtakatifu bali ni elimu za kibinadamu tu. Fahamu hilo
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Mkuu kuna sehemu nimeonesha dharau?
Au kuuliza swali na kwenyewe ni dharau?

Yesu alikuja akaondoka, (Labda angeendelea kuishi Milele hapa duniani) kwahyo sisi tusingefaidika lolote kwa kuja kwake...ila sasa wewe na mimi tulisikia habari zake kupitia Mathayo, Luka na Marko tumetofautiana, Wewe umekuwa Mlokole mimi nimekuwa msabato.
as long as you believe in Jesus Crist - your saved - hizo dini si chochote na hazikupi uzima wa milele ndugu.
 
Wapo maelfu ya watu wanaotumia akili zao kwa moyo wote kuutafuta ukweli na wengine wanaishia kuwa Mapadri,wengine wanasema ukweli ni kuitunza sabato,wengine wanasema Uislam ndio ukweli pekee nk. nk.

Sasa kwsababu wote mafundisho yao yanapingana kwa namna moja au nyingine, wote hawawezi kuwa sawa.

kuna makundi ya kidini yanayopishana mafundisho zaidi ya 50,000 (Kwa hizi Abrahamic religion)
Sasa Tuassume hapo ni kundi moja tu ndio lipo sahihi lets say Waislam wa kisunni tu,,,inamaana kuna makundi 49,000 yenye mabillioni ya watu yamepotoka.

Sasa hapa ndio hoja yangu ilipo, Hii njia ya vitabu inapotosha sana watu..Kwanini Mungu aliitumia??
Alikosa njia bora zaidi?
Mungu wa kweli ni mmoja na dini ya kweli ni Moja

Ikitokea binadamu ameshindwa Kumjua huyo Mungu wa kweli na dini ya kweli sio kama njia za Mungu zimefeli isipokuwa akili ya huyo binadamu ndio imefeli

Yani huyo binadamu amezidiwa ujanja na binadamu wenzake maana ukiondoa hiyo dini Moja ya kweli dini zilizobakia zote zimeanzishwa na binadamu

Yani binadamu wenzako wameanzisha dini alafu wakakuambia hii ndio dini ya Mungu na wewe ukakubali

Mwisho kabisa binadamu amepewa freewill na ndio maana amewekewa moto na pepo

Malaika hawana freewill na ndio maana wao maisha yao yote wanaishi peponi
 
Nani kakuambia kuwa Mungu anaweza kila kitu??, Mungu hawezi kuiba, hawezi kusema uongo, hawezi kudhulumu, hawezi kunyima haki ya mtu nk, Mungu HAWEZI kutenda mambo yote mabaya.

Ni hivi; Mungu amepanga na hakuna wa kupangua, amepanga kumuumba mtu na hatimaye huyo mtu aende akhera baada ya kufariki dunia na kufuliwa huko akhera, huko akhera kuna moto na pepo, katika moto wataingizwa wakosefu ili dhambi zao zichomwe na zikiisha ndipo wataingia peponi, ili mtu aingie peponi ni lazima afanye jitihada ya kushika mafundisho ya manabii (general case), mafundisho hayo ndio mengine yamehifadhiwa katika mfumo wa vitabu ili mtu asome na kuelewa Mungu anataka nini, kumekuwepo na mikorogano mingi katika kila dini juu ya hayo mafundisho hii inatokana na uelewa wa binadamu kuwa tofauti kwa kujua hilo ndipo Mungu kupitia dini ya kiisilamu akamtuma nabii mfuasi ili aje kufundisha dini sahihi ya Uisilamu, Uisilamu ulianzishwa na mtukufu mtume Muhammad (saw) na nabii wake Mfuasi ni Hadhrat mirza Ghulam Ahmad (as) nabii aliyeahidiwa kufika kuwaleta watu wa dini zote chini ya bendera ya Uisilamu, huyo nabii Mfuasi ndiye aliyeanzisha kwa amri ya Mungu jumuiyya ya Waisilamu wa Ahmadiyya duniani, Jumuiya hii imekuja kuvunja makundi ya dini zote duniani na kuwa kundi moja, hivyo ili kuondoa mtafaruku na miss understanding za mafundisho ya kidini hakuna haja ya kuja malaika wala Mungu kumuongezea mtu akili nk, kwani akili alizonazo binadamu Mungu mwenyewe ndiye kampa na anajua zinamtosha ili kujua neno lake.

Sasa ili umjue Mungu na mafundidho yake sahihi yasiyo na mkanganyiko ingia katika jumuiya ya Waisilamu wa Ahmadiyya .
Mungu Atakalo Huwa Na Hana Mshauri!
Kila kitu ni Mali Yake!
 
Back
Top Bottom