LATRA yatangaza ongezeko la nauli za Safari za Masafa Marefu na Mafupi kuanzia Desemba 8, 2023
Jitenge nae ili usijue matatizo yake!
Nani kati ya mawaziri aliyekuwa na maisha duni ili aujue mchungu wa maisha ya wananchi.
Wafanye masikini wa kutosha ili uweze kuwatawala.
Mdomdogo serikali inachukua hata kile kidogo walichonacho wananchi ili wawe tegemezi kwa serikali.
Mshahara kiduchu, waajiriwa wanalia leo unawaletea shida nyingine.
Tutegemee ufanisi mdogo kwa wafanyakazi wenye mishahara midogo.
Nauli za mijini huu ni mwiba mkubwa sana.

Tusubili tuone!
 
Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri Ardhini (LATRA) imetangaza mabadiliko ya nauli katika safari za masafa marefu na masafa mafupi baada ya kupitia maoni ya wadau wa usafiri nchini.

Kwa mujibu wa LATRA nauli za safari zisizozidi kilometa 10 ambayo nauli yake ilikuwa shilingi 500 sasa itakuwa 600. Kwa safari za kilometa 11 hadi 15 ambayo nauli yake ilikuwa shilingi 550 sasa itakuwa shilingi 700.

Kwa kilometa 15 hadi 20 ambapo nauli ilikuwa shilingi 600 sasa itakuwa 800 huku kwa safari za kilometa 21 hadi 25 nauli imetoka 700 hadi shilingi 900. Safari ya kilometa 26 hadi 30 nauli ni shilingi 1100, safari ya kilometa 31 hadi 35 ni shilingi 1300 na kilometa 36 hadi 40 nauli ni 1400.

Aidha nauli za wanafunzi zitaendelea kusalia 200 kwa safari za masafa mafupi.

Nauli za mabasi zimeorodheshwa kwenye jedwali hapa chini.

View attachment 2826735View attachment 2826734View attachment 2826733View attachment 2826732
Hii table imeandikwa ovyo ovyo sana. Angalia hapo Dodoma kwenda Iringa kupitia Mtera. Waiandike upya, waache ubabaishaji.
 
Hizo nauli hazitumiki Mkoa wa Mbeya,Sisi Mbeya dereva na kondakta ndo huamua nauli ziweje😁😁!
Nimepanda daladala nanenane nashukia Simike nauli ni tsh 1500!!

MBEYA HAYA HAYATUHUSU!NAULI ZILIPANDA MARADUFU HATA KABLA YA TANGAZO HILI.
MBEYA HAKUNA LATRA
 
Wanajamvi

LATRA imepandisha bei ya nauli ya mabasi na daladala wanasema ni kutokana na gharama za uendeshaji na bei ya mafuta kupanda hivyo basi wakakaa na wadau wa vyombo hivyo vya usafiri na kukubaliana upandaji huo wa nauli.

SWALI

1. Kwanini upandaji wa nauli unahusisha LATRA na wadau wa usafiri tu na kuwaacha abiria ambao ndio walaji na wahusika wakuu?

2. Tumeshuhudia mara nyingi LATRA wanapandisha bei ya nauli kila mara inapotokea mafuta yamepanda LAKINI huwezi kuwasikia wakishusha bei ya nauli inapotokea mafuta yameshuka bei.

LATRA tunaomba majibu au kama kuna mtu anaweza kueleza hili atujuze
 
Back
Top Bottom