Mwenge ni pepo na ibada ya kishetani kabisa ya kuabudu sanamu inapaswa kukemewa kwa nguvu zote Mungu atusaidie. Eti mwenge unaleta upendo, matumaini na vitu vingine uongo kabisa, ina maana mtu huwezi kuwa na upendo bila mwenge kupita? Au kuwa na matumaini kwa waliokata tamaa kwa ajili ya mwenge! Hebu tuache fikra potofu kabisa hizi. Na huu mwenge kuna watu wananufaika nao ndo maana kuna watu wanawashinikiza kwa nguvu kuchangia pesa, kwa hiyo ni kama mradi wa watu fulani hivi. Tafadhali chukua hatua, Tushirikiane kuutokomeza.