Mwenge wa Uhuru upo kwa faida ya nani?
Leo nilipokuwa katka eneo langu la kazi nilifanikiwa kuona msafara wa mwenge ukiwa umejumuisha magari mengi ya kifahari ya serikali na ulinzi wa hali ya juu. Nilipotoka kazini nilipita eneo ambalo mwenge huo umefikia na inasemekana utalala hapo, eneo hilo lilikuwa limepambwa na burudani za kutosha. Nikajikuta najiuliza je kuna umuhmu gani wa kutumia gharama kubwa kutembeza mwenge? Na sisi kama watanzania tunafaidika vipi na huu mwenge? Naombeni wadau mnijibu
 
Mwenge hueneza UKIMWI na magonjwa ya zinaa!

Rev, nami nililiwaza hilo maana nami pia nimekutana na mwenge asubuhi wakati nawahi kuwajibika, nikajiuliza hivi una faida gani? hizo gharama wanazotumia si zingefanya mambo mengine endelevu kwa Taifa.
 
Rev, nami nililiwaza hilo maana nami pia nimekutana na mwenge asubuhi wakati nawahi kuwajibika, nikajiuliza hivi una faida gani? hizo gharama wanazotumia si zingefanya mambo mengine endelevu kwa Taifa.

Matukio ya kitaifa (kama vile sherehe mbalimbali, kukimbiza mwenge, michezo, nk) huleta umoja, mshikamano na udugu! Swali ni kwamba, Je, umoja, msikamano na udugu vinasaidia kuleta maendeleo? Kama jibu ni ndiyo basi tuendelee kukimbiza mwenge wetu, otherwise tuachane nao!
 
Matukio ya kitaifa (kama vile sherehe mbalimbali, kukimbiza mwenge, michezo, nk) huleta umoja, mshikamano na udugu! Swali ni kwamba, Je, umoja, msikamano na udugu vinasaidia kuleta maendeleo? Kama jibu ni ndiyo basi tuendelee kukimbiza mwenge wetu, otherwise tuachane nao!

Mkuu sijaona bado huo umoja unaoletwa na huo mwenge, hivi tangu uanze kukimbizwa miaka hiyo nini umefanya? nisaidie hapo.
 
Hizo gharama zakuukimbiza zingetumika kununulia madawati kwa wanafunzi wanaokaa chini na kuwalipa walimu madeni yao tungekuwa tumefanya investment nzur sana kwenye elimu
 
Mkuu sijaona bado huo umoja unaoletwa na huo mwenge, hivi tangu uanze kukimbizwa miaka hiyo nini umefanya? nisaidie hapo.

Watu wa sehemu mbalimbali za nchi wanapo-interact for the common purpose inaleta umoja au wewe unafikiri umoja huletwa na nini?
 
Mwenge unaongeza ukimwi tu,wewe nenda sehemu ulipolala mwenge nenda siku ya 2 asubuhi utakuta watu wa usafi wa mji husika wanajaza gunia za kondom ambazo zimeshatumika,asimili 30 wanatumia kondom na asilimia 70 wanapiga pekupeku,je hapo kuna faida au kuna hasara ktk huo mwenge?
 
Matukio ya kitaifa (kama vile sherehe mbalimbali, kukimbiza mwenge, michezo, nk) huleta umoja, mshikamano na udugu! Swali ni kwamba, Je, umoja, msikamano na udugu vinasaidia kuleta maendeleo? Kama jibu ni ndiyo basi tuendelee kukimbiza mwenge wetu, otherwise tuachane nao!
Imetokea jana nikawa eneo la Mbauda Arusha ulipolala mwenge, lakini kwa hali niyoona jana hakuna cha umoja wala mshikamano, kwani watu wa sokoni waliendelea na biashara yao kama kawaida as if hakuna kinachoendelea, baa zikipiga muziki, wa kuita wateja, n.k. Wakati fulani mhamasishaji (au MC) iibidi afoke kidogo mwenge hoyeeee!!! Arusha Hoyeeeee!!! watu hawaitikii.... mara akasema "..... wanaotaka wanyooshe mikono (wakiitikia hoyeeee...) na wasiotaka waondoke tu..."
Ila sioni sana umuhimu wa kuwepo mbio za mwenge, kwani costs za magari tu ni nyingi. Bado sidhani kama kuna interaction ya kutosha kwani wakimbiza mwenge na wenyeji hawakutaniki sana, mbali na viongozi wa sehemu husika na baadae kupiga laga na muziki usiku kucha na ngono kwa kwenda mbele.
 
Watu wa sehemu mbalimbali za nchi wanapo-interact for the common purpose inaleta umoja au wewe unafikiri umoja huletwa na nini?

Sikubaliani na wewe, maisha yenyewe ya sasa yalivyo magumu kuna mtu kweli ana muda wa kwenda kushangaa mwenge? sasa huo ni umoja kweli?
 
Leo Asubuhi nimesikia Kiongozi wa Mbio za Mwenge Mwaka 2006 na ambae pia alipata kukimbiza Mwenge huo Nchini Msumbiji Mr Antony Mtaka akilalamika kuhusu watu wanaopiga vita mbio za Mwenge na kuwashutumu vijana ambao wanaonekana kutojua faida zake na kuwaona wanasiasa hasa upinzani japo hakuwataja, kama watu ambao wako mstari wa mbele kupinga mbio hizo za Mwenge.

Hakika mimi ni mmoja wa watu ambao kidogo nilipata kuona kidogo uzuri wa mbio za Mwenge miaka ya mwanzoni ya tisini nikiwa shule ya sekondari,na pia nimesikia simulizi zake, kuwa enzi ya Mwalimu Mwenge ulikuwa ukipita kwenye shirika la umma au ofisi yoyote ya Umma basi ukiondoka baada ya muda utaona mlipuko wa kusambalatisha watendaji wote ovyo waliokuwa wanashiriki kuyumbisha shirika au ofisi ya umma.

Hii inaonyesha ubunifu mzuri ambao Mwalimu kupitia wataalamu wake wa kutafuta taariifa za Serikali walimpomfikishia taarifa za matatizo ya watendaji wa Serikali na Mashirika basi yeye alitumia nafasi hiyo kurekebisha na kuwaadhibu viongozi hao huku wananchi wakiwa na ufahamu huo kupitia Mwenge kwa hiyo Wananchi walikuwa na kiu kila pale mwenge ulipopita ulizaaa matarajio ya wananchi hao.

Lakini leo wananchi wanaona Mwenge kama Ngeo na chombo cha mafisadi wa umma kujichotea fedh kupitia mfuko wa kuendeshea mbio hizo, na si alama ya Uzalendo na Umoja [Patriotism & Unity].Na pale ambapo Serikali imekosa Ubunifu wa kuwalithisha Watanzania vijana na watoto kuwa Mwenge ni Alama ya Umoja wa Umma na matokeo yake umekaa sana kisiasa badala ya kuwa ni KITAIFA na kuondoa ubinafsi wa chama tawala kuhodhi mbio hizo.

Umefika wakati mbio hizo kuludi kule kwenye mfumo wa utekelezaji wa Mwalimu wa kufumua na kuwafunga Mafisadi kuanzia ngazi ya kata, tarafa, wilaya ,Mkoa na atimae Taifa.Pia mbio hizo kuwa ni kitivo cha kuongoza na kuelimisha umma hasa vijana kupitia vipeperushi,elimu ya vitabu au majarida na sio kukusanya viongozi wa Serikali na kuanza kufukuzana nao huku na huku wakinyemelea posho kwa mgongo wa Mwenge.

Na Mwenge huo ukimbizwe na vijana kutoka kada zote na vyama vyote na sio vijana wa CCM tu,Wachaguliwe vijana wakakamavu kutoka CCM,CDM,CUF,NCCR na hata vyama vya Kitaaruma Vyuo na Shule za Sekondari na Msingi kuonyesha kuwa ni Kikundi cha kitaifa na mbio za kitaifa na sio kuwa ni Mali ya CCM.

Maoni yangu mimi kama Kijana tunauitaji Mwenge huo kama alama ya umoja ambako kila unakopita unatukumbusha na kutuhamasisha kama Taifa moja nje ya vyama vyetu vinavyotwambia kuwa wewe ni MwanaCCM na yule ni Mwana CDM na Kaka yake nani yeye Ni CUF.

Ila naungana na wadau wote wanaopigania mabadiliko na mageuzi ya uendeshaji mbovu wa sura ya MBIO HIZO ambao ndipo umekaa KIFISADI kiasi kuwa unaunda chuki dhidi ya wananchi na Mwenge huo.Tunaitaji kubadilisha mfumo wa kukimbiza mwenge wa kizamani na kuweka katika mfumo unaokubalina na kizazi kipya cha vijana wa kuaniza miaka ya sabini na kushuka chini yaani uwe Moden Torch of Freedom.

Nawasilisha

b00vhfwt_640_360.jpg
Hati ya Uhuru wa Tanzania na Mwalimu Julius K Nyerere [By Then Tanganyika]

a9c2c197e6e56f0069838c9b148684a4_1M.png.jpg
Marehemu Baba wa Taifa Julius Kambarage Nyerere

nyirenda-5.jpg
Marehemu Meja Alexander Gwebe Nyirenda akipokea Mwenge.
nyirendabc.jpg
Marehemu Meja Alexander Gwebe Nyirenda akipandisha Mwenge Juu Ya Mlima Kilimanjaro

torch_large.jpg
Mwenge wa Uhuru Nadni ya Shilingi Moja
View attachment 39494
Ngao ya Tanzania [coat of arms] yenye Mwenge wa uhuru
 
Hata mie nimemuona na kumsikia staili yake sikuipenda imekaa kimaslahi zaidi.Ukiona jambo linalalamikiwa na watu ujue lina kasoro.Mauthui mazuri ya mwenge yanaharibiwa na hali halisi ya nchi hivi sasa.Wale wanaopenda mambo ya kinafiki wanaona ni sawa kukimbiza mwenge na mambo mengine machafu yanaendelea.Hata huyo aliyeanzisha huo mwenge angekuwepo asingekebali maana hakuwa mnafiki kama viongozi wetu wa leo.
 
  • Thanks
Reactions: DSN
Kwa sasa Mwenge hauna faida yoyote kwa wananchi zaidi ya kuongeza matumizi ya Fedha za walipa kodi wa nchi hii bure!!!
 
Kwa sasa Mwenge hauna faida yoyote kwa wananchi zaidi ya kuongeza matumizi ya Fedha za walipa kodi wa nchi hii bure!!!

Mkuu Uzalendo wa Taifa hauna kipimo cha gharama
 
Na Mwenge huo ukimbizwe na vijana kutoka kada zote na vyama vyote na sio vijana wa CCM tu,Wachaguliwe vijana wakakamavu kutoka CCM,CDM,CUF,NCCR na hata vyama vya Kitaaruma Vyuo na Shule za Sekondari na Msingi kuonyesha kuwa ni Kikundi cha kitaifa na mbio za kitaifa na sio kuwa ni Mali ya CCM.

Hii imekaa vizuri mkuu!
 
  • Thanks
Reactions: DSN
Back
Top Bottom