Eti serikali sikivu, kipindi wanaweka hizo tozo uliita jina gani? Serikali Kuweka tozo au hata kodi Kisha kutambua zinaumiza wananchi na kuziondoa huonesha ni namna gani tulivyo na MANANGA katika wizara husika Wala sio usikivu.

Kama wanania njema na pesa za watz wapunguze matumizi kwa vitendo, in this poor country ambayo wewe mleta mada upo serikali unayoiita sikivu inatumia zaidi ya 400 billions Kila mwaka kununua V8 ambazo ni kodi za wananchi.

Acha kushabikia Kila kitu tafakari kwanza, sio sikivu sikivu......
 
Leo tar 20 mpk tar 1oct ni siku 10.
Hizo siku 10 tozo zitakazokusanywa itapigwa abla-kadabla shot-kulia zote ndani mumfuko.
Ndio ianze sheria mpya.
Na hizi ndiyo tabia za watu wenye roho mbaya na mafisadi! Ingekuwa tozo zimeongezwa zingeanza mara moja lakini kwa kuwa Mwigulu anataka kukomoa watu basi amepanga mabadiliko yaanza baada ya siku 10 na ndiyo furaha yake!
 
Kusamehe tozo ya miamala kwenye utoaji wa fedha taslimu kupitia wakala wa benki yaani ATM kwenye miamala yenye thamani ya chini ya tsh 30,000/=
Hiki ni kiini macho maana wanajua watarecover hiyo deficit kwenye miamala inayozidi hiyo 30,000/- . Huu ni ujambazi
 
Alieanzisha Tozo ni Nani!?anaezifuta ni Nani!? Mi Binafsi nina UWEZO wa kuongoza Hii NCHI bila Tozo!!

Tumeshawazoea tabia yao ni hii hapa;-

"Tengeneza Tatizo tatua tatizo halafu jipigie makofi"!

Nakazia

Rasimu ya Warioba irudi mezani SASA iwe KATIBA MPYA
 
Ushangiliaji wa Wabunge wa CCM leo kwa Dr Mwigullu Nchemba hakukuwa ule uliozoeleka, wameshangilia Kinyonge sana kana kwamba wanalazimishwa

Sijaelewa sababu au ndo makundi yashaanza!!

Karibu Tanzania TAL soma Exodus 14:14
 
Mwalimu ndie akikuwa ana jali dhamana aliyo kuwa nayo kwa watu wake
 
Wao si ndio inasemekana wamepitisha, sasa waziri amefuta bila maridhio ya waliopitisha. Lazima wawe wanyonge tu
 
HAKUNA BUNGE KUNA KUSANYIKO LA WATU SIJUI WANAFANYA NINI HUMO, WANAKIJUA WAO WANACHOKIFANYA .
 
Miamala iliyosamehewa inawafeva watu Wa kundi lipi? Je hyo miamala ndo yalikuwa malalamiko makuu au ya awamu ya pili?

Au atusaidie dr, kwan hitaji la msingi haawa ni kufutwa tozo au kuondolewa? Hebu tujiulize kdg tu toza za miamala ya sim zipo toka Mwaka, ila za mabenk miezi 2 tu wamefanyia kazi au kwa kuwa wanotumia bank ni wao?

Kunatitzo kwenye think tank.
 
SHERIA INASEMAJE KUHUSU KUKATA KODI TOKA CHANZO KIMOJA CHA MAPATO YAANI MSHAHARA

Kuhusu wafanyakazi wenye chanzo kimoja cha mapato yaani mshahara, mnakubali kulazimishwa kuhangaika kutoa miamala chini ya Tsh. 30,000 ili msifyekwe tozo


TUCTA wanasemaje kuhusu kuwatetea wafanyakazi wasipate usumbufu au kukatwa tozo pale wanapolazimika kutuma miamala au kutoa pesa zaidi ya Tshs. 30,000

 
Wana maombi ya jf tupange siku za kufunga kumlaani,

Vinginevyo afute tozo zote
 
Hata makato ya simu yamepunguzwa kutoka elf 7 mpaka elf 4
 
Na Dr Steve Nyerere nae anasemaje kuhusu kufutwa kwa tozo kiaina!!??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…