Uchaguzi 2020 NEC yamuita Tundu Lissu kufika mbele ya Kamati ya Maadili ya Taifa

Salaam wana jamvi,leo ni Siku ambayo Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo anatakiwa kufika mbele ya Kamati ya Maadili.

Pamoja na mambo mengine yawezekana Kamati ya Maadili ikamkuta na kosa kulingana na kanuni za uchaguzi, kutokana na hili naomba NEC was one beak at any a kosa Kwa kumpa adhabu ya kumsimamisha kufanya kampeni. Maana Kwa kufanya hivyo watakua wanamuongezea umaarufu na nguvu zaidi kwenye kampeni zinazoendelea.

Nawasilisha.
 
Ni kesho tarehe 29/9/2020
 
Wacha wampe adhabu ya kumsimamisha waone kama watu ndo watampenda magufuli. Wamenyima upinzani coverage ya media, kutumia chopper na hata posters kutoza kodi ili magufuli abaki peke yake, umeona wananchi wamempenda?

Kwanza watu wakiona picha sake barabarani wanasonya tu na kutukana. Zinaudhi mnoo badala ya kushawishi. Magufuli hapendeki hata kidogo.

Wakimsimamisha watu ndo watamtafuta alipo kwa miguu. Magufuli katendea watu ubaya mkubwa. Yote haya yanayomkuta kuna damu na machozi ya MTU aliyedhulumiwa yanamliliaaaa.
 
Mabibi na mabwana ni muhimu tume ikakumbuka kuwa wagombea ni wa wananchi si wa tume.

Mengi yamevumiliwa lakini hayatavumilowa yote...

Tume ya uchaguzi inataka kuhatarisha amani ya nchi.
 
Kumbe hata huru hujui maana yake? Muulize Jecha aliyechukua fomu za kugombea uraisi kupitia CCM , atakuambia

Ni kama mnacheza mechi , Yanga na Simba halafu Simba itoe mchezaji wake ndio awe Referee wa mechi , umeona wapi mambo hayo ???
Bado haujajibu swali langu,ngoja nilibadilishe kidogo labda utalielewa. Hiyo time huru ichaguliwe kutoka wapi ili kuepuka unazi wa vyama vya kisiasa ndani yake? Maana ikitokea uteuzi hapa jf,tayari wewe ni lazima utakaa upande wa CHADEMA, Sasa hao watu wa tume tuwatoe wapi?
 
Mabibi na mabwana ni muhimu tume ikakumbuka kuwa wagombea ni wa wananchi si wa tume.

Mengi yamevumiliwa lakini hayatavumilowa yote...
Maskini!

Eti mtaenda nae.
 
NEC Kuanza kudeal na Lisu kipindi hiki nikumfanyia promo.
 
Tume ya uchaguzi inataka kuhatarisha amani ya nchi.

Ni vizuri wakajua kuna limit.

Sirro na Juma so far so good. Ila tume kwa kweli pana mambo yana ukakasi sana tokea kwenu. Jaji Kaijage, ni vyema mkajitathimni. Haya mambo;
1. Kuengua wagombea
2. Kuachia baadhi ya wagombea kutumia lugha za makabila majukwaani
3. Kuita wagombea wengine majina ya kichochezi
4. Kuchochea wananchi dhidi ya wagombea wengine. Kumwita mgombea kuwa ni kibaraka majukwaani ni jambo la hatari sana
5. Yapo mengi

Tume itoshe kukwambieni safari hii tumedhamiria kweli kweli kila mtu na afanye sehemu yake;
 


Kwa hivyo hata Yanga na Simba wakicheza mechi , Simba wakichagua Referee itakuwa hatopendelea Simba ?? na Yanga waendelee kucheza tu?

Hivi Jecha alipoutia mpira kwapani alipendelea timu gani? baadaye naye akachukua Fomu za kugombea uraisi kupitia CCM?
 
Usipotumia vizuri akili zako, kuna watu kwa kukusaidia watatumia akili zao kukuamulia!
 
Kwa hii kasi ya Lissu inahitaji kifua kuivumilia naona CCM wameanza kushika shati baada ya kuzidiwa mbio.

Ile kauli ya Bashiru kuwa tutatumia Vyombo vya dola kubaki madarakani naona wamenza kuifanyia kazi...
Ninaposoma maandishi kama haya toka kwa mchangiaji kama huyu, ninaanza kuwa na matumaini makubwa juu ya Tanzania yetu.

Watabaki watu walioharibika beyond repear kama akina 'Wakudadavua, jinga, Magonjwa, Paskali' na wengine wachache wa aina hiyo.
 
Ikiwa hakuna sehemu yeyote ndani ya Tz tunaweza kupata mtu mwenye sifa za kuingia kwenye time,na ambae sio mnazi wa chama fulani,dhana ya time huru Ni ngumu sana kutekelezeka,hata kama hawatateuliwa na Rais. Otherwise watumike robots.
 
Malalamiko ya Tundu Lisu anapaswa kuyaelekeza ama kwa serikali au kwa bunge linaloisimamia serikali lakini siyo kwa Dr Magufuli kama mgombea.

Lisu anapaswa kuzilalamikia sera za CCM kama anaona zimefeli maana kinachoshindanishwa sera za vyama siyo watu.

Huu mtindo wa kushambulia watu binafsi tusipoukemea utatufikisha pabaya.
Yuko wapi Sadiffa aliyekuwa anamzushia Lowassa kila aina ya uzushi?
Siasa siyo uadui wagombea mnapaswa kuheshimiana.

Johnthebaptist leo Iringa mjini.

Maendeleo hayana vyama!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…