Njoo huku tuswali Sunnah,hatubadili kitu huku hakuna mwenye mamlaka hayo
Ukinionyesha hukumu aliyo hukumia Allah kwa wanaume wanaopumuliana nitakuja tuswali wote!
Allah anasema!
[emoji116][emoji116]

وَٱلَّٰتِى يَأْتِينَ ٱلْفَٰحِشَةَ مِن نِّسَآئِكُمْ فَٱسْتَشْهِدُواْ عَلَيْهِنَّ أَرْبَعَةًۭ مِّنكُمْ ۖ فَإِن شَهِدُواْ فَأَمْسِكُوهُنَّ فِى ٱلْبُيُوتِ حَتَّىٰ يَتَوَفَّىٰهُنَّ ٱلْمَوْتُ أَوْ يَجْعَلَ ٱللَّهُ لَهُنَّ سَبِيلًۭا ﴿١٥﴾

Na ambao wanafanya uchafu miongoni mwa wanawake wenu, washuhudizieni watu wane katika nyinyi. Watakapo shuhudia, basi wazuieni majumbani mpaka wafishwe na mauti au Mwenyezi Mungu awatolee njia nyengine.

وَٱلَّذَانِ يَأْتِيَٰنِهَا مِنكُمْ فَـَٔاذُوهُمَا ۖ فَإِن تَابَا وَأَصْلَحَا فَأَعْرِضُواْ عَنْهُمَآ ۗ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ تَوَّابًۭا رَّحِيمًا ﴿١٦﴾

Na wawili kati yenu wafanyao hayo waadhibuni. Na wakitubia wakatengenea basi waacheni. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kupokea toba, Mwenye kurehemu

Yaani hata huku kwetu uswazi unaitwa mchezo wa kisilamu![emoji28]
 
Wasiotoa michango ya Jumuia mnawatenga na Padri anagoma hata kuwafanyia IBADA YA MAZIKO (japo haina msaada kwa Marehemu) ,,,iweje leo ghafla muwapende MASHOGA eti tusiwatenge [emoji23][emoji23]
Kambishie Mungu mimi nimemnukuu tu!
Dhahir eeh?!
 
Hiyo Aya ya pili inazungumzia wanaume,si kila dhambi Ina hukumu yake duniani,hakuna adhabu ya muongo,mfitini,mchawi duniani Ila atahukumiwa akhera,ukitaka kujua zaidi kuhusu uislam na ushoga ambao mmehalalisha mtafute nabii lut(lutu/lot) kwenye Qur'an...
 
Umeeleza Vizuri sana.Nadhani wa kukuelewa amekuelewa.
 
Inahitajika akili kubwa sana kumuelewa Papa Francis otherwise utahisi anapotosha.
 
Hukumu ishatoka hapo, Allah anasema waadhibuni na wakitubu na kutengenea WAACHENI!
Kwenye zina hamna wepesi!; Lat qarab zina!
Dhahir eeh!
 
Huyo Papa nina Uhakika 100% ni Shoga.
Yesu Ameonya!
[emoji116][emoji116]
Matthew 7:1-5
[1]Msihukumu, msije mkahukumiwa ninyi.

[2]Kwa kuwa hukumu ile mhukumuyo, ndiyo mtakayohukumiwa; na kipimo kile mpimiacho, ndicho mtakachopimiwa.

[3]Basi, mbona wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe huiangalii?

[4]Au utamwambiaje nduguyo, Niache nikitoe kibanzi katika jicho lako; na kumbe! Mna boriti ndani ya jicho lako mwenyewe?

[5Mnafiki wewe, itoe kwanza ile boriti katika jicho lako mwenyewe; ndipo utakapoona vema kukitoa kile kibanzi katika jicho la ndugu yako. Kutweza Kitakatifu

Paulo Mtume wa Yesu Amekazia!
[emoji116][emoji116]
1 Corinthians 4:1,3-5
[1]Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu.

[3]Lakini, kwangu mimi, si kitu kabisa nihukumiwe na ninyi, wala kwa hukumu ya kibinadamu, wala sijihukumu hata nafsi yangu.

[4] Maana sijui sababu ya kujishitaki nafsi yangu, lakini sihesabiwi haki kwa ajili hiyo; ila anihukumuye mimi ni Bwana.

[5]Basi ninyi msihukumu neno kabla ya wakati wake, hata ajapo Bwana; ambaye atayamulikisha yaliyositirika ya giza, na kuyadhihirisha mashauri ya mioyo; ndipo kila mtu atakapoipata sifa yake kwa Mungu.
 
Binafsi sijaona kosa la Papa hapo yeye alichomaanisha ni kuwapenda hao watu na kutowatenga ingawa wanatenda dhambi mbele za Mungu, lakini hakuna mwenye haki mbele za Mungu.

Wote sisi ni watenda dhambi na machukizo mbele za Mungu sema machukizo yetu yanatofautiana. Na yeye kama kiongozi wa kanisa aliwaadress viongozi wasitumie sheria za kawaida kuwanyima watu hao kwenda kanisani.

Embu ndugu zangu tuongee ukweli, kwenye kanisa wote tuko sawa ni watoto wa Mungu pamoja na mapungufu yetu wote tunatakiwa kwenda mbele za Mungu kutubu na kumuomba pia. Hivyo sidhani kama ni vyema kanisa likafukuza watu kutokana na dhambi zao. Huyu anaweza kuwa na dhambi ya ushoga, yule akawa na dhambi ya uzinzi, huyu anaweza kuwa na dhambi ya uwizi yule akawa na dhambi ya utoaji mimba, usengenyaji uonevu, unyanyasaji na utapeli. Hivyo tukifukuza shoga kanisani kwa nini tusifukuze na hao wadhambi wengine au kwa kuwa ni vigumu kuwatambua?

Tunachokishangaa kwa Papa hivi leo hatatukuwa tofauti na Yesu alivyoshangawa na mafarisayo pale alipokwenda kuosha miguu ya makahaba.
 
Utafanya je jambo kuwa la haki kisheria halafu tena utake litubiwe?
Papa anatunga sheria za nchi? Kila serikali ipambane na sheria zake, isitafute kichaka. Kiroho itashughulikiwa na taasisi za dini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…