Prof. Mukandala: Matokeo ya Rais yahojiwe Mahakamani
Watanzania tuna mambo,eti tunaridhia na kumuomba MTU aliyopo madarakani ndio arekebishe Katiba na aturuhusu kufanya mikutano ya kisiasa.
Kwa kweli sisi ni matahira wa mwisho Duniani.
Tunataka uhuru wetu na Taifa letu pia. Tatizo letu ni mahakama ya Tanzania imejaza watu wasio huru. Hili jambo lingemalizwa na mahakama lakini yenyewe huwa inajifanya haijui ifanye nini.
 
Kuna kitanzi kinataka kuning'ing'izwa hapo ili jamaa waende na maji.😁.

"Msajili wa vyama aandae muongozo wa chaguzi za ndani za vyama vya siasa".
 
Kauli za rais zinavunja moyo.
Kikosi kazi kimefanya kazi nzuri sana
 
Hili ni moja kati ya mambo ya kawaida ambayo kwa akili za kawaida za mwanadamu hayakutakiwa kuzungumziwa kabisa kwenye huu ulimwengu tuliopo.

Lakini kwasababu tumeamua kujirudisha nyuma kama taifa, ndio maana zaidi ya mwaka mzima tumekuwa tukipigia kelele jambo la kisheria liruhusiwe kufanyika!

Mimi nataka nione kama atatangaza kuanza huo mchakato wa Katiba Mpya, na hiyo Katiba yenyewe itakuwa ni ipi? Rasimu ya Warioba au ile Pendekezwa?

Kutoka hapo ndio tutajua hili taifa linaelekea wapi, kama ni kuendelea kuzunguka mbuyu kama kawaida yetu, au tutaamua kusonga mbele.
Kama walikaa karibu mwaka mzima kujadili hizi hoja 18 ambazo hazina mashiko siyo jipya zaidi ya matumizi mabaya ya fedha za umma.
 
Watanzania tumepigwa na kitu kizito kisigoni hatujui ni kipi kitatokea

Hakuna jipya hapo yote ni blaah blaah zakusogeza siku Ili 2024&2025 zifike na wanaojiona wanahati miliki ya nchi wachukue vyao

Kuna ugumu gani Kwa mh rais kuhuisha rasimu ya warioba ? Gharama za tume hii busara tu wangenyofoa kipengele Cha aina ya muungano mengine yote wakayaacha kama yalivyo na inakuwa katiba

Inatia hasira nchi hii kweli eti ,jambo dogo linachukua miezi kumi ?

Na hao mnajiita mpo kwenye maridhiano tayari mmekwisha kupoteza tayari. Jiulize swala ambalo lipo kisheria tayari nalenyewe kamati inashauri ifunguliwe kipindi hicho sheria inaitambua .

CHADEMA kazi kwenu kuendelea na maridhiano ambayo nayo yatachukua miezi kumi au mjitoe
 
CHADEMA kazi kwenu kuendelea na maridhiano ambayo nayo yatachukua miezi kumi au mjitoe
Mara nyingi CHADEMA inakuwa kama iko juu kileleni na inataka kuangukia ama kwenye mwamba au kwenye ardhi ngumu. Maridhiano ni muhimu, lakini CHADEDMA inapata nini na inapoteza nini, ndiyo jambo la kujadili.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akipokea Ripoti ya Kikosi Kazi cha Kuratibu Maoni ya Wadau wa Demokrasia ya Vyama Vingi vya Siasa Ikulu jijini Dar es Salaam leo tarehe 21 Oktoba, 2022



Mapendekezo 18 ya Ripoti yanasomwa na Prof. Rwekaza Mukandala
  1. Kikosi kazi kinapendekeza mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa iruhusiwe kufanyika kwa mujibu wa katiba na sheria, mikutano ya ndani ya vyama vya siasa iendelee kufanyika bila vikwazo vyovyote, yafanyike marekebisho ya sheria ili kuhakikisha mikutano ya hadhara inafanyika kwa ufanisi.
  2. Sheria ya vyama vya siasa ifanyiwe marekebisho ili kulipatia baraza la vyama vya siasa linaloundwa na vyama vyenyewe mamkala ya kushughulikia swala la uvunjifu wa maadili ya vyama vya siasa kupitia kamati yake ya maadili, msajili wa vyama vya siasa aandae muongozo wa chaguzi za ndani za vyama vya siasa.
  3. Mfumo wa sasa wa kugawa ruzuku kwa vyama vya siasa uendelee, isipokuwa 10% ya fedha zinazotolewa sasa zitolewe kwa mgawanyo sawa kwa vyama vyote vyenye usajili kamili.
  4. Tume ya taifa ya Uchaguzi isilazimike kufuata amri au maagizo ya mtu yeyote, idara yoyote ya serikali, chama chochote cha siasa, taasisi au asasi yoyote na utendaji wake uruhusiwe kuhojiwa kwenye mahakama ya juu ili kuongeza uwajibikaji wa tume.
  5. Wajumbe wa tume ya taifa ya uchaguzi wateuliwe na kamati inayoongozwa na jaji mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (mwenyekiti) jaji mkuu wa Zanzibar (M/mwenyekiti), kamishna wa serkretarieti ya maadili ya viongozi wa umma Tanzania bara, mwenyekiti wa tume ya maadili ya viongozi wa umma ya Zbar, mwenyekiti wa tume ya haki za binadamu na wajumbe 2 watakaoteuliwa na jaji mkuu wa JMT baada ya kupendekezwa na chama cha wanasheria Tanganyika na chama cha wanasheria Zbar. Pia, angalau wajumbe wawili wa uteuzi wawe wanawake, sifa za kuwa mwenyekiti, makamu au mjumbe ziainishwe, nafasi za ujumbe zitangazwe, watu wafanyiwe usaili kisha majina yapelekwe kwa Rais kwa uteuzi
  6. Matokeo ya Rais jahojiwe kwenye Mahakama ya juu
  7. Wasimamizi wa uchaguzi wazingatie sheria, maadili, weledi, uwazi na ushirikishwaji wa wadau wakati wa kufanya kazi zao. Wasimamizi watakaokiuka taratibu wawajibishwe kwa mujibu wa sheria.
  8. Tume ya taifa ya uchaguzi ipewe fedha kwa wakati ili iweze kutelekeza majukumu yake ipasavyo.
  9. Itungwe sheria kusimania shughuli za tume ya uchaguzi, pia iwepo sheria moja ya kusimamia chaguzi zote badaa ya uwepo wa sheria mbili kama sasa, maafisa wa uchaguzi watakao engua wagombea kushiriki uchaguzi bila kuzingatia sheria na weledi wawajibishwe kwa mujibu wa sheria.
  10. Matumizi ya tehama kwenye uchaguzi yaboreshwe na kuongezwa.
  11. Sharti ya uwepo wa sera ya jinsia liwepo kwenye kila chama cha siasa, na ujumuishi wa makundi maalumu, pia ushiriki wa jinsia moja kwenye vyombo vya maamuzi isipungue 40%. Pia, utaratibu wa uwakilishi wa viti maalumu kwa wanawake uendelee, isipokuwa sheria ziboreshwe kuweka ukomo wa miaka 10 pekee.
  12. Sheria zinazokwamisha ushiriki wa wa watu wenye ulemavu kwenye siasa ziangaliwe upya
  13. Juhudi za ushirikishwaji wa vijana kwenye siasa ziongezwe
  14. Serikali iongeze utoaji wa elimu ya uraia, pia ifundishwe kwenye ngazi zote za elimu, pia mtaala wa elimu uzingatoe elimu ya uraia.
  15. Swala la rushwa litamkwe katika katiba ya nchi ili wananchi watambue kuwa vitendo vya rushwa havitavumiliwa wala kuonewa muhali.
  16. Kuanzishwe utaratibu wa mijadaa kila mwaka itakayohusisha viongozi wakubwa wa kitaifa na kisiasa ili kudumisha mshikamano, mahakama iwe ni mamlaka ya mwisho ya kuamua pindi maridhiano yanapokwama
  17. Wanahabari waunde chombo cha kusimamia wanahabari na vyombo vyao, vyombo vya umma vitoe muda sawa wa kutangaza habari za wagombea wa vyama vyote kwa usawa, uwepo mchakato wa wazi wa kuwajibisha vyombo vya habari badala ya kufungiwa pekee na mkurugenzi wa habari na mawasiliano
  18. Mchakato wa katiba mpya uendelee, hata hivyo mjadala wa kitaifa kuhusu katiba mpya uanze kabla ya kuanza kwa mchakato wa kuandika katiba mpya ili kujadili maswala ya msingi kama muungano, mamkala ya Rais, madaraka ya serikali za mtaa, Rushwa, mfumo wa uchaguzi n.k. Pia, sheria ya mabadiliko ya katiba na sheria ya kura ya maoni zihuishwe pamoja na kuundwa kwa jopo la wataalamu ili kufanya mapitio ya katiba inayopendekezwa kwa kuzingatia hali ya sasa ya kiasiasa, kiuchumi na kijamii.
Maneno ya Rais Samia Suhuhu Hassan
Kazi hii imechukua miezi 10, haikuwa rahisi. Pengine ningewaacha ingechukua zaidi ya muda huu, lakini mimi pia navutwa shati.

Tumepokea, na kama mlivyoona ripoti yenu ina mambo kadhaa, sisi kwenye serikali inabidi tujipange vikosi kadhaa, na wengine kati yenu tutawaomba mje kwenye vikosi kazi hivyo tujadili.

Siyo kwamba leo tumepewa ripoti ya kikosi kazi, kesho tutaanza kutekeleza hapana. Tumepokea, na wananchi wasikie tumepokea na tutafanyia kazi.

Na nyie watu wa siasa mjichambue, ni kazi ya jaji mtungi na watu wake. Nakubailiana na hoja ya 40% ya wanawake kwenye vyama vya siasa.

Tumepokea marekebisho ndani ya vyama vya siasa na wenyewe wasiwe mahodari wa kuirekebisha serikali lakini na wenyewe ndani tutizame je wanavyokwenda mambo ya usawa wa kijinsia yapo, mambo ya matumizi mazuri ya fedha yapo na mwengine akipata chama cha siasa anasema ni chake

Mgao wa ruzuku tutauangalia, hatuwezi kusema tutaongeza fedha zaidi sababu ni swala la kibajeti.

Matumizi ya teknolojia kwenye tume ya uchaguzi ni muhimu, ili teknolojia inayotumika iweze kutoa matarajio ambayo watu wanataka.

Tume ya uchaguzi tutalikalia kitako, ya serikali yatakwenda na ya ripoti nayo tutayaangalia.

Mijadala ya kisiasa kila mwaka iwepo, kaeni mjijadili, msijadili tu serikali, mjijadili na ninyi wenyewe. Mijadala heathy, hata serikali inaweza kuwezesha mijadala hii.

Wanawake mara nyingi nafasi muhimu wakigombea wanaambiwa kaa upande, au wanaambiwa njoo chukua hiyo gombea. Ukikuta wanawake kawekwa ni mwepesi mno, kapangwa kumsindikiza mtu. Kwa hili nakubaliana nao, ni pamoja na kuwasomesha wanawake, kuwatia moyo kwamba wanaweza.

Rushwa ni kidonda ndugu, hakuna hata chama kimoja kimenusurika hapa. Hakuna chama ambacho hakifanyi, nadhani ni tabia ambayo tunatakiwa kuibadilisha. Watu wajue, kuchaguliwa si mimi, ni chama. Hili la Rushwa, tujitazameni sote.

Maswala ya mikutano hakuna anayekataa, lakini lazima kuwe na jicho. Hatutaki kurudi tulikotoka, polisi wataanza tena kupiga watu. Tunaposema kwamba kanuni lazima tuzitazame siyo kwa nia mbaya, ni nia njema. Lazima tutazame kanuni na sheria ndipo turuhusu.
Mfumo mzuri wa uaandaji.. tusibir serikali ifanye maamuzi yake...
Ila kama mama akikubali hili na kabadili katiba.. bas atawekwa kwenye kumbukumbu kubwa ya tz hii
 
Wajumbe wa tume ya taifa ya uchaguzi wateuliwe na kamati inayoongozwa na jaji mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (mwenyekiti) jaji mkuu wa Zanzibar (M/mwenyekiti), kamishna wa serkretarieti ya maadili ya viongozi wa umma Tanzania bara, mwenyekiti wa tume ya maadili ya viongozi wa umma ya Zbar, mwenyekiti wa tume ya haki za binadamu
Je, Hawa sio wateule wa rais?(ambaye ni m/kiti wa ccm/chama Cha siasa). Hii haitakuwa sawa na kutwanga maji kwny kinu?
 
Dominated power ya tawala hata iundwe mahakama chini ya mwamba bado mgombea wa tawala atapita tu!

Kitu kimoja ninachojifunza, hasa nikiangalia haya yanayoendelea na akili za oppositions wetu, tawala wapo smart sana sana! Huku kwenye porojo tunawapopoa lakini ndani wamejipanga in a very complicated system.

Kama hujanielewa angalia game ya Al hilal vs Yanga! Yanga walitawala mchezo lakini hawakucheza kufuzu, Al Hilal hawakutawala lakini walicheza kufuzu! Ndicho wanachofanya tawala.

Sometimes wanaacha mpige kelele hadi mhisi mnabeba nchi saa mbili asubuhi lakini wanajua mwisho wa utawala wenu ni kwenye kelele huku wao wanashinda na kuwaacha muendelee kupiga kelele! Mnapewa viti vya uwakilishi huko dom kuwapoza, viongozi wa upinzani na wawakilishi wa dom wanapewa vi safari na viposho posho wana enjoy life huku wakiunda vikundi vya kupiga kelele mitandaoni kulinda nafasi zao!

Mfumo wa sihasa uko very corrupted! Tunadanganyana majukwaani tu!
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akipokea Ripoti ya Kikosi Kazi cha Kuratibu Maoni ya Wadau wa Demokrasia ya Vyama Vingi vya Siasa Ikulu jijini Dar es Salaam leo tarehe 21 Oktoba, 2022



Mapendekezo 18 ya Ripoti yanasomwa na Prof. Rwekaza Mukandala
  1. Kikosi kazi kinapendekeza mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa iruhusiwe kufanyika kwa mujibu wa katiba na sheria, mikutano ya ndani ya vyama vya siasa iendelee kufanyika bila vikwazo vyovyote, yafanyike marekebisho ya sheria ili kuhakikisha mikutano ya hadhara inafanyika kwa ufanisi.
  2. Sheria ya vyama vya siasa ifanyiwe marekebisho ili kulipatia baraza la vyama vya siasa linaloundwa na vyama vyenyewe mamkala ya kushughulikia swala la uvunjifu wa maadili ya vyama vya siasa kupitia kamati yake ya maadili, msajili wa vyama vya siasa aandae muongozo wa chaguzi za ndani za vyama vya siasa.
  3. Mfumo wa sasa wa kugawa ruzuku kwa vyama vya siasa uendelee, isipokuwa 10% ya fedha zinazotolewa sasa zitolewe kwa mgawanyo sawa kwa vyama vyote vyenye usajili kamili.
  4. Tume ya taifa ya Uchaguzi isilazimike kufuata amri au maagizo ya mtu yeyote, idara yoyote ya serikali, chama chochote cha siasa, taasisi au asasi yoyote na utendaji wake uruhusiwe kuhojiwa kwenye mahakama ya juu ili kuongeza uwajibikaji wa tume.
  5. Wajumbe wa tume ya taifa ya uchaguzi wateuliwe na kamati inayoongozwa na jaji mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (mwenyekiti) jaji mkuu wa Zanzibar (M/mwenyekiti), kamishna wa serkretarieti ya maadili ya viongozi wa umma Tanzania bara, mwenyekiti wa tume ya maadili ya viongozi wa umma ya Zbar, mwenyekiti wa tume ya haki za binadamu na wajumbe 2 watakaoteuliwa na jaji mkuu wa JMT baada ya kupendekezwa na chama cha wanasheria Tanganyika na chama cha wanasheria Zbar. Pia, angalau wajumbe wawili wa uteuzi wawe wanawake, sifa za kuwa mwenyekiti, makamu au mjumbe ziainishwe, nafasi za ujumbe zitangazwe, watu wafanyiwe usaili kisha majina yapelekwe kwa Rais kwa uteuzi
  6. Matokeo ya Rais jahojiwe kwenye Mahakama ya juu
  7. Wasimamizi wa uchaguzi wazingatie sheria, maadili, weledi, uwazi na ushirikishwaji wa wadau wakati wa kufanya kazi zao. Wasimamizi watakaokiuka taratibu wawajibishwe kwa mujibu wa sheria.
  8. Tume ya taifa ya uchaguzi ipewe fedha kwa wakati ili iweze kutelekeza majukumu yake ipasavyo.
  9. Itungwe sheria kusimania shughuli za tume ya uchaguzi, pia iwepo sheria moja ya kusimamia chaguzi zote badaa ya uwepo wa sheria mbili kama sasa, maafisa wa uchaguzi watakao engua wagombea kushiriki uchaguzi bila kuzingatia sheria na weledi wawajibishwe kwa mujibu wa sheria.
  10. Matumizi ya tehama kwenye uchaguzi yaboreshwe na kuongezwa.
  11. Sharti ya uwepo wa sera ya jinsia liwepo kwenye kila chama cha siasa, na ujumuishi wa makundi maalumu, pia ushiriki wa jinsia moja kwenye vyombo vya maamuzi isipungue 40%. Pia, utaratibu wa uwakilishi wa viti maalumu kwa wanawake uendelee, isipokuwa sheria ziboreshwe kuweka ukomo wa miaka 10 pekee.
  12. Sheria zinazokwamisha ushiriki wa wa watu wenye ulemavu kwenye siasa ziangaliwe upya
  13. Juhudi za ushirikishwaji wa vijana kwenye siasa ziongezwe
  14. Serikali iongeze utoaji wa elimu ya uraia, pia ifundishwe kwenye ngazi zote za elimu, pia mtaala wa elimu uzingatoe elimu ya uraia.
  15. Swala la rushwa litamkwe katika katiba ya nchi ili wananchi watambue kuwa vitendo vya rushwa havitavumiliwa wala kuonewa muhali. Katiba ya Chama cha Siasa iwe na adhabu ya kumuondoa katika Mchakato wa Uchaguzi Mgombea aliyedhaminiwa na chama akithibitika kuhusika na vitendo vya rushwa
  16. Kuanzishwe utaratibu wa mijadaa kila mwaka itakayohusisha viongozi wakubwa wa kitaifa na kisiasa ili kudumisha mshikamano, mahakama iwe ni mamlaka ya mwisho ya kuamua pindi maridhiano yanapokwama
  17. Wanahabari waunde chombo cha kusimamia wanahabari na vyombo vyao, vyombo vya umma vitoe muda sawa wa kutangaza habari za wagombea wa vyama vyote kwa usawa, uwepo mchakato wa wazi wa kuwajibisha vyombo vya habari badala ya kufungiwa pekee na mkurugenzi wa habari na mawasiliano
  18. Mchakato wa katiba mpya uendelee, hata hivyo mjadala wa kitaifa kuhusu katiba mpya uanze kabla ya kuanza kwa mchakato wa kuandika katiba mpya ili kujadili maswala ya msingi kama muungano, mamkala ya Rais, madaraka ya serikali za mtaa, Rushwa, mfumo wa uchaguzi n.k. Pia, sheria ya mabadiliko ya katiba na sheria ya kura ya maoni zihuishwe pamoja na kuundwa kwa jopo la wataalamu ili kufanya mapitio ya katiba inayopendekezwa kwa kuzingatia hali ya sasa ya kiasiasa, kiuchumi na kijamii.
Maneno ya Rais Samia Suhuhu Hassan
Kazi hii imechukua miezi 10, haikuwa rahisi. Pengine ningewaacha ingechukua zaidi ya muda huu, lakini mimi pia navutwa shati.

Wananchi waelewe kuwa maoni ya kikosi kazi sio amri kwa Serikali. Tutaitana tena tuangalie na hali halisi ndani ya serikali na hali halisi ya sheria zetu pia ili tuweze kuyafanyia kazi vizuri

Tumepokea, na kama mlivyoona ripoti yenu ina mambo kadhaa, sisi kwenye serikali inabidi tujipange vikosi kadhaa, na wengine kati yenu tutawaomba mje kwenye vikosi kazi hivyo tujadili.

Siyo kwamba leo tumepewa ripoti ya kikosi kazi, kesho tutaanza kutekeleza hapana. Tumepokea, na wananchi wasikie tumepokea na tutafanyia kazi.

Na nyie watu wa siasa mjichambue, ni kazi ya jaji mtungi na watu wake. Nakubailiana na hoja ya 40% ya wanawake kwenye vyama vya siasa.

Tumepokea marekebisho ndani ya vyama vya siasa na wenyewe wasiwe mahodari wa kuirekebisha serikali lakini na wenyewe ndani tutizame je wanavyokwenda mambo ya usawa wa kijinsia yapo, mambo ya matumizi mazuri ya fedha yapo na mwengine akipata chama cha siasa anasema ni chake

Mgao wa ruzuku tutauangalia, hatuwezi kusema tutaongeza fedha zaidi sababu ni swala la kibajeti.

Matumizi ya teknolojia kwenye tume ya uchaguzi ni muhimu, ili teknolojia inayotumika iweze kutoa matarajio ambayo watu wanataka.

Tume ya uchaguzi tutalikalia kitako, ya serikali yatakwenda na ya ripoti nayo tutayaangalia.

Mijadala ya kisiasa kila mwaka iwepo, kaeni mjijadili, msijadili tu serikali, mjijadili na ninyi wenyewe. Mijadala heathy, hata serikali inaweza kuwezesha mijadala hii.

Wanawake mara nyingi nafasi muhimu wakigombea wanaambiwa kaa upande, au wanaambiwa njoo chukua hiyo gombea. Ukikuta wanawake kawekwa ni mwepesi mno, kapangwa kumsindikiza mtu. Kwa hili nakubaliana nao, ni pamoja na kuwasomesha wanawake, kuwatia moyo kwamba wanaweza.

Rushwa ni kidonda ndugu, hakuna hata chama kimoja kimenusurika hapa. Hakuna chama ambacho hakifanyi, nadhani ni tabia ambayo tunatakiwa kuibadilisha. Watu wajue, kuchaguliwa si mimi, ni chama. Hili la Rushwa, tujitazameni sote.

Maswala ya mikutano hakuna anayekataa, lakini lazima kuwe na jicho. Hatutaki kurudi tulikotoka, polisi wataanza tena kupiga watu. Tunaposema kwamba kanuni lazima tuzitazame siyo kwa nia mbaya, ni nia njema. Lazima tutazame kanuni na sheria ndipo turuhusu.


Tatizo la Rais wetu Hana kauli ya moja kwa moja. Anaongea kwa katikati Yani hatoi suluhisho.
 
Mara nyingi CHADEMA inakuwa kama iko juu kileleni na inataka kuangukia ama kwenye mwamba au kwenye ardhi ngumu. Maridhiano ni muhimu, lakini CHADEDMA inapata nini na inapoteza nini, ndiyo jambo la kujadili.
Hayana umuhimu wowote zaidi yanaisadia CCM kuendelea kujimilikisha nchi kama mali yao

Hujaone jinsi walivyopendekeza kuhusu msajili wa vyama na chaguzi za ndani ya vyama ?

Nilifikili nyundo waliokuwa wanapewa space walizifanyia kazi , kumbe na wao ni sawa tu na serikali na mambo yake
 
Dominated power ya tawala hata iundwe mahakama chini ya mwamba bado mgombea wa tawala atapita tu!

Kitu kimoja ninachojifunza, hasa nikiangalia haya yanayoendelea na akili za oppositions wetu, tawala wapo smart sana sana! Huku kwenye porojo tunawapopoa lakini ndani wamejipanga in a very complicated system.

Kama hujanielewa angalia game ya Al hilal vs Yanga! Yanga walitawala mchezo lakini hawakucheza kufuzu, Al Hilal hawakutawala lakini walicheza kufuzu! Ndicho wanachofanya tawala.

Sometimes wanaacha mpige kelele hadi mhisi mnabeba nchi saa mbili asubuhi lakini wanajua mwisho wa utawala wenu ni kwenye kelele huku wao wanashinda na kuwaacha muendelee kupiga kelele! Mnapewa viti vya uwakilishi huko dom kuwapoza, viongozi wa upinzani na wawakilishi wa dom wanapewa vi safari na viposho posho wana enjoy life huku wakiunda vikundi vya kupiga kelele mitandaoni kulinda nafasi zao!

Mfumo wa sihasa uko very corrupted! Tunadanganyana majukwaani tu!


Ndio maana CHADEMA wanalilia Katiba Mpya ili kuondoa hicho unachokisema.
 
Back
Top Bottom