Rais Samia anavyowaandaa wanawake wamchague mwanamke 2025, vyama pinzani navyo viruhusiwe kufanya siasa kupambana na huyo Mwanamke

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2019
Posts
762
Reaction score
6,984
Rais ametangaza rasmi kwamba wanawake watakuwa na kazi yakumpata Rais mwanamke 2025 means kwa kauli hii amewaambia chama chake kwamba mgombe atakuwa mwanamke aidha yeye au mwanamke mwingine. Hii inatoa tafsiri ya wazi kwamba wanaume kwa upande wake awataruhusiwa kupambana na mwanamke atakayepitishwa hivyo kwa kukuwa yeye ni Mwenyekiti wa chama mapinduzi, wanaume wote waliotamani kugombea nafasi ya Urais 2025 kupitia chama hicho waanze kutafuta kazi nyingine yakufanya vinginevyo Mwenyenzi Mungu afanye miujiza.

Kwa upande wa pili, kauli hii haiwezi kuwa na nguvu upande wa upinzani kwa sababu wao bado wanao mfumo wao wakupata wagombea Urais. Mfumo huo haufungwi na kauli za Rqis, lakini pia kwakuwa ametangaza adharani na kwa nafasi yake maana yake kampeni za uchaguzi 2025 zimeanza rasmi leo.

Nasema zimeanza rasmi leo kwa sababu muda si mrefu kila atakayekuwa anasimama jukwaani atakuwa anampigia chapuo mwanamke wa 2025, hii kauli ni maelekezo kwa Mawaziri ,wabunge wa CCM na wengine wote ambao wanaishi kwa kasababuu ya uteuzi qa Rais na serikali iliyopo. Kampeni hizi naamini na natabiri zitamabtana na nyimbo, zitaambatana na matangazo kwenye vyombo vya habari na zitaambatana pia wale wanaopinga agizo hili au wanaoonekana kutaka kuwa na nguvu zaidi ya mwanamke kuwajibishwa.

Ni muda Sasa vyama vya upinzani navyo kuanza KUJIANDAA kuanzia ngazi ya mtaa kuwashawoshi wapiga kura ambao kwao wao hawachagui jinsia Bali wanachagua kiongozi. Kwamba tuchague jinsia hii haitaweza kuwa agenda kwa wananchi 2025 Bali agenda itakuwa maji, elimu, demokrasia, katiba, afya na mapambano ya tozo zinazouma.

Kuendelea na kauli mbiu ya kuacha siasa tufanye maendeleo wakati upande mmoja unafanya siasa na kuandaa wagombea pamoja na kuwanadi nikuendeleza ukandamizaji ambao haitakuwa na tija kwa Taifa Bali utakuwa na tija kwa huyo Mwanamke anayeamini kupata urais bila democracy.
 
Huyo Rais Mwanamke atakuwa mwengine ama yeye ndio anataka aendelee? Kama anataka aendelee ndio tuseme kwa hii miezi 6 tu kesha ona ameiweza hii kazi na changamoto zake na kaingiwa na matamanio ya kuendelea. JK Nyerere alisema mkiona mtu anaukimbilia Urais huyo ni wakuogopwa kama..... Kwa nyakati hizi tungesema corona.
 
Uwe unajibu posts wanazoandika watu kwenye thread zako
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Wanaume tujiangale eti tusifanye masihara tukawa legelege
Wanauliza - watatuwezaaaaa
Wanaitika - hawatuweziiiiii

*Kweli sisi wanaume hatuwawezi wanawake?
*Wanasema sisi ni majirani KWELIII!

Adam alikabidhiwa dunia na Mungu atawale kilakitu kisha akafanyiwa msaidizi wake!! Leo msaidizi anatuita sisi wenyedunia MAJIRANI?

Wanaume tujipige vibao tumebaguliwa sana Leo

Kwa niaba ya wanaume tunaojitambua ninakemea vikali kitendo cha wanawake kushindana nasisi,nakemea pia kutuita sisi majirani sisi ni wenyenyumba majirani ni kenya,Uganda nk. Tabia hiyo ikome kabla sijakasirika ala!!! Hatuwezi kuwa na nchi ya kusutana. Tunakwama wapi? Leteni katiba mpya chapu tunapokwenda sio
 
Wamuache Mama mjukuu wa Machalila alitutesa sana ila kinachonishangaza Kina Humphrey na John walidhan watamyumbisha wakapanga mpaka mengine ya kumhujumu wakakuta kuna fence huku Mabeyo huku Jakaya alafu kati kati SIRRO 😂 naendelea KUSISITIZA LILE DOKEZO

mimi Furaha yangu ni kuona Magufuli hayupo Ikulu wala Bashiru sasa Furaha haja zaidi CCM ikitoweka kabisa
 
Sio kwamba viruhusiwe wana haki kwa kuwa yeye mwenyewe ametangaza atagombea urais hivyo ametangaza rasmi vita ya kisiasa kwa hiyo awe tayari kwa mashambulishi ya 'character assassination' na aitumie madaraka yake vibaya kuwanyanyasa wengine.
 
Mama kakosa content, hakupanga kusema hayo kama angejua madhara. Swali hilo aliulizwa na BBC akalikwepa leo kalivaa mazima
 
Kama ni sahihi ninafikiri basi katika ngazi zote hizo za uongozi watu waanze kufunguka! Ni muda muafaka akina Mwigulu, Polepole, Lusinde, Musukuma, na wapenda madaraka wengine kujitangaza kuwa watagombea mwaka 2025. Au ninakosea waungwana?

"Mie ni MCCM lakini nina uhakika Mbowe sio Gaidi!"
 
Naona anafuata style ya Ruto huko Kenya, manake alitangaza kugombea mara baada tu ya a uchaguzi uliopita wa 2017! Haya bana, mtifuano ngoja uanze baada ya kipyenga hiki kulia,na kwa hilo si ajabu kama maendeleo yenye tija na ya maana kwa wananchi yataweza fikiwa....sie watazamaji.
 
Back
Top Bottom