Suala wasizuie mikutano ya kisiasa kwa vyama vyote hata kama kuna tishio la UVIKO-19 haijarishi mbona wao wanakusanyana mpaka wanapakazana majasho?

Huyo mama ameanzisha vita ambayo ndio itakayo mfanya aone jua linatokea magharibi kuelekea mashariki
 
... kwa Rais anayeendelea huwa inachapishwa fomu moja tu! Ndio uataratibu wa chama.
 
Mama amepandisha mabega, anaamini ameshalidhibiti Sukuma Gang na kwa msaada wa Msoga Gang anaweza kufanya lolote sasa.
 
Kutafuta uhalali wa kisiasa kwa kutumia kabila lako ni Ubaguzi, kutafuta uhalali wa kisiasa kwa kutumia dini yako ni ubaguzi. Kutafuta uhalali wa kisiasa kwa kutumia maumbile yako ni ubaguzi. Na dhambi ya ubaguzi dawa yake ni kukemewa kwa nguvu na kulaaniwa.
 
Msiba wa nani tena?Mbona Nyerere tulishamaliza msiba!
Bob hivi mumeo akifa hata mwaka haujaisha unaweza tangaza kufunga ndoa hata miezi minane haijatimia??? Hivi unadhani watoto wa marehemu mumeo hawatafikiri ulimuua baba yao ili uolewe????
 
Kuna wakati katika moja ya hotuba zake, aliwaasa wanaCCM waache kuwaza 2025 na badala yake wachape kazi kipindi hicho kikifika basi mambo yatajijibu yenyewe.

Lakini sasa, ameamua kupakimbilia mwenyewe huku alishawakataza wenzie.

Ni uhuni.
 
Hili li mtu lishajisahau
Hivi madaraka yana nini?? Mbona kama huwachanganya watu wakaacha kufikiri..
Huyu anajuaje atakuwepo 2025!!
 
Si vizuri kwa vyama vya siasa kufanya mikutano wakati huu ambao nchi inakabiliwa na ugaidi.
 
Bob hivi mumeo akifa hata mwaka haujaisha unaweza tangaza kufunga ndoa hata miezi minane haijatimia??? Hivi unadhani watoto wa marehemu mumeo hawatafikiri ulimuua baba yao ili uolewe????
Mimi ndiyo baba nimekufa.
 
Kipenga ndio kimeshapulizwa hivyo ..haijatokea kwa bahati mbaya iyo... Hata February kurudishwa kundini ni kwa ajili ya kumpunguza nguvu na hatimaye kumdhibiti madelu
February na bimkubwa mentor wao ni mmoja...!
 
Hawapendani ... Na hao ndio hao watakaomnyima kura kwa wingi
 
Nimemsikia mama akisema 2025 atagombea urais na mwaka huo ndiyo wanawake wanaenda kumchagua Rais mwanamke.

Mimi sina matatizo na msimamo wake huo, matatizo yanakuja wakati yeye kama mkuu wa nchi anapotumia platform ya kitaifa kujipigia upatu ilihali wapinzani wake wakiwa wamezibwa midomo na kufungwa mikono.

Rais alitangaza mikutano ya kisiasa hairuhusiwi na wasubiri uchumi uimarike. Hakuna taifa lililosubiri uchumi ukaimarika ndipo likaanza kutenda haki, halipo na huenda halitakuja kuwepo. Kiongozi mkuu wa nchi anapokoswa uwezo wa kupambanua mambo ni hasara kwa taifa.

Kama Rais Samia ataendelea na tabia ya kuwanyanyasa wapinzani wake kisiasa atakiona cha mtema kuni. Mungu wetu yu hai na ataendelea kutupigania.

Mithali 19:1 Afadhali maskini aendaye katika unyofu wake, kuliko mpotofu wa midomo aliye mpumbavu.
 
Ila CCM wahuni sana. Wamemfunga Mbowe, si kwa sababu ya madai ya katiba mpya au ugaidi. Wamemfunga kwa sababu kwa jinsi CCM walivyogawanyika, CHADEMA walikuwa wanaenda kuzoa wafuasi wengi sana.

Samia hana base yoyote ya kisiasa. Anategemea calculations za Kikwete aweze kuendesha nchi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…