Rais Samia: Hatukutoa fursa ya Mikutano ya hadhara watu wakavunje sheria, wasimame kutukana, kukashifu na kuchambua dini za wengine

Rais Samia: Hatukutoa fursa ya Mikutano ya hadhara watu wakavunje sheria, wasimame kutukana, kukashifu na kuchambua dini za wengine

Wakiambiwa ukweli wanajificha kwenye kichaka cha udini kuwa wanakashifu dini za watu na wanatukana matusi,kashifa na matusi hawayasemi ni yapi yaliyotukanwa,sheria wanazodai zimevunjwa ni zile za kubumbwabumbwa ambazo wakipeleka mahakamani wanaishia kushindwa.
 
Kama anaamini katika demokrasia lazima aonyeshe kwa vitendo, aache ukandamizaji wa upinzani, kama alivyoapa kulinda katiba atimize wajibu wake, kamata kamata isiyo na msingi iachwe, na sasa umefika wakati wa kukubali kukoselewa, kama anavyokosolewa kuchemka kwake kwenye suala la Dipiwedi, Kukubali udhaifu sio dhambi, mabadiliko ya katiba ni ya wananchi sio CCM,CCM waache kuhodhi katiba. lakini lazima tuwe na mahakama ya Katiba katika mapendekezo ya katiba mpya.
"Lingine, hakuna aliye juu ya sheria. Kila anayefanya makosa sheria itamshika. Kama umekiuka sheria, sheria itakushika. Ajenda yetu kubwa kama watanzania ni kudumisha amani, umoja na mshikamano wa kitaifa."
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akishiriki Mkutano Maalum wa Baraza la Vyama va Siasa na Wadau wa Demokrasia katika ukumbi wa JNICC leo tarehe 11 Septemba, 2023 katika viwanja vya Ikulu, jijini Dares Salaam.


Kituo cha TCD kinafanya kazi vizuri tangu Rais Samia aingie madarakani, na ndie amekipa uhai. TCD ilifanya mkutano na wadau kujadili hali ya demokrasia kuelekea chaguzi za 2024 na 2025, baada ya kujadili kuna mambo tulifanyia maazimio na tutayaleta hapa.

Kuhusu Katiba, mchakato wa kupata katiba mpya uweze kuendelea, lakini kwa muda uliopo huenda tunaweza tusipate Katiba Mpya. Lakini mabadiliko ya katiba yanaweza kufanyika ikiwemo kufanya mabadiliko kifungu cha 74 cha Katiba ili tume huru iweze kusimamia uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025.

Pawepo mgombea binafsi, kufanyia marekebisho kifungu cha 39 (2) cha katiba ya sasa kuhusu Rais na kifungu cha 67(1) kuhusu wagombea ubunge. Kuwa Rais atangazwe akishinda kwa zaidi ya 50% ya kura kwa hiyo kurekebisha kifungu cha 41 (6) na uchaguzi wa Rais uweze kuhojiwa mahakamani hivyo kubadilisha kifungu cha 41 (7).

JENISTA MHAGAMA, WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE NA URATIBU)
Amemshukuru Rais Samia kwa kukubali kuwa mgeni rasmi kwenye mkutano huu.

Kwenye siku tatu za Mkutano huu, wajumbe watashiriki kujadiliana ni namna gani taifa letu litaimarisha na kuboresha demokrasia hapa nchini.

Pia, tathimini ya maoendekezo ya kikosi kazi yatajadiliwa kwenye mkutano huu.

Rais Samia amedhihirisha kuwa ni kiongozi anayezingatia utawala bora na kutenda haki kwa watanzania wote.

SAMIA SULUHU HASSAN, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Leo tunapokutana na kuzungumza mapendekezo ya kikosi kazi ni mapendekezo ambayo wote wadau wa siasa nchini wameyaleta kwa pamoja.

Tutapishana tu kwa jinsi ya kusukuma utekelezaji, huyu anataka kalileta leo lifanywe kesho, mwingine ana subira kidogo, lakini wote maono yetu ni kama yanaenda pamoja.

Tayari Serikali imeanza kuchukua hatua ya baadhi ya mapendekezo ya kikosi kazi na mnayajua, kwa mfano kuruhusu Mikutano ya hadhara, tayari imeruhusiwa watu wanakwenda na tunawasikia yanayosemwa huko.

Lakini pia tulishauriwa kuunda kanuni za kuendesha hiyo mikutano ya hadhara, zimeundwa na zinatekelezwa, hilo limeshafanyika.

Lakini pia kuna jambo mahsusi ambalo ndio kila mtu analisubiri la katiba, marekebisho ya katiba yetu ambalo nalenyewe limeanza kufanyiwa kazi na pengine mkutano huu ni kuelekea huko pia.

La mikutano ya hadhara, tumeruhusu tukiwa na nia ya vyama vya siasa vizungumze wananchi wasikie sera zao, mada zao, mipango yao ili vyama vikue na virudishe watu wale walio wapoteza, vyama visimame, viwe madhubuti, tukienda kwenye uchaguzi kila chama kimejijenga vya kutosha na ndio maana ya kutoa fursa hii ya mikutano ya hadhara.

Hatukutoa fursa ile watu wakavunje sheria, watu wakasimame kutukana, watu wakasimame kukashfu, watu wakasimame kuchambua dini za watu. Lakini sishangai kwanini haya yanatokea, kwa sababu ya kuzungumzwa hakuna.

Tulianza na katiba, tukaenda ikakatika katikati, bandari imeenda sasa katiba tena. Tumieni hiyo fursa kajijengeni kwa wananchi, elezeni sera zenu, mtafanya nini, ili wananchi warudi wawaunge mkono ili tukienda kwenye uchaguzi vyama vyote vimejijenga vizuri.

Uendeshaji wa Tanzania unahitaji fikra za kila mtu, hakuna mtu mwenye hati ya kuimiliki, hata kitoto kilichozaliwa yeye kina haki, ili tuendeshe vizuri kila kundi litoe mawazo tuendeshe nchi yetu.

Niseme tena, fursa hii iliyotoka isiende kuharibu neema na baraka aliyotupa Mungu. Isiende kuharibu misingi ya uendeshaji nchi hii wazee wetu waliyotuachia.

Lingine, hakuna aliye juu ya sheria. Kila anayefanya makosa sheria itamshika. Kama umekiuka sheria, sheria itakushika. Ajenda yetu kubwa kama watanzania ni kudumisha amani, umoja na mshikamano wa kitaifa.

Tulitoa uhuru wa maoni, maoni mengi sana yanatoka kwa watanzania, tunayaona, mazuri tunayachukua na mengine unayapima maoni yao. Nina kikundi maalumu kinachoangalia maoni yote maoni na kuchukua yale mazuri na kuyaweka kwenye mipango yetu kuyafanyia kazi.

Kuna uhuru wa maoni lakini huu uhuru wa maoni una mipaka yake, sio tu kisheria, hata kibinadamu.

Yaani ukimsikiliza SAMIA unaona kabisa kwamba haelewi anacho ongea na haelewi anachowasilisha,KAZI ya wanawake waachiwe kupika na kazi ya uongozi waachiwe wanaume,Rais hana jipya zaidi ya mipasho tu ambayo ndio KAZI ya akina mama walio wengi,lkn utakuwa wajinga wanasifu.Amesema hakuna mtu mwenye hati miliki na nchi hii,ni vzr ametambua maana amechelewa sana kuelewa hilo yy alidhan ana hati miliki ya nchi hii na ameingia mikataba ya kipumbavu kana kwamba hii nchi ni yake.mama hajielewi na hawezi kuzungumza na akajua anaongea na akina nani yaani ni sifuri kabisa.
 
mikutano ya siasa , huwa ni huruma ya Rais au ipo ki katiba ? ila sawa... Rais yupo juu ya katiba na kila kitu kwa Tanzania
 
Huyu mama nchi imemshinda hii!

Upo huru na maoni yako, kwa lipi zaidi?

Wengine tunaona kazi zake adhimu na adimu ni njema sana.

"Wengi wape lakini wengine wasikilize" - mama Samia.

Tunakusikiliza.
 
Ya kuzungumza hakuna !
Anataka kutuambia Kila kitu kipo mwake!
 
Kama anaamini katika demokrasia lazima aonyeshe kwa vitendo, aache ukandamizaji wa upinzani, kama alivyoapa kulinda katiba atimize wajibu wake, kamata kamata isiyo na msingi iachwe, na sasa umefika wakati wa kukubali kukoselewa, kama anavyokosolewa kuchemka kwake kwenye suala la Dipiwedi, Kukubali udhaifu sio dhambi, mabadiliko ya katiba ni ya wananchi sio CCM,CCM waache kuhodhi katiba. lakini lazima tuwe na mahakama ya Katiba katika mapendekezo ya katiba mpya.
Walikomaa na maridhiano uchwara ,kiko wapi sasa
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akishiriki Mkutano Maalum wa Baraza la Vyama va Siasa na Wadau wa Demokrasia katika ukumbi wa JNICC leo tarehe 11 Septemba, 2023 katika viwanja vya Ikulu, jijini Dares Salaam.


Kituo cha TCD kinafanya kazi vizuri tangu Rais Samia aingie madarakani, na ndie amekipa uhai. TCD ilifanya mkutano na wadau kujadili hali ya demokrasia kuelekea chaguzi za 2024 na 2025, baada ya kujadili kuna mambo tulifanyia maazimio na tutayaleta hapa.

Kuhusu Katiba, mchakato wa kupata katiba mpya uweze kuendelea, lakini kwa muda uliopo huenda tunaweza tusipate Katiba Mpya. Lakini mabadiliko ya katiba yanaweza kufanyika ikiwemo kufanya mabadiliko kifungu cha 74 cha Katiba ili tume huru iweze kusimamia uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025.

Pawepo mgombea binafsi, kufanyia marekebisho kifungu cha 39 (2) cha katiba ya sasa kuhusu Rais na kifungu cha 67(1) kuhusu wagombea ubunge. Kuwa Rais atangazwe akishinda kwa zaidi ya 50% ya kura kwa hiyo kurekebisha kifungu cha 41 (6) na uchaguzi wa Rais uweze kuhojiwa mahakamani hivyo kubadilisha kifungu cha 41 (7).

JENISTA MHAGAMA, WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE NA URATIBU)
Amemshukuru Rais Samia kwa kukubali kuwa mgeni rasmi kwenye mkutano huu.

Kwenye siku tatu za Mkutano huu, wajumbe watashiriki kujadiliana ni namna gani taifa letu litaimarisha na kuboresha demokrasia hapa nchini.

Pia, tathimini ya maoendekezo ya kikosi kazi yatajadiliwa kwenye mkutano huu.

Rais Samia amedhihirisha kuwa ni kiongozi anayezingatia utawala bora na kutenda haki kwa watanzania wote.

SAMIA SULUHU HASSAN, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Leo tunapokutana na kuzungumza mapendekezo ya kikosi kazi ni mapendekezo ambayo wote wadau wa siasa nchini wameyaleta kwa pamoja.

Tutapishana tu kwa jinsi ya kusukuma utekelezaji, huyu anataka kalileta leo lifanywe kesho, mwingine ana subira kidogo, lakini wote maono yetu ni kama yanaenda pamoja.

Tayari Serikali imeanza kuchukua hatua ya baadhi ya mapendekezo ya kikosi kazi na mnayajua, kwa mfano kuruhusu Mikutano ya hadhara, tayari imeruhusiwa watu wanakwenda na tunawasikia yanayosemwa huko.

Lakini pia tulishauriwa kuunda kanuni za kuendesha hiyo mikutano ya hadhara, zimeundwa na zinatekelezwa, hilo limeshafanyika.

Lakini pia kuna jambo mahsusi ambalo ndio kila mtu analisubiri la katiba, marekebisho ya katiba yetu ambalo nalenyewe limeanza kufanyiwa kazi na pengine mkutano huu ni kuelekea huko pia.

La mikutano ya hadhara, tumeruhusu tukiwa na nia ya vyama vya siasa vizungumze wananchi wasikie sera zao, mada zao, mipango yao ili vyama vikue na virudishe watu wale walio wapoteza, vyama visimame, viwe madhubuti, tukienda kwenye uchaguzi kila chama kimejijenga vya kutosha na ndio maana ya kutoa fursa hii ya mikutano ya hadhara.

Hatukutoa fursa ile watu wakavunje sheria, watu wakasimame kutukana, watu wakasimame kukashfu, watu wakasimame kuchambua dini za watu. Lakini sishangai kwanini haya yanatokea, kwa sababu ya kuzungumzwa hakuna.

Tulianza na katiba, tukaenda ikakatika katikati, bandari imeenda sasa katiba tena. Tumieni hiyo fursa kajijengeni kwa wananchi, elezeni sera zenu, mtafanya nini, ili wananchi warudi wawaunge mkono ili tukienda kwenye uchaguzi vyama vyote vimejijenga vizuri.

Uendeshaji wa Tanzania unahitaji fikra za kila mtu, hakuna mtu mwenye hati ya kuimiliki, hata kitoto kilichozaliwa yeye kina haki, ili tuendeshe vizuri kila kundi litoe mawazo tuendeshe nchi yetu.

Niseme tena, fursa hii iliyotoka isiende kuharibu neema na baraka aliyotupa Mungu. Isiende kuharibu misingi ya uendeshaji nchi hii wazee wetu waliyotuachia.

Lingine, hakuna aliye juu ya sheria. Kila anayefanya makosa sheria itamshika. Kama umekiuka sheria, sheria itakushika. Ajenda yetu kubwa kama watanzania ni kudumisha amani, umoja na mshikamano wa kitaifa.

Tulitoa uhuru wa maoni, maoni mengi sana yanatoka kwa watanzania, tunayaona, mazuri tunayachukua na mengine unayapima maoni yao. Nina kikundi maalumu kinachoangalia maoni yote maoni na kuchukua yale mazuri na kuyaweka kwenye mipango yetu kuyafanyia kazi.

Kuna uhuru wa maoni lakini huu uhuru wa maoni una mipaka yake, sio tu kisheria, hata kibinadamu.

CCM Walishafeli siasa za majukwaani miaka mingi toka Nyerere atutoke. Juzi juzi wamekimbizana kuwatetea DPW ila wakagundua hakuna mwananchi anawaelewa. Wamerudi kwenye kichaka chao kinachoitwa polisi.
 
Back
Top Bottom