Rais Samia: Kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake, lakini mbona mnakula sana mnavimbiwa? Jipimieni!

Rais Samia: Kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake, lakini mbona mnakula sana mnavimbiwa? Jipimieni!

Tuhamasishe wananchi wawakatae hata kabla ya uchaguzi?

Tuandamane?

Tugome na kufanya migomo ya nguvu?

" kila waziri anatakiwa ale kulingana na urefu wa kamba yake" Anonymous.
Kuandamana?Makamanda wenyewe wameacha hayo mambo ya maandamano wewe utaweza?
 
Akafumuliwa kuwa kuwa kama alipata division 1 form 4 kwa point 4 ni kwa nini hakwenda form 5, akawa hana jibu

Division 1 Form 4 kwa point 4 !!! Wanalikuwa wanahesabu masomo mangapi walipo gawa haya madaraja? Cambridge form four school certificate walikuwa wanahesabu masomo 6 walipokuwa wanatoa divisions!
 
Kama Kiguu analitambua hilo. Then what ? She think this is the Solution ? Serikali yakipigaji hiii , kama mpaka masterroom ya Inch inalitambua hili na hamna hatua
Nchi za watu kunusa public fund adhabu yake ni risasi Sisi bado tuna madubwasha Yana encourage watu kuiba. Kinachonifurahisha hata kama wasomi wetu ni ma traitors wa pesa tulizowasomesha reaction za watu zinanipa Moyo kwamba kuna kizazi hakidaki huu uhuni .serikali ya kihuni kabisa .#@£&££#@@
 
Kama Wanajulikana Si Watolewe Kwenye Mfumo. Haya Mambo Yanahitaji Vitendo Na Uchukuaji Hatua Seriously La Sivyo Ni Business As Usual Maana Wathu Hawatakuwa Na Hofu Wakijua Hamna Watakalofanywa.
 
Nimepitia uzi huu mda huu (Rais Samia: Kila mbuzi hula urefu wa kamba yake, lakini mbona mnakula sana, mnavimbiwa? Si kweli kama hampati kwenye maeneo yenu. Jipimieni...) wa usiku nimejikuta nawza tu na kucheka, sasa na mimi nauliza je yule mwenye kamba ambayo ina urefu wa kula kwa mwezake hapo vipi, lakini pia kwa sababu ni kula majani kwa urefu wa kamba yake.. kwa wale ambao ni majani walifikiri wanamwagiliziwa ili nao wanawili sasa wajiandae kuliwa kwa kasi sana na baada ya hapo watolewe kama pupu, chooni na umaliziwe na funza kabisa.

Nimefurahi kwa sababu mama ameonesha na amekweka wazi kuwa analitambua hilo lakini lifanyike kwa tahadhari bila kuathiri miradi kuwa chini ya kiwango. lakini zaidi mama hataki watu kusema kwake. maana mtot anayependa kshtaki sana huyo huwa ni mnoge na hajui kujitetea.

Sasa jiulize wewe ni majani unaoliwa au wewe ni mlaji wa majani, kama ni mlaji basi hakikisha hauvibewi na usiwe na tamaa ya 2025
 
Kwani we ukisikia neno mafisadi unaelewa nini, ama unajifanya punguani na wewe au sio.!
Kama unajua kuwa huna kitu kichwani chaguo sahihi ni kukaa kimya ili kuficha ujinga.

Ufisadi ni neno linalojumuisha matumizi yote yasiyo sahihi ya fedha za uma kama vile kutumia fedha za uma nje ya budget,kutumia fedha za uma kutoa zawadi nje ya sheria,kutumia fedha za uma kutoa misaada nchi nyingine nje ya sheria na budget,wizi wa fedha za uma,rushwa,kutumia fedha za uma kununua wapinzani,kufanya matumizi zaidi ya budget,kulipa miradi hewa,kutoa tenda nje ya utaratibu,kutakatisha fedha chafu na kadhalika.

Ni neno pana sana.Wizi ni sehemu ndogo sana ya maana ya neno ufisadi.Siku nyingine jifunze kukaa kimya ili kuokoa server za JF zisijae ujinga na ili ujiokoe wewe pia kuonyesha ujinga wako.
 
Division 1 Form 4 kwa point 4! Wanalikuwa wanahesabu masomo mangapi walipo gawa haya madaraja? Cambridge form four school certificate walikuwa wanahesabu masomo 6 walipokuwa wanatoa divisions!
Samahani, nadhani nimekosea hiyo namba kwani siikumbuki tena; point 4 zilikuwa ya form 6 nadhani. Hicho cheti cha form 4 kilikuwa na A tano, C moja (ya Kiswahili) na B mbili za Siasa na Kiingereza; sikumbuki kwa jumla hizo zilikuwa point ngapi wakati huo. Lakini walimkamata kuwa kwa pass hizo asingeishia form four tu.
 
Samahani, nadhani nimekosea hiyo namba kwani siikumbuki tena; point 4 zilikuwa ya form 6 nadhani. Hicho cheti cha form 4 kilikuwa na A tano, C moja (ya kiswahili) na B mbili za Siasa na Kiingereza; sikumbuki kwa jumla hizo zilikuwa point ngapi wakati huo. Lakini walimkamata kuwa kwa pass hizo asingeishia form four tu.

Thanks for your clarification!!
 
Hii kauli ina maana zaidi ya moja. Haikupaswa kutoka hadharani.
Naam,lugha huzingatia utamaduni na mapokeo ya jamii...Kila mbuzi anakula kwa urefu was kamba yake ,hata kama Ina maana nzuri,lakini nanna linavyitumika ...no kuhslalisha wizi na ufisadadi!
 
Fisadi namba moja ni Rais ambae anahamasisha ufisadi kupitia TV ya Taifa🤡🤡🤡
 
Jipimieni!🤡🤡🤡
 
Mleta uzi huwa nakuonea huruma sana.Hivi unaelewa kuwa Tanzania haina Bunge?

Unaelewa kuwa hawa wabunge waliopo walipewa ubunge na serikali?Wabunge waliopewa ubunge na serikali watatoa wapi uwezo/nguvu ya kuiondoa serikali hiyo madarakani?

Yaani unamuondoa vipi madarakani mtu aliekupa zawadi ya ubunge?Unamuondoa vipi madarakani mtu ambae amekupa tonge bure?Mleta uzi utaanza kuwa serious lini?
 
Kama unajua kuwa huna kitu kichwani chaguo sahihi ni kukaa kimya ili kuficha ujinga.

Ufisadi ni neno linalojumuisha matumizi yote yasiyo sahihi ya fedha za uma kama vile kutumia fedha za uma nje ya budget,kutumia fedha za uma kutoa zawadi nje ya sheria...

"Unaelewa maana ya ufisadi?Nani kakwambia kuwa ufisadi ni kuiba?"

Unaniuliza nani alie niambia kwamba ufisadi ni kuiba alafu tena unajijibu mwenyewe kwamba,

"Wizi ni sehemu ya ufisadi"

Basi uko sawa, umekata gogo!!, alafu umezoa mwenyewe.
 
Back
Top Bottom