Rais Samia: TAKUKURU wamefuta kesi za kubambikizia 147, Polisi na nyie jitazameni
Well said Mama President!! Nakupa 👍👌

Ila tunaomba uangazie vyombo vingine vya kutoa haki sio Jeshi la Polisi na Mahakama tuu!!!

Kuna chombo kama TUME YA UTUMISHI WA UMMA. Hii taasisi imekuwa ni kero sana kwa watumishi wa Umma ambao wanakata rufaa au wanapeleka malalamiko yao.

Kama unavyoona Mahakama au Jeshi la Polisi zinavyopora haki za watu vivyo hivyo hii inatokea kwa TUME YA UTUMISHI WA UMMA.

Tume ya Utumishi wa Umma wamekuwa ni wababaishaji sana katika kushughulikia matatizo au kero zinazopelekwa na watumishi wa umma kwa njia ya rufaa au malalamiko dhidi ya waajiri wao.

Tume ya Utumishi wa Umma imekuwa; haifanyi critical review ya malalamiko na rufaa za watumishi na mara nyingi hulalia upande wa mwajiri

Tume ya Utumishi wa Umma imekuwa na tabia ya ucheleweshaji wa rufaa na malalamiko yanayopelekwa na watumishi wa umma, na mara nyingi wamekuwa too defensive!!

Ukienda kuulizia hatma ya jambo lako wanakuwa wakali na hawawi cooperative at all, customer care ni zeero kabisa ktk hii ofisi.

Nafikili hata technical know how jinsi ya kufanya kazi ni tatizo, inaonekana hata ujuzi waliokuwa nao wafanyakazi wa hii Tume ya Utumishi wa Umma ni questionable na ndio maana wanaishia kuvurunda case za watu huku zikiwa zimekaa muda mrefu.

Mama President, hii ofisi ya TUME YA UTUMISHI WA UMMA ni mojawapo ya taasisi inayoharibu na kuwanyima haki watumishi wa umma, imekuwa ni mojawapo ya vichochoro vinavyotumiwa na waajiri waliokosa maadili na kuwaharibia utumishi watumishi wa umma.

Inaonekana hii tume inatumika na waajiri kuwakandamiza watumishi wa umma. How comes, rufaa au malalamiko ya mtumishi yanakaa mwaka au hata zaidi ya mwaka bila kupata muafaka au kulikamilisha. Tume ya Utumishi wa Umma imekuwa ni mojawapo ya taasisi zinazokiuka sheria badala ya kuzisimamia na kuzifuata ipasavyo.

Tunaomba mamlaka husika ziingalie hii ofisi ya TUME YA UTUMISHI WA UMMA jinsi inavyofanya kazi ili kudhibiti upotevu wa haki za watumishi wa umma.

Asante!
Haiwezekani kati ya rufaa 178 zilizopelekwa zilizoamuliwa na ofisi ya TUME YA UTUMISHI WA UMMA tena kwa kuchelewa, ni rufaa 5 tu ndizo zilizoshinda!!!

Tume ya Utumishi wa Umma inashirikiana na waajiri wasio na maadili kuwakandamiza na kuwanyima haki watumishi wa umma.

Mama President, kindly take up this matter seriously!!

Asante sana.
 
Hii ni baada ya kutakiwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kuondoa kesi za kubambika.

====




Rais Samia Suluhu: Kwenye suala la wingi wa mahabusu, labda niseme kwamba jana nikiapisha majaji nililigusia hili, uharakishwaji wa kesi na nimezitaka taasisi zote ikiwemo jeshi la polisi ambalo uchunguzi unaanza kwenu kuharakisha chunguzi za kesi mbalimbali zilizopo ili kuharakisha kesi kusikilizwa na iadha kufutwa au mtu kuhukumiwa ipasavyo lakini pia niongee na jeshi la Polisi kupunguza kesi za kubambikiza.

Kuna mlolongo mkubwa wa makesi ya kubambikiza, huu ukipungua na mahabusu watapungua, kwasababu wengi wapo wanasubiri kuhukumiwa, kesi haiendi, ushahidi hakuna, mpelelezi anashindwa kupeleka kesi kwasababu hakuna ushahidi.

Niombe sana, nilizungumza hili na TAKUKURU, wameweza kufuta kesi 147 ambazo waliwabambikizia watu, kwahiyo nanyi Jeshi la polisi jikagueni kama kuna za aina hiyo nazo zifutwe ili tupunguze wingi wa mahabusu kwenye majela yetu.

Lazima tuwe na sheria ya watu wanambambikia watu makosa,hivihivi yatajirudia..Bunge limelala,tungeni sheria,ili suala hamlioni???
 
Waizi watarudi mitaani Tu enzi zake zimefika
Chuki zaidi ya uhalisia. Ungekuwa na ndugu anayesota mahabusu kwa kesi isiyo na kichwa wala miguu usingesema haya. Ungekuwa na ndugu ambaye kosa lake ni kupiga kampeni tu na kisha kuwekwa mahabusu KWA kesi ya uhujumu uchumi usingesema haya.
 
... kumbe hii issue ya kubambika kesi nikajua ni polisi kumbe hadi TAKUKURU ipo? Dah; kwanini hao waliofungua hayo mafaili ya kubambika raia wema kesi wasitimuliwe na kushitakiwa? Huu ujinga utaendelea kutamalaki hadi lini!
Sio kama wanabambikiwa bali ushahidi ulipo ni hafifu kuwatia hatiani.
 
Haiwezekani kati ya rufaa 178 zilizopelekwa zilizoamuliwa na ofisi ya TUME YA UTUMISHI WA UMMA tena kwa kuchelewa, ni rufaa 5 tu ndizo zilizoshinda!!!

Tume ya Utumishi wa Umma inashirikiana na waajiri wasio na maadili kuwakandamiza na kuwanyima haki watumishi wa umma.

Mama President, kindly take up this matter seriously!!

Asante sana.
Kama jinsi Jeshi la Polisi linavyowabambika kesi raia basi ni hivyohivyo jinsi Waajiri waliokosa maadili wanavyowabambika kesi watumishi wao.

Na bada ta watumishi hao kupeleka malalamiko au kukata rufaa TUME YA UTUMISHI WA UMMA, Tume ya Utumishi wa Umma wa umma wanashindwa kufanya critical review ili kutoa the balanced conclusion bali wamekuwa wanaegemea upande wa mwajiri ili kumkandamiza Mtumishi wa Umma.

Asante.
 
Ndio maana inabidi raia wapiganie upatikanaji wa Katiba mpya itakayosimamisha mifumo imara katika nchi
Nchi ikikosa Rais mzuri mifumo yote inakuwa ya kishetani. Akina Igp siro leo wanafanya kazi kwa uhuru kwa mujibu wa sheria za nchi. Wametukosea sana kwa kushiriki maovu na vitendo vibaya wakati wa Ibilisi Jiwe.
 
kuzuia fao la kujitoa ni sheria kandamizi inabidi hili pia aliangalie kwa umakini. wengi wetu kazi zetu za mikataba inapoisha unateseka sana ni bora mtu achukue mafao yake akafanye biashara zake na kuachana na hizi ajira zenye mateso.
 
Nchi ikikosa Rais mzuri mifumo yote inakuwa ya kishetani. Akina Igp siro leo wanafanya kazi kwa uhuru kwa mujibu wa sheria za nchi. Wametukosea sana kwa kushiriki maovu na vitendo vibaya wakati wa Ibilisi Jiwe.
Yule kwangu sioni kama alikuwa binadamu wa kawaida. Binadamu gani anaona fahari watu kupigwa risasi, kuokotwa kwenye viroba, kupotezwa jumla, kudhalilisha watu hadharani n.k.
 
Sio kama wanabambikiwa bali ushahidi ulipo ni hafifu kuwatia hatiani.
... Rais kasema ni kesi za kubambika wewe unasema ni kesi zenye ushahidi hafifu sijui nani mjuvi kuliko mwingine.
 
Mama ana matamanio fulani lakini mifumo yetu imekaa kibabe, kibaguzi na mingi haifuati sheria na katiba ya nchi. Kuna watu wana roho mbaya sana nchi hii, wanateswa wenzao kwa sababu ya kutofautiana vitu vidogo sana hasa upande wa siasa. Ili watu wetu wapate haki na fikra huru inatakiwa tupate katiba mpya na kubadilisha upatikanaji wa Jaji mkuu, Spika wa bunge, majaji, wakuu wa taasisi i.e takukuru, police, etc na pia kubadilisha mfumo wa usalama wa taifa ili wawe kwa maslahi ya nchi na siyo chama
Mama anataka kama wewe ni polisi tenda haki
Hakimu tenda haki
Takukuru tenda haki
Polisi tenda haki
NEC tenda haki.
 
... kumbe hii issue ya kubambika kesi nikajua ni polisi kumbe hadi TAKUKURU ipo? Dah; kwanini hao waliofungua hayo mafaili ya kubambika raia wema kesi wasitimuliwe na kushitakiwa? Huu ujinga utaendelea kutamalaki hadi lini!
Shida ipo kwa waliokwamia bado awamu,ile nawaliokubali kutekeleza mawazo ovu almuradi mkono uende kinywani,hao ni wakusaka na kufurushwa kwani wataendelea na uchafuzi na kutaka kuikwamisha nia njema iliyopo kwakuwa walinufaika,au kujinufaisha na mfumo walioupenda.
 
Lazima tuwe na sheria ya watu wanambambikia watu makosa,hivihivi yatajirudia..Bunge limelala,tungeni sheria,ili suala hamlioni???
Walikuwa mbio kuipitisha miswaada kandamizi waliyoona inamaslahi kwao kwa hati za dharura,ila zile za kulisaidia taifa haikupewa kipaumbele kwa hizo hati za dharura,kama za kuwadhibiti wa bambikia kesi.
 
Back
Top Bottom