Rais Samia: TAKUKURU wamefuta kesi za kubambikizia 147, Polisi na nyie jitazameni
Mambo mengine tusipende kuwaonea tu watu.hivi mkuu wewe binafsi ukipewa changamoto na bosi wako unaweza kujiuzulu?
Mkuu hili la kuwabambikia Raia kesi ni kashfa kubwa kwa Jeshi lenye jukumu la kuwalinda Raia na mali zao. Ni Raia wangapi waliohukumiwa kwa kesi na ushahidi wa kuwabambikia?? Kwa mfano Raia anakamatwa na kubambikiwa madawa ya kulevya ama silaha. Hapo shahidi ni Polisi na ushahidi ni kile alichodai kamkuta nacho Raia.

Hapa ningeshauri Mama SASHA angeunda Tume chini ya Mawakili Wabobezi kupita kwenye Magereza yote Nchini kuwaibaini wote walioonewa. Ninaamini wako wengi Magerezani.
 
Samia ana huruma juu ya waTanzania lakini huruma yake inakosa mipaka na baadhi ya watu wanaitumia huruma hiyo kupenyeza ajenda zao kwa manufaa yao......matamko yake mengi yako kisiasa badala ya kiweledi........

Kiweledi kufuta kesi unazodai za kubambikiza bila ya kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua waliobambikizia watu kesi.........Mama anapaswa kujua kuwa yeye ni rais wa Tanzania wote........
 
Shujaa wa Mazezeta alikuwa Raisi mbovu sana,Raisi asiyefuata Katiba na Sheria,hakujua kwamba kutesa Watu hakuwezi kukuacha salama.. Rot in Hell Zezeta lao.
icon_lol.gif
 
Mkuu hili la kuwabambikia Raia kesi ni kashfa kubwa kwa Jeshi lenye jukumu la kuwalinda Raia na mali zao. Ni Raia wangapi waliohukumiwa kwa kesi na ushahidi wa kuwabambikia?? Kwa mdano Raia anakamatwa na kubambikiwa madawa ya kulevya ama silaha. Hapo shahidi ni Polisi na ushahidi ni kile alichodai kamkuta nayo Raia.

Hapa ningeshauri Mama SASHA angeunda Tume chini ya Mawakili Wabobezi kupita kwenye Magereza yote Nchini kuwaibaini wote walioonewa. Ninaamini wako wengi Magerezani.
Halaiser
Hiyo ni kweli tupu.

Hivi inawezekanaje kwa Jeshi la Polisi linalopaswa kuwalinda raia wake, ndiyo liwe la kuwakomoa raia wake kwa kuwabambikia kesi??

Naunga mkono pendekezo lako, kuwa iundwe Tume Huru, itakayoutafuta ukweli na kubaini ni watu wangapi wapo magerezani kwa kundiwa kesi za kubambika
 
Kabla ya kushangilia shinikizo la rais kwa vyombo vya usalama kuhusu kufutwa kesi zinazoitwa za kubambikiwa watu tujue kwanza kesi zenyewe ni zipi na nani wanahusika kubambikiza kesi hizo
Nasema hivyo kwa sababu kuna kesi za uhujumu mkubwa kama ile ya iptl ambazo zina ugumu kutokana na wahujumu na washirika wao kua na uwezo mkubwa kuvuruga ushahidi au kuzuia ushahidi. Isitoshe licha ya matendo ya uhujumu wao kuleta madhara makubwa kwa uchumi wa nchi watu hao wakiachiwa eti kwa kukosekana ushahiti bila shaka wataendelea kutumia mahakama kulihujumu taifa kwa kufanya madai ndani na nje ya nchi ambayo yatakua na athari kubwa kwa uchumi wetu.
Kwa hivyo yafaa serikali kuweka wazi kesi zipi zinaitwa za kubambikiza na nani wanashutumiwa kubambikiza. Na kwamba hatua gani zinachukuliwa kwa wabambikizaji. Vinginevyo tutaona fisadi wakubwa wakubwa ambao baada ya kutupwa lupango tumeona utulivu mkubwa wa uchumi na kupungua kwa kasi hujuma kwa uchumi wa nchi.
Wewe akili yako ni ndogo sana. Ya iptl ni ya kubambika? Tuanzie hapo kwanza
 
Wananchi wa nchi hii wamekuwa wakitoa malalamiko yao ya muda mrefu sana, kuwa Jeshi la Polisi linawabambikia kesi wananchi wasio na hatia, hususani wale wanaowaona wanà mlengo wa kisiasa wa vyama vya upinzani.

Kauli hiyo imekuwa ikipingwa vikali na Jeshi la Polisi, likidai kuwa Jeshi la Polisi linafanya kazi yake kwa weledi na kila mshukiwa wa kesi anapaswa ajibu mashtaka yake kwenye vyombo vya sheria.

Hata hivyo leo hii Rais Samia Suluhu Hassan amekitengua kitendawili hicho kwa kueleza ukweli kuwa Jeshi hilo linawabambikia kesi wananchi wasio na hatia na hivyo kuleta msongamano mkubwa usio na ulazima huko magerezani.

Kwa kauli hiyo iliyotoka mdomoni kwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, ni kwanini IGP Sirro hataki kujiuzulu??

Kama IGP Sirro atagoma kujiuzulu, basi tunamuomba Rais Samia Suluhu, amfute kazi Mkuu huyo wa Jeshi la Polisi, kwa kuwa amekuwa akidanganya kwa kusema kuwa Jeshi lake linafanya kazi kwa weledi, wakati katika hali halisi, linafanya uonevu wa hali ya juu kwa wananchi wasiokuwa na hatia.

Tukumbuke pia wajibu namba moja wa Jeshi la Polisi nchini ni kuwalinda raia na mali zao.
IGP Sirro ni askari mwema na mzuri ila amepata bahati mbaya sana kufanya kazi na Katili Jiwe.

Amemchafua sana
 
wacha twende tutafika nchi ya ahadi anayotupeleka mama.

nchi ambayo kila mtu atabembelezwa achague adhabu ipi inamfaa baada ya kutenda kosa.
mtu anatenda kosa barabarani makusudi anashauri aonywe[emoji23][emoji23][emoji23].

uzuri ni kwamba hazina hakuna biashara inafanyila kule,zinaingia ambazo zilitoka[emoji2223][emoji2223][emoji2223]
Mimi nimeanza kuingiwa na wasiwasi kuwa ninyi sio Watanzania mbona mnapenda ukatili ukatili sisi Watanzania tuna hulka moja ya UPENDO au ninyi ni Interehamwe?
 
IGP Sirro ni askari mwema na mzuri ila amepata bahati mbaya sana kufanya kazi na Katili Jiwe.

Amemchafua sana
Utendaji kazi wake umeingia doa, kwa kuwa huyo mwendazake, anayedaiwa kuwa ndiyo aliyekuwa anamuagiza kufanya uovu wote huo, ametangulia mbele ya haki...........

Sasa balaa kamuachia IGP Sirro, ambaye ameelezwa hadharani na Rais Samia Suluhu, kuwa Jeshi lake ndilo linawabambikia kesi raia wasio na hatia!
 
Hii inchi bana [emoji28], Takukuru [emoji23][emoji23][emoji23], Unapamba na rushwa kwa kubambikia watu kesi
 
Ndiyo maana ni muhimu, kuchunguza kwa umakini, kabla ya mtu kumwingiza kwenye mfumo wa utawala, kujua kama huyo mtu ana Roho wa Mungu au ana roho ya ibilisi...
Mimi ninamuunga mkono Mhe. Raisi Mama Samia Suluhu Hassan a.k.a Mama SASHA kuhusu kufutia kesi watu waliobambikiziwa makesi bila kosa lolote.

Mimi namuomba Mhe Raisi hasiishie kwenye kuzifuta kesi tu za watu waliobambikiwa kesi bali aende mbali zaidi na kuwachukulia hatua kali wale wote waliofaidika na mpango mzima wa kuwaumiza watanzania wenzetu! Kuna watu wameumia sana nchi hii bila kosa lolote.
 
Mimi nimeanza kuingiwa na wasiwasi kuwa ninyi sio Watanzania mbona mnapenda ukatili ukatili sisi Watanzania tuna hulka moja ya UPENDO au ninyi ni Interehamwe?
sijui wewe utatuitaje,ila kwa sababu ya Tanzania sio ishu.
 

Mikumi tena kwa Madame President.

Ni kweli haiwezekani mtu anakaa jela miaka miwili halafu tunaambiwa uchunguzi haujakamlika,sasa kama hamjakamilisha uchunguzi ya nini kumkamata?
 
Kwakweli Samia suluhu amejifunza mambo mengi kupitia mapungufu ya mtangulizi wake. Hapendi kuendeleza mabaya. Tutarajie hata sheria kandamizi hapo mbeleni zitakuja kupelekwa Bungeni kwa marekebisho
Atleast its made difference yo yhose 147 individuals. Lakini anatakiwa aweke process itakayo prevent that from ever happening again!
 
Back
Top Bottom