Mkuu hili la kuwabambikia Raia kesi ni kashfa kubwa kwa Jeshi lenye jukumu la kuwalinda Raia na mali zao. Ni Raia wangapi waliohukumiwa kwa kesi na ushahidi wa kuwabambikia?? Kwa mfano Raia anakamatwa na kubambikiwa madawa ya kulevya ama silaha. Hapo shahidi ni Polisi na ushahidi ni kile alichodai kamkuta nacho Raia.Mambo mengine tusipende kuwaonea tu watu.hivi mkuu wewe binafsi ukipewa changamoto na bosi wako unaweza kujiuzulu?
HalaiserMkuu hili la kuwabambikia Raia kesi ni kashfa kubwa kwa Jeshi lenye jukumu la kuwalinda Raia na mali zao. Ni Raia wangapi waliohukumiwa kwa kesi na ushahidi wa kuwabambikia?? Kwa mdano Raia anakamatwa na kubambikiwa madawa ya kulevya ama silaha. Hapo shahidi ni Polisi na ushahidi ni kile alichodai kamkuta nayo Raia.
Hapa ningeshauri Mama SASHA angeunda Tume chini ya Mawakili Wabobezi kupita kwenye Magereza yote Nchini kuwaibaini wote walioonewa. Ninaamini wako wengi Magerezani.
Wewe akili yako ni ndogo sana. Ya iptl ni ya kubambika? Tuanzie hapo kwanzaKabla ya kushangilia shinikizo la rais kwa vyombo vya usalama kuhusu kufutwa kesi zinazoitwa za kubambikiwa watu tujue kwanza kesi zenyewe ni zipi na nani wanahusika kubambikiza kesi hizo
Nasema hivyo kwa sababu kuna kesi za uhujumu mkubwa kama ile ya iptl ambazo zina ugumu kutokana na wahujumu na washirika wao kua na uwezo mkubwa kuvuruga ushahidi au kuzuia ushahidi. Isitoshe licha ya matendo ya uhujumu wao kuleta madhara makubwa kwa uchumi wa nchi watu hao wakiachiwa eti kwa kukosekana ushahiti bila shaka wataendelea kutumia mahakama kulihujumu taifa kwa kufanya madai ndani na nje ya nchi ambayo yatakua na athari kubwa kwa uchumi wetu.
Kwa hivyo yafaa serikali kuweka wazi kesi zipi zinaitwa za kubambikiza na nani wanashutumiwa kubambikiza. Na kwamba hatua gani zinachukuliwa kwa wabambikizaji. Vinginevyo tutaona fisadi wakubwa wakubwa ambao baada ya kutupwa lupango tumeona utulivu mkubwa wa uchumi na kupungua kwa kasi hujuma kwa uchumi wa nchi.
IGP Sirro ni askari mwema na mzuri ila amepata bahati mbaya sana kufanya kazi na Katili Jiwe.Wananchi wa nchi hii wamekuwa wakitoa malalamiko yao ya muda mrefu sana, kuwa Jeshi la Polisi linawabambikia kesi wananchi wasio na hatia, hususani wale wanaowaona wanΓ mlengo wa kisiasa wa vyama vya upinzani.
Kauli hiyo imekuwa ikipingwa vikali na Jeshi la Polisi, likidai kuwa Jeshi la Polisi linafanya kazi yake kwa weledi na kila mshukiwa wa kesi anapaswa ajibu mashtaka yake kwenye vyombo vya sheria.
Hata hivyo leo hii Rais Samia Suluhu Hassan amekitengua kitendawili hicho kwa kueleza ukweli kuwa Jeshi hilo linawabambikia kesi wananchi wasio na hatia na hivyo kuleta msongamano mkubwa usio na ulazima huko magerezani.
Kwa kauli hiyo iliyotoka mdomoni kwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, ni kwanini IGP Sirro hataki kujiuzulu??
Kama IGP Sirro atagoma kujiuzulu, basi tunamuomba Rais Samia Suluhu, amfute kazi Mkuu huyo wa Jeshi la Polisi, kwa kuwa amekuwa akidanganya kwa kusema kuwa Jeshi lake linafanya kazi kwa weledi, wakati katika hali halisi, linafanya uonevu wa hali ya juu kwa wananchi wasiokuwa na hatia.
Tukumbuke pia wajibu namba moja wa Jeshi la Polisi nchini ni kuwalinda raia na mali zao.
itakuwa jambo la kheri
Mimi nimeanza kuingiwa na wasiwasi kuwa ninyi sio Watanzania mbona mnapenda ukatili ukatili sisi Watanzania tuna hulka moja ya UPENDO au ninyi ni Interehamwe?wacha twende tutafika nchi ya ahadi anayotupeleka mama.
nchi ambayo kila mtu atabembelezwa achague adhabu ipi inamfaa baada ya kutenda kosa.
mtu anatenda kosa barabarani makusudi anashauri aonywe[emoji23][emoji23][emoji23].
uzuri ni kwamba hazina hakuna biashara inafanyila kule,zinaingia ambazo zilitoka[emoji2223][emoji2223][emoji2223]
Utendaji kazi wake umeingia doa, kwa kuwa huyo mwendazake, anayedaiwa kuwa ndiyo aliyekuwa anamuagiza kufanya uovu wote huo, ametangulia mbele ya haki...........IGP Sirro ni askari mwema na mzuri ila amepata bahati mbaya sana kufanya kazi na Katili Jiwe.
Amemchafua sana
ππ πππππkazi iendelee
Wanasiasa Wajanja Mno Leo Wanaongea Kama Wametoka Sayari Ya Mars ππ πππππHii inchi bana [emoji28], Takukuru [emoji23][emoji23][emoji23], Unapamba na rushwa kwa kubambikia watu kesi
Mimi ninamuunga mkono Mhe. Raisi Mama Samia Suluhu Hassan a.k.a Mama SASHA kuhusu kufutia kesi watu waliobambikiziwa makesi bila kosa lolote.Ndiyo maana ni muhimu, kuchunguza kwa umakini, kabla ya mtu kumwingiza kwenye mfumo wa utawala, kujua kama huyo mtu ana Roho wa Mungu au ana roho ya ibilisi...
sijui wewe utatuitaje,ila kwa sababu ya Tanzania sio ishu.Mimi nimeanza kuingiwa na wasiwasi kuwa ninyi sio Watanzania mbona mnapenda ukatili ukatili sisi Watanzania tuna hulka moja ya UPENDO au ninyi ni Interehamwe?
labda mama yuko tayari sijui.Bila Kutia Mahaba Yoyote Huu Ndiyo Ukweli
Haki Ikitendeka Tawala Hawawezi Kuzipata...
Atleast its made difference yo yhose 147 individuals. Lakini anatakiwa aweke process itakayo prevent that from ever happening again!Kwakweli Samia suluhu amejifunza mambo mengi kupitia mapungufu ya mtangulizi wake. Hapendi kuendeleza mabaya. Tutarajie hata sheria kandamizi hapo mbeleni zitakuja kupelekwa Bungeni kwa marekebisho