Serikali: Walimu sasa kufanya mtihani wa kupima uwezo kabla ya kuajiriwa

Serikali: Walimu sasa kufanya mtihani wa kupima uwezo kabla ya kuajiriwa

Ule mtazamo kuwa taaluma ya ualimu ni chaguo la mwisho baada ya kukosa fursa nyingine unakaribia ukingoni, baada ya Serikali kutangaza utaratibu mpya katika ajira za taaluma hiyo.

Utaratibu huo, kwa mujibu wa Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda utahusisha, ili uajiriwe kuwa mwalimu utapaswa kufanya mtihani wa kupima uwezo wako.

Kwa sasa, ajira ya ualimu inahusisha kutuma maombi katika tovuti maalum ya maombi ya ajira, kisha anayepata nafasi hufanyiwa usaili kisha kupangiwa eneo la kazi.

Mwananchi
Pia.

-Wasajiliwe na kupewa Leseni kama taaluma zingine( Kabla ya huu mchakato ndio wapimwe kwanza kupitia mitihani)

-Maslahi yao yaboreshwe ili waweze kumudu kuhuisha leseni zao.


Hili la Walimu kupimwa uwezo wao tumelijadili sana humu, naona kilio chetu kinaenda kupata majibu.
 
Wabunge Nao wafanye mitihani kabla ya kuingia mjengoni. 😅
 
Mbona fresh tu. Huo utaratibu ni mzuri, ishu je mtihani utahusu nini, ni yale masomo ya sekondari au ya chuo? Maana chuoni ni mbinu za kufundishia tu na sekondari ni yale masomo ambayo mwalimu atayakuta shuleni akafundishe. Sasa huo mtihani uta base wapi? Kimsingi walimu wanatakiwa kupimwa yale wanayoenda kuyafundisha na si yale waliyofunzwa chuoni. Kuna vituko vingi sana mashuleni walimu kukwepa kufundisha baadhi ya masomo na madarasa
 
Enzi hizo natafuta kazi nikaitwa kufanya interview matokeo yake wanajopo wakaniunganisha niwe miongoni mwao. Kuhoji waombaji wenzangu, nilidharau sana taasisi Ile. Sitasahau Ile siku.

Kwakweli maswali yalikuwa chin ya kiwango. Na uwezo wao ilikuwa duni sana
Duuuh! Kwa hiyo ukapata nafasi ya kazi au uliishia kuwafanyia usahili wenzako?
 
Mbona sisi wahasibu tunafanya ili kupata ajira, vyuo haviaminiki? Tumia akili, hili suala nimelileata jana tu, hata kada ya afya nao wafanyishwe mitihani
Hivi kada ya Afya hadi apate Leseni unajua kapitia hatua zipi?

Kabla ya kupata Leseni anakula mafunzo kwa vitendo kwa mwaka mzima, akimaliza anachapwa pepa akifaulu ndio anapata leseni.

Walimu hatua hiyo hawapiti hata kidogo
 
Lakini mbona itakuwa mkanganyiko? Yaani ufaulu mtihani wa chuo upewe cheti halafu ufeli mtihani mdogo wa kuomba kazi, hii haijakaa vizuri kwa maana kuwa kuna watu hawana vyeti vya chuo wana vya sekondari na leaving certificate za chuo wanaweza kukokotoa hesabu na sayansi kuliko hata hao wenye vyeti vya chuo, nani bora hapo? Yule mwenye uwezo wa kuyatawala maarifa atakayokwenda kuyafundisha shuleni apewe nafasi ya ajira ikibainika ana uwezo huo. Hayo ma GPA weka pembeni pepa iletwe watu wajibu maswali wapate ajira wanazozimudu
 
Mbona fresh tu. Huo utaratibu ni mzuri, ishu je mtihani utahusu nini, ni yale masomo ya sekondari au ya chuo? Maana chuoni ni mbinu za kufundishia tu na sekondari ni yale masomo ambayo mwalimu atayakuta shuleni akafundishe. Sasa huo mtihani uta base wapi? Kimsingi walimu wanatakiwa kupimwa yale wanayoenda kuyafundisha na si yale waliyofunzwa chuoni. Kuna vituko vingi sana mashuleni walimu kukwepa kufundisha baadhi ya masomo na madarasa
Si itaandaliwa Guidelines mkuu, ili walimu wa Arts wawe na pepa yao na walimu wa Sayansi, Uchumi, Biashara wawe na pepa yao.

Mfano mimi ningependekeza hivi, mtihani uwe na category hizi.

- Pepa kuhusu maadili na sheria za utumishi
-Pepa kuhusu mbinu za kufundisha
-Pepa kuhusu masomo husika uliyosomea.
 
Hivi kada ya Afya hadi apate Leseni unajua kapitia hatua zipi?

Kabla ya kupata Leseni anakula mafunzo kwa vitendo kwa mwaka mzima, akimaliza anachapwa pepa akifaulu ndio anapata leseni.

Walimu hatua hiyo hawapiti hata kidogo
Mhasibu hadi kupata CPA unajua amepitia hatua ngapi?????? Uzijizime data
 
Hahahaaa kwani uyo mwalimu analipwa bei gani? Mpk mambo yawe mengi ivyo
 
Ameseme ualimu ni chaguo la mwisho baada ya kufeli sehemu zote. Waziri wa elimu kayasema hao dar Es salaam
1687005713442.jpg
1687001584980.jpg


Mpwayungu Village
 
Mashule mengi ya msingi na sekondari yamejaa walimu wababaishaji na wakaguzi wa elimu hawalijui hili. Unakuta mwalimu anakwepa kufundisha madarasa fulani anajijua ni mtupu kichwani, wanang'angana na darasa la tatu, nne na form one. Hayo madara mengine ukiacha ya awali, la kwanza na pili wanaogopa sana mada zake. Na wakijikakamua kuingia huko wataruka mada wasizokuwa na uwezo nazo kuzikokotoa. Wanafunzi wanabaki weupe mpaka siku ya mtihani wa mwisho wanakutana na maswali ambayo hawakuwahi kufundishwa na walimu wao. Unakuta shule ina walimu wengi ila ni mmoja tu au hakuna mjuzi wa kukukotoa mahesabu ya mada ngumu kama algebra, jometry, sequence and series, matrix na nyingine nyingi zinazofanana na hizo. Kule kwenye physics na chemistry kunako mahesabu ya equation ni balaa. Sasa kama una mwalimu anafundisha msingi na hakupitia hayo mahesabu au alipitia akaambulia sifuri tegemea akipewa kufundisha msingi ataishia la tatu na nne huko juu akifundisha ataruka mada au atababaisha wanafunzi. Walimu wanye mtihani
 
Mhasibu hadi kupata CPA unajua amepitia hatua ngapi?????? Uzijizime data
Kwenye comment yangu umeona nimetaja Mhasibu?

Hapa tunazungumzia walimu mbapo mnaanza kusema na Kada ya Afya ifanyiwe interview ndipo nikakueleza namna wanavyopata leseni zao.

Nikamalizia na kusema Walimu hawapitii hizo hatua, na ndio maana tunaunga mkono kauli ya Waziri
 
Back
Top Bottom