Serikali: Walimu sasa kufanya mtihani wa kupima uwezo kabla ya kuajiriwa

Serikali: Walimu sasa kufanya mtihani wa kupima uwezo kabla ya kuajiriwa

Utakuwa ni upumbavu wa hali ya juu.
Kwa nini iwe kwa walimu tu na si kada zingine?
Kwani walimu ndiyo waliopitisha Azimio la kubinafisishwa kwa Bandari yetu pendwa?
Huyo Prof ni Prof uchwara kabisa.
Yaliyomshinda Mungai J,anataka kuyarudia.
Anawashwa huyu!
 
Utakuwa ni upumbavu wa hali ya juu.
Kwa nini iwe kwa walimu tu na si kada zingine?
Kwani walimu ndiyo waliopitisha Azimio la kubinafisishwa kwa Bandari yetu pendwa?
Huyo Prof ni Prof uchwara kabisa.
Yaliyomshinda Mungai J,anataka kuyarudia.
Anawashwa huyu!
Kuna kada unapata kazi bila usaili?
 
Ule mtazamo kuwa taaluma ya ualimu ni chaguo la mwisho baada ya kukosa fursa nyingine unakaribia ukingoni, baada ya Serikali kutangaza utaratibu mpya katika ajira za taaluma hiyo.

Utaratibu huo, kwa mujibu wa Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda utahusisha, ili uajiriwe kuwa mwalimu utapaswa kufanya mtihani wa kupima uwezo wako.

Kwa sasa, ajira ya ualimu inahusisha kutuma maombi katika tovuti maalum ya maombi ya ajira, kisha anayepata nafasi hufanyiwa usaili kisha kupangiwa eneo la kazi.

Mwananchi

Hivi kuna taaluma Gani inachukua wenye ufaulu mkubwa tofauti na ualimu mfano udocta:uwe na D 3 yaani phys,chem,bios hiyo ni 4 ya 28 (vyuo vyote ngazi ya certificate na diploma)
Engineer:uwe na D 2 za masomo ya science somo lolote (vyuo vyote ngazi ya certificate na diploma )
Uhasibu😀 4 za masomo yeyote
Na kozi zingine zilizobaki sifa ni hizohizo..
Sasa UALIMU MWISHO NI DIV 3 ...sasa utasemaje ualimu ni chaguo la mwisho ndugu mtoa mada

NB: kama ningeambiwa nichague kazi basi ni UALIMU
 
Wasisahau kuwapelekea na package ya mishahara kuanzia M1 na posho ya kufundishia na posho ya nyumba.

Otherwise waache ujinga.
 
Uwaziri ni nafasi za uteuzi, ili uwe waziri lazima kwanza uwe mbunge. Hii ndio mfano wa MWALIMU MKUU, lazima kwanza uwe Mwalimu. Au kuna usaili wa kuwa MWALIMU MKUU?
Ndo maana inabidi ateuliwe Kisha afanyiwe usaili ili nae tumpime uwezo wake
 
Huu mtihani tuanzea na wanasiasa tuanze na wagombea Uraisi tuje kwa wabunge tumalize na madiwa.
Wabunge, rais na madiwani mitihani yao ni uchaguzi, mkiwachagua ina maana mmeona wanafaa...
 
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda ametangaza utaratibu mpya wa ajira za Ualimu unaoelekeza Walimu kufanya Mtihani wa Kuwapima uwezo kabla ya Kuajiriwa, lengo likiwa ni kurudisha hadhi ya taaluma ya ualimu, isitazamwe kuwa chaguo la mwisho baada ya kukosa nyingine

Utaratibu wa ajira hizo kwa sasa unahusisha kutuma maombi katika tovuti maalum ya maombi ya ajira, kisha anayepata nafasi hufanyiwa usaili kisha kupangiwa eneo la kazi.

Kwa mujibu wa Profesa Mkenda, utaratibu huo utaanza kufanyika katika ajira mpya za taaluma hiyo, na hautafuta mchakato wa usaili, akisisitiza utaendelea kama kawaida ili kupata walimu

Amesema, "Wakati wa kutangaza nafasi mpya za ualimu, wakitaka kupata kazi, watafanya mtihani haijalishi tayari umesoma, kwanza itatuondolea matatizo. Kuajiriwa kuwa Mwalimu utafanya mtihani, utaona matokeo, tutaangalia idadi inayohitajika tutachukua waliofaulu tutawaajiri,"


Chanzo: Mwananchi
Kurudisha hadhi gani ambayo ualimu umewahi kuwa nayo hapa nchini!
Ualimu haujawahi pewa hadhi.
Huko vijijini walimu waliheshimika kwa sababu walikuwa wanaweza kula mboga yenye mafuta mwisho wa mwezi tofauti wanakijiji wengine?
 
Enzi hizo natafuta kazi nikaitwa kufanya interview matokeo yake wanajopo wakaniunganisha niwe miongoni mwao. Kuhoji waombaji wenzangu, nilidharau sana taasisi Ile. Sitasahau Ile siku.

Kwakweli maswali yalikuwa chin ya kiwango. Na uwezo wao ilikuwa duni sana
Niliombwa kushiriki usaili kwenye halmashauri moja, wakati huo mimi nikiwa mtumishi kutoka serikali kuu kwenye hiyo wilaya. Sasa akaja jamaa mmoja aliyeomba nafasi ya uhasibu,na kuna bwana alikuwa ndiye acting DT wa hiyo halmashauri akaanza kumpiga maswali. Jamaa akiulizwa swali anawasahihisha kwanza wanaomuuliza kwamba nadhani kwenye swali lenu mnamaanisha hiki na hiki na then anatoa majibu. Kuna muda akawa anawapiga shule wanaomuuliza maswali akiwemo huyo acting DT. Baada ya maswali machache ilibidi wamuache na kumuambia asubiri nje maana alikuwa anawaaibisha.. [emoji23] [emoji23]
 
Mashule mengi ya msingi na sekondari yamejaa walimu wababaishaji na wakaguzi wa elimu hawalijui hili. Unakuta mwalimu anakwepa kufundisha madarasa fulani anajijua ni mtupu kichwani, wanang'angana na darasa la tatu, nne na form one. Hayo madara mengine ukiacha ya awali, la kwanza na pili wanaogopa sana mada zake. Na wakijikakamua kuingia huko wataruka mada wasizokuwa na uwezo nazo kuzikokotoa. Wanafunzi wanabaki weupe mpaka siku ya mtihani wa mwisho wanakutana na maswali ambayo hawakuwahi kufundishwa na walimu wao. Unakuta shule ina walimu wengi ila ni mmoja tu au hakuna mjuzi wa kukukotoa mahesabu ya mada ngumu kama algebra, jometry, sequence and series, matrix na nyingine nyingi zinazofanana na hizo. Kule kwenye physics na chemistry kunako mahesabu ya equation ni balaa. Sasa kama una mwalimu anafundisha msingi na hakupitia hayo mahesabu au alipitia akaambulia sifuri tegemea akipewa kufundisha msingi ataishia la tatu na nne huko juu akifundisha ataruka mada au atababaisha wanafunzi. Walimu wanye mtihani
Hivi haya mambo Huwa mnayajuaje!? Wewe ni mkaguzi!? Kwan wakaguzi hujui ni walimu nao walikimbia!?
 
Na yeye ndo tunapendekeza afanyiwe usaili pengine anauwezo mdogo halafu hatujui
Yeye ashafanyiwa na wananchi kama mbunge. Elewa kuwa Waziri lazima uwe Mbunge, afu waziri ni mshauri wa Rais lazima uelewe.
 
Back
Top Bottom