Serikali yatoa kibali kuagiza mchele nje ya nchi
Mchele uje Kwa kweli,unambiwa mtume mwenyewe alisisitiza sana punje
 
Bwasheee anasema anaruhusu chakula kisombwe holela kwenda nje ili wakulima wanufaike wakati kiuhalisia wanaonufaika ni madalali na walanguzi ambao sasa anawapa shavu jingine la kuagiza chakula kilekile walichopeleka nje kukirudisha nchini kuwauzia wakulima wasio na chakula kwa sasa........eti hizo ndo akili za jiniaz.​
Anavyotoaga macho unafikiri anajiandaa kulamba ndimu
 
Siku zote njia ya mwongo ni fupi tulimwambia Bashe nchi haina chakula stop export ya mazao kwa muda mpaka hali ikawe vizuri, tukapewa majibu kwamba hatumsaidii mkulima shmbani. Leo tena tumeamua kufanya importation ni nini tunafanya??

Viongozi wetu wanatambua wanachofanya??
Jamaa anavyotoaga macho sijui huwa anatumia akili gani
 
Kama mbona una emotional trauma. So unataka na wafanyabiashara waachiwe huru mafuta ya petrol wauze wanavyotaka, pia na sukari.kama vile una chuki na wasiolima. Kuna utaratibu wa kila kitu katika nchi yenye utawala
huyu mtu hajitambui,food security ni suala nyeti sana,yule waziri mjinga anayesema wakulima wanauza nje kwa bei nzuri aje atuambie kwanini sasa hivi tununue nje wakati chakula kipo ndani?,
ushabiki wa kijinga sana.
 
Ngoja sasa muanze kuletewa ma mchele yenye sumu, nakumbuka miaka ya 90s kampuni ya kina Mo Dewji ilileta mchele hatarishi kwa watu, serikali ya mzee Mwinyi ikajikoroga ikaupiga marufuku, lile sakata lake liliua watu wote walioshughulika na huo mchele kuanzia Long room hadi kwa wakemia wa nchi walioshughulikia.

Waliuawa vifo vya utata sana. Kwahio kuruhusu mchele toka nje ni fursa ya kuwaletea wananchi makanjanja na faida kwa wafanyabiashara na wala sio eti njia ya kupunguza makali ya bei ya mchele. Time will tell.
Fear of unknown
 
Hizi ndio akili za mwafrika, tena mtanzania. Mchele umeuzwa nje leo tunaenda kununua mchele nje.
Ni kitu gani hamkielewi hapa?
Kwanza kabisa wakulima wetu wanalima bila KUJALI TIJA.

Haidhuru basi hata bila Tija lakini Bei haikuwa mbaya!

Sasa bei imepaa!

Mazao yako Shambani.

Busara ni kuagiza Mchele kwa wakulima wakubwa ambao wao hulima kwa Tija na kutuuzia.

Hapa kazi ya Serikali ni kuset Standards-basi.

Halafu Serikali inaweka provision Price.. hapo ndipo kukabiliana na Mfumuko wa bei kwa mkakati wa Muda Mfupi!

Halafu tuliambiwa Shehena ya Mahindi nayo inafunguliwa Kutoka NFRA mwezi huu.

Maana yake tutaingia Mwezi wa Tatu tukiwa na uwezo wa kununua mbegu kwa wale tunaolima Masika kwa Sababu bei za Mahindi na Mchele zitakua zimeshaanza kushuka!

Hii ni mipango mizuri!!!
 
mnakula nyie mjini huku shambani hatuvijui
Muda ukifika mtavijua,hata sisi watu wa Mjini mwanzo hatukuvijua,ila sasa tunavijua! Ukija Mjini nileetee Kuku moja la Kienyeji nitafune pls ndg wa shambani!!
 
Mzigo utakuwa mwingi sana na watataka wauuze kwa wingi
lakini tujue kabisa huo (UBWECHE)sio kama huu tuliouzoea wa kwetu hata bila mboga tu unakula!!ule bnana ni kama ugali bila mboga ya maana huuliiii!!!hauna ladha!!lakini potelea mbali uje tu,kwani ni hatari yaani familia zimerudi kwenye ile miaka ya 90 ya kula wali ni anasa!!!
 
Serikali ni ya ajabu sana, unatoa vibali vya kuuza mchele nje ya nchi, na baadae unatoa vibali vya kwenda kuunua huo mchele nje ya nchi, kwanini hiyo pesa na bei inayonunulia nje wasipewe wakulima wa ndani. Na uhakika mchele kwa wakulima upo wa kutosha, tengeneza sera nzuri kwa hao wafanyabiashara wanaotaka vibali kwenda kununua kwa wakulima ili mchele uingie sokoni kwa wingi , supply ikiwa kubwa, demand itashuka tu hivyo bei itashuka pia.
Mkuu sio kweli kwa sasa nchini hakuna mchele wa kutosha kabisa!!yaani huko mikoani maghara mengi yako tupu kabisa!!kwani mavuno ya msimu 2021/22 yalikuwa ni madogo sana,hivyo kupelekea bei ya mchele kupanda toka mwezi sita hivyo wakulima wengi walianza kuuza mazao yao muda huo.Kwa taarifa yako hadi sasa kongo mchele hauendi kutokana na ugumu wa kuupata hapa nchini,wengi waliokuwa wanapeleka ZAMBIA,DRC,BURUNDI NA RWANDA.wameshindwa kupeleka kutokana na upatikanaji wake na bei ziko juu sana.
 
Tutumie akili zetu kutatua tatizo la chakula na si kufikiria kuagiza tu kutoka nje kwamba ndo last resort.

Nguvu kazi ipo, ardhi yenye rutuba ipo na ya kutosha, maji ya mito, vijito na vyanzo vingine pamoja na maziwa yapo, mvua za kutosha zipo.

Nchi yetu haina tatizo la ukame ni nchi safi kabisa kwa kilimo cha mazao yote khasa ya chakula.
Kwa kilimo cha nchi hii,mito,maziwa havijawahi kuwa msaada kwetu tofauti na mvua tu.Kuyatoa maji kwenye hivyo vyanzo na kuyatumia kwenye kilimo ni inshu nyingine kabisa.
 
Wakulima msipoungana na kuwa na chama chenu Cha sauti mtaishia kuwa maskini kama anavyosema Mwigulu hapa [emoji116]
Screenshot_20230207-084644.jpg
 
Back
Top Bottom