Pre GE2025 Tundu Lissu atahadharisha uchaguzi ndani ya chama kuingiliwa na fedha za Rais Samia na mwanae Abdul

Pre GE2025 Tundu Lissu atahadharisha uchaguzi ndani ya chama kuingiliwa na fedha za Rais Samia na mwanae Abdul

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Wananunua madaraka nakuita wenzao wezi.

Mtoa rushwa anapo sahau kuwa rushwa nayo ni jinai na inaondoa integrity vile vile.
anapoona wagombea wanapesa za ajabu ajabu yawezekana yakawa ni mapandikizi ya ccm. Na ukajikuta uongozi mzima wa mkoa ccm tupu, baadae yanajifaragua na kusema narudi ccm, kumbe yalitoka hukohuko.
 
Haya Yameanza leo? Magu alidhibiti hili and soon mama atabana tena hizi pesa za wafadhili wenye agenda
Umenichanganya kwelikweli na andiko lako hili.
"...soon mama atabana tena hizi pesa za wafadhili wenye agenda"?
Sasa sijui kama huyo mama atabana vipi endapo yeye ndiye mwenye agenda!
 
Ningeungana nawe kutia mashaka kama ingekuwa ni wakati wa Magufuli. Hawa wawili wapo karibu sana na Mama; kama alivyo Mbowe.
Chunga sana namba.
Jamaa ameshindwa kuelewa kwamba viongozi wandamizi karibia wote wapo karibu sana na mama au yule jamaa mstaafu adui wao alikuwa mwendazake naona TAL ndiye kagoma kuelewa somo
Ningeungana nawe kutia mashaka kama ingekuwa ni wakati wa Magufuli. Hawa wawili wapo karibu sana na Mama; kama alivyo Mbowe.
Chunga sana namba.
 
Ni wagombea wanahonga? Inatakiwa Chadema iwe macho sana kwa sababu CCM wanaweza kupandikiza watu ili wakivuruge chama.
Ni vizuri kwamba hili limefahamika kungali mapema. CHADEMA wakishindwa kulidhibiti hili, itakuwa ni halali kwao kusambaratika. Hakuna wa kumlaumu tena, bali watajilaumu wenyewe.
 
Jamaa ameshindwa kuelewa kwamba viongozi wandamizi karibia wote wapo karibu sana na mama au yule jamaa mstaafu adui wao alikuwa mwendazake naona TAL ndiye kagoma kuelewa somo
Hili nilianza kulielewa kwa mara ya kwanza niliposikia hotuba ya Mbowe aliyoitoa kule ughaibuni akiwahutubia diaspora wa Marekani kuhusu uhusiano wake na mama kwenye wakati wa mazungumzo ya maridhiano. Toka wakati huo; na baadaye kidogo kufuatiya sarakasi zilizofanyika ndani ya chama kupoza msimamo waliokuwa wamufikia kama chama kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa na ule uchaguzi mkuu.

Hitimisho langu baada ya hapo, nikajuwa CHADEMA ya Mbowe tayari wanajiandaa kuungana na CCM ya Samia kwenye chaguzi hizo na serikalini endapo kama Samia atapenya kwa njia yoyote atakayoitumia kuendelea madarakani.

Msimamo wangu huo, sasa unazidi kuimarika, mambo kama haya anayoyazungumzia Tundu Lissu kwenye mikutano hii.

Sasa sijui CHADEMA itakuwaje, na inawezekana pia tukaanza kuulizana swali kama hilo huko ndani ya CCM. Sijui.
 
Naangalia maandamano namuangalia Lissu nawaangalia wandamanaji ...kuna sauti ya Mungu inatembea!!!
 
Umenichanganya kwelikweli na andiko lako hili.
"...soon mama atabana tena hizi pesa za wafadhili wenye agenda"?
Sasa sijui kama huyo mama atabana vipi endapo yeye ndiye mwenye agenda!
Hana agenda unayotaka ionekane hivyo
 
AISEEE!.
Tulisha sema humu. Pesa ya Mwarabu itamwagika uchaguzi utakapowadia; lakini naona wameamua kuwahi mapema.
Pesa sasa hivi iko kila mahala mpaka kwenye halmashauri vijijini, ndani ya ccm,kwenye wilaya,vijiji vitongoji nk kwa kofia ya mikopo kwa vikundi,miradi na watu binafs.Na hii sasa naona ni mpaka kwenye Upinzani zimetua. Hii hatari Nyerere huko aliko anajuta.Madaraka kwa pesa.Jamani Rupia haijawahi kushindwa CDM ni tegemeo la wananchi msihongeke kirahisi hivyo ondoeni makapi yarudi huko. Shida ni Kanda ya Nyasa. watchout!
 
Kuna fedha za ajabu ndani ya Chadema ambazo chanzo chake hakijulikani. Hizi hela kama siyo za Abdul na mama yake, ni za nani?

Kuna fedha za ajabu, Iringa, njombe na kwingineko. Pesa za Abdul na mamake zitatuangamiza. Chagueni viongozi ambao hawatatuangamiza. Kuweni macho na hizo pesa. Mkavhagueni viongozi wanaowaamink, siyo wanaowaonga.

Tunapohangaika kufanya mikutano ya hadhara, hatuna hela. Tunaposwekwa ndani, hakuna hela. Kwemye chaguzi, hizi pesa zinayoka wapi? Kuweni macho na hizi pesa chafu za yuda Iskarioti.

View: https://www.youtube.com/live/FoVe12k-pog?si=mcWmwLLODWK55UEW
Tundu Lissu Iringa leo...MoDs Futeni tena.

Hizi wanazozunguka Nchi nzima wamezitoa wapi?
 
Mnaparurana wenyewe kwa tamaa zenu halafu lawama mnapeleka kwingine.Kundi la maskini na kundi la kibosile tuone nani atashinda.
 

Wenyeviti wa mitaa walia na Halmashauri kuhusu posho​

November 11, 2023 2 min read
Na Lubango Mleka, Times Majira Online – Igunga.

WENYEVITI wa Serikali za mitaa Mamlaka ya mji mdogo Igunga mkoani Tabora wameilalamikia Halmashauri ya wilaya ya Igunga kwa kutowalipa posho zao za kila mwezi shilingi laki moja kwa zaidi ya miaka miwili na nusu.

Wenyeviti hao wametoa malalamiko hayo kwenye ofisi ya Mamlaka ya Mji mdogo Igunga wakati wakizungumza na waandishi wa habari na ueleza kuwa walishatoa malalamiko hayo kwa aliyekuwa Waziri wa TAMISEMI Sulemani Jafo wakati huo, ambapo kwa sasa wamemuomba Waziri mwenye dhamana kuingilia kati suala hilo.
IMG-20231110-WA0032-1024x576.jpg
Wenyeviti wa Serikali za mitaa katika Halmashauri ya Mji Mdogo wa Igunga wakitoka katika ofisi hizo baada ya kuongea na waandishi wa habari juu ya madai yao ya posho kwa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
Wamesema hali hiyo imesababisha hadi wengine wameshastaafu na wengine kufariki jambo ambalo linawasababisha kuishi kwa shida pia walio kazini kuwa katika hatari ya kushawishika kupokea rushwa pindi wanapotoa huduma kwa wananchi.
Hawa Hamis mwenyekiti (viti maalumu) amesema wamekuwa wakifuatilia madai yao ya fedha mara kwa mara bila mafanikio.

“Kwa kweli sisi Wenyeviti wa Serikali za Mitaa katika Mamlaka ya Mji Mdogo Igunga halmashauri yetu haitutendei haki kwani hizo posho za shilingi laki moja kila mwezi ni haki yetu lakini kila tunapofuatilia tumekuwa tukiahidiwa bila mafanikio,”.
IMG-20231110-WA0034.jpg

Wamesema kuwa, kutokana na hali hiyo wamekuwa wakifanya kazi katika mazingira magumu kwani wao ndio wana watu katika mitaa yao ambapo kila siku lazima watoe huduma mbalimbali na huduma zingine zinahitaji kuchapisha karatasi za vibali vya kuwapatia wananchi ikiwemo kupeleka mifugo yao mnadani, kudhamini Polisi na Mahakamani
Serikali ndio inapaswa kulipa wafanyakazi hawa sio CCM
 
Kuna fedha za ajabu ndani ya Chadema ambazo chanzo chake hakijulikani. Hizi hela kama siyo za Abdul na mama yake, ni za nani?

Kuna fedha za ajabu, Iringa, njombe na kwingineko. Pesa za Abdul na mamake zitatuangamiza. Chagueni viongozi ambao hawatatuangamiza. Kuweni macho na hizo pesa. Mkavhagueni viongozi wanaowaamink, siyo wanaowaonga.

Tunapohangaika kufanya mikutano ya hadhara, hatuna hela. Tunaposwekwa ndani, hakuna hela. Kwemye chaguzi, hizi pesa zinayoka wapi? Kuweni macho na hizi pesa chafu za yuda Iskarioti.

========

Tundu Lissu akiwa mkoani Iringa uwanja wa Mwembetogwa jana May 03, 2024 ametahadharisha kuhusu pesa nyingi ndani
Dalili za kuweweseka, yaani hela za Samia inakuaje ziwepo huko Chadema?

Au mgombea wake maji ya shingo?
 
Kuna fedha za ajabu ndani ya Chadema ambazo chanzo chake hakijulikani. Hizi hela kama siyo za Abdul na mama yake, ni za nani?

Kuna fedha za ajabu, Iringa, njombe na kwingineko. Pesa za Abdul na mamake zitatuangamiza. Chagueni viongozi ambao hawatatuangamiza. Kuweni macho na hizo pesa. Mkavhagueni viongozi wanaowaamink, siyo wanaowaonga.

Tunapohangaika kufanya mikutano ya hadhara, hatuna hela. Tunaposwekwa ndani, hakuna hela. Kwemye chaguzi, hizi pesa zinayoka wapi? Kuweni macho na hizi pesa chafu za yuda Iskarioti.

========

Tundu Lissu akiwa mkoani Iringa uwanja wa Mwembetogwa jana May 03, 2024 ametahadharisha kuhusu pesa nyingi ndani ya chama hicho kuelekea chaguzi za ndani nchi nzima.

Tundu Lissu: Kuna mtafaruku mkubwa sana wa uchaguzi ndani ya chama chetu, kuna pesa nyingi ajabu kwenye uchaguzi huu. Hela ambayo tukisema tufanye mikutano, tutafute vyombo vya matangazo, huwa haipo.

Leo kwenye uchaguzi kuna hela ya ajabu, nyie mnafikiri hii hela ni ya wapi? Nyie mnafikiri hii hela ni ya nani? Mnafikiri hii hela itatuacha salama?

Ukitaka kujua tu kwamba hatuko salama, fatilia mitandaoni. Sasa nayazungumza haya kwa wananchi, na nayazungumza viongozi wayasikie, hizo pesa kwanza sio za Chadema kwasababu sisi huwa hatuna hela siku zote.

Kwahiyo hizi hela ni za nani? Kama sio za Abdul na mama yake! Nyie mnafikiri ni za nani? Na zinavyosambazwa hivi ni kwaajili ya manufaa ya chama chetu?

Sasa nyie wananchi wa Iringa mimi nawaombeni, kwasababu niliambiwa nisije kuzungumza kwenye mkutano huu, nisije kabisa, niliambiwa nisubiri uchaguzi upite ndio nije, yaani nisubiri mchafuane na kukatana mapanga na kutukanana, kuraruana halafu mkishararuana vya kutosha ndio nije.

Nawaombeni sana muwe macho na hizi pesa, nimesema ni za Abdul na mama yake, zitatuangamiza tusipoangalia na sio Iringa peke yake, ni kila mahali.
Dalili za kuweweseka, yaani hela za Samia inakuaje ziwepo huko Chadema?

Au mgombea wake maji ya shingo?

View: https://twitter.com/Sisimizi3/status/1786241828036985268?t=ftaN6u1Guu1cMwnRJrBe3w&s=19
 
Inahitaji akili kubwa kuelewa anapoona wagombea wanapesa za ajabu ajabu yawezekana yakawa ni mapandikizi ya ccm. Na ukajikuta uongozi mzima wa mkoa ccm tupu, baadae yanajifaragua na kusema narudi ccm, kumbe yalitoka hukohuko
Pesa za ajabu ajabu ndio pesa zipi? Sugu na Lisu au Msigwa nani ana pesa?

Umaskini ndio uweledi? Huu ni ujinga wa wajima,ni wapi huko pesa Huwa haitumiki kwenye chaguzi?
 
Pesa za ajabu ajabu ndio pesa zipi? Sugu na Lisu au Msigwa nani ana pesa?

Umaskini ndio uweledi? Huu ni ujinga wa wajima,ni wapi huko pesa Huwa haitumiki kwenye chaguzi?
Ndiyo maana nimekwambia akili kubwa ndiyo inang'amua pesa za ajabu ajabu ndizo ziliwanunua akina Joshua nasari na akina harima mdee sio rahisi wewe mwenye ubongo wa kuku kuelewa
 
Kuna fedha za ajabu ndani ya Chadema ambazo chanzo chake hakijulikani. Hizi hela kama siyo za Abdul na mama yake, ni za nani?

Kuna fedha za ajabu, Iringa, njombe na kwingineko. Pesa za Abdul na mamake zitatuangamiza. Chagueni viongozi ambao hawatatuangamiza. Kuweni macho na hizo pesa. Mkavhagueni viongozi wanaowaamink, siyo wanaowaonga.

Tunapohangaika kufanya mikutano ya hadhara, hatuna hela. Tunaposwekwa ndani, hakuna hela. Kwemye chaguzi, hizi pesa zinayoka wapi? Kuweni macho na hizi pesa chafu za yuda Iskarioti.

========

Tundu Lissu akiwa mkoani Iringa uwanja wa Mwembetogwa jana May 03, 2024 ametahadharisha kuhusu pesa nyingi ndani ya chama hicho kuelekea chaguzi za ndani nchi nzima.

Tundu Lissu: Kuna mtafaruku mkubwa sana wa uchaguzi ndani ya chama chetu, kuna pesa nyingi ajabu kwenye uchaguzi huu. Hela ambayo tukisema tufanye mikutano, tutafute vyombo vya matangazo, huwa haipo.

Leo kwenye uchaguzi kuna hela ya ajabu, nyie mnafikiri hii hela ni ya wapi? Nyie mnafikiri hii hela ni ya nani? Mnafikiri hii hela itatuacha salama?

Ukitaka kujua tu kwamba hatuko salama, fatilia mitandaoni. Sasa nayazungumza haya kwa wananchi, na nayazungumza viongozi wayasikie, hizo pesa kwanza sio za Chadema kwasababu sisi huwa hatuna hela siku zote.

Kwahiyo hizi hela ni za nani? Kama sio za Abdul na mama yake! Nyie mnafikiri ni za nani? Na zinavyosambazwa hivi ni kwaajili ya manufaa ya chama chetu?

Sasa nyie wananchi wa Iringa mimi nawaombeni, kwasababu niliambiwa nisije kuzungumza kwenye mkutano huu, nisije kabisa, niliambiwa nisubiri uchaguzi upite ndio nije, yaani nisubiri mchafuane na kukatana mapanga na kutukanana, kuraruana halafu mkishararuana vya kutosha ndio nije.

Nawaombeni sana muwe macho na hizi pesa, nimesema ni za Abdul na mama yake, zitatuangamiza tusipoangalia na sio Iringa peke yake, ni kila mahali.
Matokeo ya kupokea makapi kutoka CCM na kuwapa audience kubwa ndani ya chama.

Rushwa imeasisiwa na Chanzo Cha Matatizo na inarnea kwa kasi kubwa
 
Back
Top Bottom