Pre GE2025 Tundu Lissu: Tuna upungufu wa kutisha wa fedha kwa ajili ya shughuli za Chama (CHADEMA), msiniulize nimekuta nini, jibu halitakuwa zuri!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
si alisema pesa zinatumika vibaya, nae ataweka vizuri matumizi ya pesa za chama?

ziko wap hizo pesa sasa gentleman?🐒
Na alisena yeye kama makamu mwenyekiti kuwa Chadema pesa ziko nyingi zinaishia kuliwa makao makuu hazifiki matawini

Akasema akishika atahakikisha hizo pesa zinafika matawini.Azifikishe sasa

Ulaghai una mwisho kampaka matope Mbowe weeee

Atakayechanga atakuwa akili hana aambiwe alizosema zipo ashushe matawi
 
Lissu na safari mpya ya kujenga chama.
JokaKuu zitto junior Tindo Retired Lusungo

 
Ndani ya miaka 5 iliyopita mh.Katibu Mkuu wa. cHADEMA ndg.John Mnyika amesema kuwa walipata RUZUKU bilioni 12.5....yaani hizi zote zilitumika na kuisha ?!!!

TL aelewe kuwa kazi ya kuuona ufukara wa CHADEMA ndio imeanza hivyo kwani wale wafanyabiashara "piga ua CDM" pale kariakoo wamejiapiza kuwa hawatatoa tena michango yao kwa mwenyekiti wa CDM ambaye ni "wa kuja na asiyeamini katika GENERAL OBJECTIVES za kuanzishwa chama hicho ".

Ni muda wa kuendelea kusikilizia maumivu ya UKATA wa kutisha hapo viungani CHADEMA ...
 
Maji ya shingo....

Ni rahisi sana ukiwa jukwaani kumzodoa mnenguaji kuwa haendi sambamba na miondoko ya ngoma.....
 
Hapo ndio hoja yako ilipoishia sasa kama alisema atapanga matumizi bila ya kuwepo na pesa utayapangaje matumizi?

Yeye ameingia juzi na ameona hali ni tofauti sasa kinachofanyikaan ni kufanya utaratibu ili pesa ipatikane halafu apange matumizi hata hili linakushinda kuelewa ndugu mtafiti?

Kazi ipo sana kwa watafiti wetu
 
Yeye afanye kazi aache siasa za kulalamika,kama hakuna hela aseme chama hakina hela wanachama watachanga na siyo kulalamika kwamba hakukuta kitu wakati anajuwa fika Mwenyekiti mstaafu ndiyo alikuwa mfadhili wa Chama.
Sikiliza video boss, kasema wazi chama hakijawahi kufadhiliwa na mtu mmoja, chama ni cha wanachama.
 


Usirukie mambo yasiyokuhusu. Kwani alikuwa anakuambia wewe?

Lisu alikuwa anaongea na wanachama na wapenzi wa CHADEMA, cha ajabu wanaochanganyikiwa na kukurupuka ni chawa wa CCM! Hivi hao machawa watakuwa na angalao hata ile akili ndogo kabisa ya mwanadamu?
 
Sikiliza video boss, kasema wazi chama hakijawahi kufadhiliwa na mtu mmoja, chama ni cha wanachama.
Awaambie wanachama wachangie /Waanzishe miradi ili kuondokana na hiyo michango ya kila mara.
 
Reactions: Tsh
Bado hamjasema. Maana moto mnakwenda kuupata.
 
Kusema tu kuwa jibu halitakuwa zuri tayari ametoa jibu.
Tundu Lissu ni mwanasiasa wa hovyo mno.... analeta UANAHARAKATI siasani.......

Mwenzake Trump ni mwanaharakati siasani ila anajivunia UTAJIRI alionao.....

TL yeye ni masikini.....hivi hajui gharama za MASKINI JEURI ?!!! Ha ha ha ha
 
Reactions: Tui


Wewe inaonekana kichwani ni kutupu kabisa!

Hata kama alisema hivyo, kama kwa sasa hakuna pesa, unataka afikishe nini huko chini?

Ungekuwa na akili japo kidogo, ungesubiri kwanza ipite angalao hata miezi 6, wanachama na wapenzi wa chama wachangie, na hiyo ruzuku ndogo iingie, halafu uone matumizi yake yanakuwaje, ndipo uwe na haki ya kusema na kuhukumu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…