dronedrake
JF-Expert Member
- Dec 25, 2013
- 23,901
- 58,103
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Looo huo ni uonevuMkuu,Kwamba huo wimbo wamejifunzia hapo shuleni?Mbona tuna kazi nchi
Umenichekesha sana mkuu. Au kutokana na kukaa na wanafunzi wanageuka kuwa wanafunzi piaNimezungukwa na walimu nimelelewa na mwalimu nawapata vizuri sana vichwa vyao, kiufupi mwalimu ni mwanafunzi asiyevaa uniform
Nipatie official statement mkuu...kama hutojali.Waziri Wa Elimu, Sayansi Na Teknojia Anaitwa Professor Adolf Mkenda
Ndiyo Ameagiza Hayo
Kabisa kwenye hili wameonewa kiukweli[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Na hao hao CCM watayakata mauno jukwaani ili wapewe kura
2015 walicheza mapanga ya TMK .
Si ajabu mwaka 2025 wakaja na zuchu..na hata kwenye ziara zake wanaenda naye ,si ndio hizo hizo nyimbo anazoimba?
Ila hapo wanawaona walimu wakosaji.
Hiyo nyimbo watoto wengi wanapenda,na usipowawekea wanaidai.
Wawaache walimu.
Kwanini BASATA hawakuufungia huo wimbo kama wanajua madhara yake na kwamba haufai?wimbo wa kukata viuno, siyo nzuri ni ku inculcate sense ya "ngono" kwa watoto
Akili zetu tz tunazijua wenyewe,sasa kama nyimbo hazina maadili kwa nini wali zipitisha,huu wimbo na ule wa nay,upi hauna maadili.View attachment 2801642
Baada ya kipande cha video kinachowaonesha watoto wa shule za msingi wakicheza wimbo wa msanii Zuchu ‘Honey’ wilayani Tunduma kusambaa mitandaoni, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda ameagiza walimu wakuu wawili wa shule hizo wavuliwe vyeo.
Amesema hayo nje ya Bunge jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu video hiyo ambapo pia amepiga marufuku wanafunzi kucheza nyimbo zisizo na maadili na kuwataka walimu kuwa wasimamizi wa maadili pindi wanafunzi wawapo shuleni.
“Tumeshatambua shule yenyewe iko Tunduma, kulikuwa na kikundi kimeenda kutoa msaada shuleni pale, baada ya kutoa msaada ule kikaweka na muziki halafu wanafunzi wakacheza, na maudhui ya muziki wenyewe kila mtu ameusikia sina haja ya kuurudia,” amesema Profesa Mkenda.
Ameongeza, “tumeongea na wadhibiti ubora wapeleke taarifa kule, mkurugenzi awaondoe walimu wakuu wa shule mbili; moja shule ya Tunduma na nyingine ambazo ni kama shule pacha, waondolewe madaraka ya ukuu wa shule watafutwe wakuu wengine wa shule. Tunafanya hivi ili kutuma ujumbe, walimu wakuu tusaidieni msiruhusu vitu kama hivi viingie mashuleni.”
Kwa upande wake Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima amempongeza Profesa Mkenda kwa kukemea kitendo hicho na kutoa wito kwa watoa huduma wote na wanaohudumia watoto kusimamia malezi na makuzi ya watoto.
Aliyewasimamisha kazi atakuwa ni mpumbavu.Siongei mengi... Ni kweli!?? Wamefukuzwa kazi!?? Anyone.,..!!
View attachment 2801918
Hawajawa demoted mkuu, waziri kasema wavulie tu vyeo vya ukuu wa shule.Mkuu kama una official statement ya demotion au video..
Naomba uiweke hapa..
Hivi Watanzania akili tumemkopesha nani siku hizi? Huo wimbo una maadili gani ya kumfundisha mtoto? Umeyasilikiliza vizuri hayo maneno yanayotamkwa kwenye huo wimbo? Tunatetea vitu vya kijingaaWaziri husika huyo ni nani!?
Hao Walimu wamefanya kosa gani!??
Ahhh!!!
Huyo Waziri angejua jinsi gani Walimu huku vijijini wanapambana na dropout ya wanafunzi..utoro...this is purely insane, yaani imefika hatua waziri anawanyima watoto haki yao ya msingi ya kucheza na kufurahi?
Wanatishwa sana, wapo kama nyumbu nidhamu ya uoga ndivyo walivyo,Umenichekesha sana mkuu. Au kutokana na kukaa na wanafunzi wanageuka kuwa wanafunzi pia
Wawakatie viuno vizuri hao wapenzi wao siyoMtoto wa miaka miwili ana enjoy vibe la honey, wawarudishe tu hao walimu
Mimi sio niliyewatoa, kwahiyo siwezi kukujibu mcheki Mkenda ndio kawatoaKwa kosa lipi!?
Nitajie Kosa..
That is demotion...Hawajawa demoted mkuu, waziri kasema wavulie tu vyeo vya ukuu wa shule.
Sasa si ndiyo ku-demote?Hawajawa demoted mkuu, waziri kasema wavulie tu vyeo vya ukuu wa shule.
ndo huyo huyo mkuu, tena katoa hayo maagizo akiwa kwenye viwanja vya bunge letu tukufu, na mh dorothy gwajima kamuunga mkonoThat is demotion...
Kama kweli ni huyu Mkenda ninae mjua mimi, atengue hayo maamuzi haraka..