Tunduma: Wakuu wa shule wavuliwa nyadhifa kisa wimbo wa Zuchu (Honey)

Tunduma: Wakuu wa shule wavuliwa nyadhifa kisa wimbo wa Zuchu (Honey)

mkuu acha makasiriko, acha watoto waenjoy kwa muda
Nafikri waziri atakuwa hajachukizwa na kucheza mziki, kilichomwuzi utakuwa ujumbe ulioko kwenye mziki! "Mpenzi wangu akinuna namkatia kiuno". Hivi hata wewe mkuu ukiwa umenuna my wife wako akakuingiza chemba akakutia kiuno utaendelea kununa?
 
Hivi ni nani huyo kaifanya hii furaha ya watoto kuwa tukio la kiharifu?

Hii nchi Kuna namba viongozi wetu wanarukwa na akili.
Sijui ndo kiwewe cha uongozi.


Wakatekeleze mambo ya msingi.
Miaka 60 ya uhuru ,shule bado watoto wanakaa chini
Ila yapo yanaitana kujadili nyimbo ya Zuchu.

Pumbavu sana,wakajadili na Basata
Ama wamwite Zuchu mwenyewe.
Nimeshawatolea povu huko juu mdogo wangu acha tu viongozi mizigo ndo hao na walivyosimama sasa wapo serious na yule maza gwajima poh utasema watu kumbe vilaza tu
 
kabisa mkuu, sijui kwa nn anataka kuwanyima watoto haki yao ya msingi ya kucheza na kufurahi na walimu wao.
Yeye alivyomaliza darasa la 4 na 7
Hakucheza mziki?

Kulivtokuwa na tafrija mbalimbali shuleni,
Waliimba akapera sijui Akapela ?

Wasitutoe kwenye reli
Nchi Ina matatizo mengi sana upande wa elimu
Ya muhimu yamewashinda,,
Sasa wamejitafutulia ya kwao

Hatukuwatuma kufanya kazi ya kujadili nyimbo za kina Zuchu.
 
Kwa kosa lipi!? Kuna kosa gan hapo LA kucheza mziki!!!
FUNKY analogy , issue ni content ya wimbo na kwa age gani . Hawa ni watoto wadogo unawaimbia mambo ya kukata viuno, honey etc etc...siyo sawa. Wanao utawaimbia wimbo huo sebulei?...... anyway inawezekana najibizana na vijana wadogo..kwaheri!
 
Well said. Ukitazama kwenye video yaani ni watoto wote wanaufahamu wimbo na wanauimba mwanzo mwisho. Kama ni kulinda maadili kwa hawa watoto basi serikali ingeanzia kwenye kuhakikisha kwamba nyimbo zisizo na maadili hazipenyi kwenye media na popote kwingine. Pia mtu au taasisi iliyokwenda kufanya jambo lake shuleni walipaswa kujua au kuambiwa na uongozi/mamlaka iliyowapa kibali cha kufanya shughuli yao hapo shuleni kwamba hawapaswi kupiga nyimbo yoyote isiyo na maadili mbele ya watoto. Na kwa mtazamo wangu hata hao walimu wakuu wanaotakiwa kuvuliwa vyeo vyao angalau basi wangepewa onyo tu na siyo kuwavua vyeo baada ya kuteleza kwenye tukio hilo. Ni mara ngapi hata hao mawaziri wameharibu mambo lakini hadi leo bado wapo ofisini?
Yaani Serikali ikulindie maadili ya mtoto wako?

Hii dhana ya kila kitu Serikali serikali inatulemaza sana kwako wewe huo wimbo una maadili?? Maneno yake na vitendo vyake ni vya maadili?? Kama sio kwanini kabla ya serikal tungeanza sisi wazazi kuupinga huu wimbo?? Serikal kupitia waziri wake imeonyesha kuwa huu wimbo sio sisi hao haaaa! Serikal hapa imekurupuka, huko BASATA si wanalipia?

Kwa mawazo huo wimbo haukupaswa kupigwa shule hata kama watoto wanaujua kwasababu hawajajifunzia shule ni huko mtaani na tuseme ule ukweli wimbo hauna maadili hata ingekuwa wewe kwa mwanao usingekubali auimbe auige kwa sababu ya maneno yake
 
FUNKY analogy , issue ni content ya wimbo na kwa age gani . Hawa ni watoto wadogo unawaimbia mambo ya kukata viuno, honey etc etc...siyo sawa. Wanao utawaimbia wimbo huo sebulei?...... anyway inawezekana najibizana na vijana wadogo..kwaheri!
Watu wanabisha tu wanajifanya hawaoni huo wimbo hauna maadili kabisa na haufai
 
Nimeshawatolea povu huko juu mdogo wangu acha tu viongozi mizigo ndo hao na walivyosimama sasa wapo serious na yule maza gwajima poh utasema watu kumbe vilaza tu
Heri sijapoteza muda kuangalia hayo matamko.
Kwanini wasianze kwanza kuzichambua na kuzifungia hizo nyimbo?
Mbona wameziacha zinatrend

Dkt. Gwajima D
Hii ni sawa?
 
FUNKY analogy , issue ni content ya wimbo na kwa age gani . Hawa ni watoto wadogo unawaimbia mambo ya kukata viuno, honey etc etc...siyo sawa. Wanao utawaimbia wimbo huo sebulei?...... anyway inawezekana najibizana na vijana wadogo..kwaheri!
Nchi hii sasa hivi tuna mizazi ya hovyo hovyo sana! Hii ndiyo inaona hata watoto kuwa mashoga ni sawa tu maana ndio usasa huo!
 
Hii siyo warrant ya kuendekeza nyimbo za ngono mashuleni kwa vile miaka 60 hakuna desks...think deep and make rational judgement
Walichukua hatua gani kuzidhibiti?
Shuleni si sawa kuweka nyimbo
Ila kwenye ziara za CCM,Zuchu kutumbuiza nyimbo hizohizo ni sawa?
 
Kwa Umri huo Hakuna sense hiyo

Tumesoma shule hizo hizo na tumeimba nyimbo hizohizo

Ni mawazo ngono yetu watu wazima ndiyo yanangonolize watoyo
Uliimba nyimbo hizo hizo zipi?

Wakati nasoma nyimbo za kupinga ukimwi ulikuepo wa Ferouz Starehe Gharama na Usione Soo wa kundi la wasanii wa Tz lakini tulikua tukienda kwenye matamasha ya ukimwi nyimbo zilipigwa za TOT za Mgeni Kaingia.

Ninaunga mkono adhabu iliyotolewa
 
Mimi kama mwalimu mzoefu nachelea kusema kuwa waziri kakurupuka,shuleni sio mahali pa kujifunza ya darasani tu,kuna extra curriculum ambayo inajumlisha mambo hayo,huo wimbo wa kawaida sana,wasitake kutufanya walimu tuishi kama panya mashinoni

Kama wazirianaona hii comment imemkela na mimi anifukuze kazi,niko shule ya msingi mpigamiti wilaya ya liwale
Unajiamini sana mwalimu si ndiyo...?!
Umesema upo hapo mpigamiti tarafa ya Upwilu...?
Basi sawa ntamtuma mkurugenzi Nantoombe mushi akupige demotion.
 
Walichukua hatua gani kuzidhibiti?
Shuleni si sawa kuweka nyimbo
Ila kwenye ziara za CCM,Zuchu kutumbuiza nyimbo hizohizo ni sawa?
makosa ya BASATA kutouzuia siyo warrant ya kuimbwa mashuleni. Unatumia common sense kama mwalimu Mkuu na mzazi. Issue ni audience ipi wimbo huo unaimbwa. Yes shulni si swa maana kule kuna mitaala na wale ni watoto wadogo
 
Back
Top Bottom