Isitishwe>????? Wewe usitoe na hatuamini tu! hii ahadi ilitolewa wakati Tundu alipomininiwa gololi 38 matokeo yake??Michango isitishwe sasa
Maana kwenye vimedia uchwara
Naona watangazaji washaanza...
Kuwaomba watu watoe hela
Ova
Michango iendelee mkuu!; kwani ilichangwa Kwa sababu Jay ni mtu maarufu au Kwa sababu ni binadamu au ilichangwa Kwa malengo yaliyojificha na Sasa watu wamekasirika kuwa malengo yao yamekwama?Wanasiasa na fursa za kutafuta popularity.
Hapo hapo MNH kutakuwa na wagonjwa makapuku kwelikweli wanashindwa kufanya dialysis kwa kukosa tu fedha but no one will care,lakini kwa mtu maarufu huyu ambaye kashaanza kuomba michango kwa umma serikali inasema italipia full,so michango i-stop.
wewe ni nani hadi ututukane watu zaidi ya milioni 50 ni wapumbavu ?Watanzania walivyo wapumbavu watashangilia na kuruka ruka huku wakibinua makalio kana kwamba waziri ametatua changamoto ya afya kitaifa.
Jiulize wewe, mtoto au mzazi au ndugu yako akiumwa atapata hiyo favour?au ni wale waliokula keki ya taifa wanaipata hiyo neema peke yao?
Tunahitaji kupaza sauti juu ya bima ya afya kwa kila raia wa Nchi hii. Ni heri tutumie fedha kuhudumia afya ya za wananchi wetu huku wakiwa wanapita kwenye barabara zenye foleni kuliko kuwapitisha kwenye flyover wakiwa ndani ya jeneza.
hili lipo toka enzi na enzi, hata kwa Mungu hakuna usawa,hata Yesu aliwahaidi pepo wale jamaa aliosurubiwa nao, utauliza kwanini wale aliwakubalia kuwa nao katika ufalme wa mbinguni huku akiacha wengine wajipiganie wao ?Hiyo sio nongwa. Tatizo sio yeye kusaidiwa. Asaidiwe privately.
Ni discrimination kutumia pesa ya umma kumsaidia mtu mmoja ilhali watu wengine walio katika situation kama yake wakiachwa kujipigania wenyewe!
Pongezi nyingi Kwa serikali.. wametumia busara nyingi hapaWaziri wa Afya, Ummy Mwalimu amesema kuanzia sasa Serikali itagharamia matibabu ya aliyekuwa Mbunge wa Mikumi Joseph Haule Profesa J anayetibiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili hadi hapo atakaporuhusiwa kurudi nyumbani.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu alipofika Muhimbili leo kumjulia hali Msanii huyo.
Pia soma:
Tumuombee sana Profesa J
Mke wa Profesa Jay afunguka, familia yaomba msaada wa matibabu
then anakuja kusaidia mtu mwenye pesa na uwezo, ni ujinga na haupaswi kunyamaziwaView attachment 2117004
Wawakilishi wa nchi kama hawa hawasaidiwi
Bado upo usingizini, wangekua wanasaidiwa wangeshindwaje kulipia matibabu hadi maiti inadaiwa?Umeambiwa bure au kusaidiwa kama Prof J?? hakuna watu wanasaidiwa na serikali kwenye matibabu??
na unavyokuwa unazungumzia wizara ya afya boss ni yeye,hivyo hayo kayasema kwa hisia zake kupitia mgongo wa serikali maana pesa yeye hana inatoka kwetu kwenda kumhudumia tajiri anaejiweza ni ujinga na upumbavuUmmy kasema serikali itagharimia, siyo yeye.
exactlyNchi ya laana yani kiongozi badala ya kupanga strategy ya kusaidia wengi wasiojiweza yeye anakimbilia kusaidia mtu maarufu ili apate kiki kisiasa. Hawa viongozi wetu wana uwezo mdogo sana wa kufikiri
Wewe mtu upo Tanzania hii kweli? Mtu mwenye shida ya matibabu akamuone diwani atasaidiwa?Wewe uko wapi ?
Mbona wanatibiwa ! Na kama Hana Elfu kumi si akamuone hata Diwani wake wa CCM au Mtendaji ili aseme kuwa hawezi kulipa?
Ukumbuke kuwa Matibabu ya Jay. bila kumsaidia ujue atafilisika kabisa.
Matibabu madogo madogo watu wanapewa dawa na serikali Kwa kiwango kidogo Cha magonjwa madogo. Lakini magonjwa makubwa hasa magonjwa yanayotokana na tabia za kimaisha hua Matibabu yake ni ghali sana. Na Kwa Karne hii magonjwa yasiyoambukizwa / yanayotokana na hali ya kimaisha yanawakuta watu wengi sana.
Ndio maana hata Mabeberu hawajajitokeza Afrika kufadhili Matibabu ya magonjwa yatokanayo na tabia za kimaisha mana yanagharama kubwa sana.