Kommando muuza madafu
JF-Expert Member
- Aug 30, 2022
- 3,216
- 7,254
Imekaa sawa hii.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Safi sanaa walitaka kukengeuka waje pamoja tuijenge nchi yetu.Uongozi wa TEC chini ya Father Kitima upo hapo ukumbini ukishuhudia utiaji saini wa mikataba.
Hii Haina tofauti na kelele za chanjo ya uviko kuwafanya mazombie 😁😁Pamoja na kelele zote za watanganyika kuhusu bandari yao kuuziwa mwarabu, bado serikali inayoongozws na rais Samia imepuuza na kuwapa bandari warabu wa DP World.
View attachment 2789020
Leo mikataba 3 ya DP World inasainiwa rasmi.
Wala Bure hawana nguvu hiyo, walikua wakidekezwa tu na wanaowasamehe dhambi...Leo kilajicho lione kwamba Kuna nchi na taasisi zingine binafsi,kwamba Dola Ina nguvu kuliko mbuzi yoyote hapa tzSauti ya wale washika vinubi imedharauliwa!
Fuatilia yanayojiri kutoka Ikulu kwenye Halfa ya utiaji saini wa Mikataba mahsusi 3 ya uwekezaji Bandari ya Dar es salaam, leo Oktoba 22, 2023.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TPA Bw. Plasduce Mkeli Mbossa amesema uwekezaji huu wa Serikali kupitia TPA utaongeza ufanisi kwa huduma za meli na shehena, kupunguza muda kwa bandari katika kuchakata nyaraka, kuongezeka kwa mapato ya serikali, kupungua kwa udanganyifu, kuimarisha nafasi ya ushindani kwa bandari, kuongeza ajira na kupunguza gharama za usafirishaji wa mizigo kuja bandari ya Dar es salaam.
Aidha, muda wa usafirishaji wa mizigo kutoka mashariki ya mbali utapungua kutoka siku 30 hadi 15.
Haitegemewi kufungwa kwa biashara zozote za wazawa zinazofanyika bandarini.
Aidha, Mkeli Mbossa amefafanua kuwa wastani wa meli kukaa nangani ikisubiri huduma ni siku 5 hadi 10 huku bandari ya Mombasa ni siku 1.25 na Bandari ya Durban ikiwa ni wastani wa siku 1.6. Hii inatokana na kukosekana kwa uwekezaji mkubwa wa muda mrefu ambao ungepelekea kuongezeka kwa namba za gati. Pia, gharama za kusafirisha makasha ni kubwa, jambo linalofanya kupanda kwa bei ya bidhaa kwa mtumiaji wa mwisho.
Mikataba inayosainiwa leo ni baina ya Nchi mwenyeji, mkataba wa ukodishaji na uendeshaji wa gati namba 4-7 lakini pia kutakuwa na sehemu ambayo gati 0-3 zitaendeshwa kwa ushirikiano wa pamoja kati ya TPA na kampuni ya DP World kwa shughuli za kibiashara na shughuli za kiserikali.
Mikataba hii haihusishi eneo lote la bandari wala bandari zingine za Tanzania. Upande wa gati namba 8-11, mchakato wa kumpata mwendeshaji mwingine umeshaanza kufanyika na akipatikana mwekezaji mwingine mwenye sifa atakabidhiwa na sio DP World.
Fuatilia yanayojiri kutoka Ikulu kwenye Halfa ya utiaji saini wa Mikataba mahsusi 3 ya uwekezaji Bandari ya Dar es salaam, leo Oktoba 22, 2023.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TPA Bw. Plasduce Mkeli Mbossa amesema uwekezaji huu wa Serikali kupitia TPA utaongeza ufanisi kwa huduma za meli na shehena, kupunguza muda kwa bandari katika kuchakata nyaraka, kuongezeka kwa mapato ya serikali, kupungua kwa udanganyifu, kuimarisha nafasi ya ushindani kwa bandari, kuongeza ajira na kupunguza gharama za usafirishaji wa mizigo kuja bandari ya Dar es salaam.
Aidha, muda wa usafirishaji wa mizigo kutoka mashariki ya mbali utapungua kutoka siku 30 hadi 15.
Haitegemewi kufungwa kwa biashara zozote za wazawa zinazofanyika bandarini.
Aidha, Mkeli Mbossa amefafanua kuwa wastani wa meli kukaa nangani ikisubiri huduma ni siku 5 hadi 10 huku bandari ya Mombasa ni siku 1.25 na Bandari ya Durban ikiwa ni wastani wa siku 1.6. Hii inatokana na kukosekana kwa uwekezaji mkubwa wa muda mrefu ambao ungepelekea kuongezeka kwa namba za gati. Pia, gharama za kusafirisha makasha ni kubwa, jambo linalofanya kupanda kwa bei ya bidhaa kwa mtumiaji wa mwisho.
Mikataba inayosainiwa leo ni baina ya Nchi mwenyeji, mkataba wa ukodishaji na uendeshaji wa gati namba 4-7 lakini pia kutakuwa na sehemu ambayo gati 0-3 zitaendeshwa kwa ushirikiano wa pamoja kati ya TPA na kampuni ya DP World kwa shughuli za kibiashara na shughuli za kiserikali.
Mikataba hii haihusishi eneo lote la bandari wala bandari zingine za Tanzania. Upande wa gati namba 8-11, mchakato wa kumpata mwendeshaji mwingine umeshaanza kufanyika na akipatikana mwekezaji mwingine mwenye sifa atakabidhiwa na sio DP World.
Katika mikataba hii, Serikali itakuwa inapata ada na tozo kutoka DPW ambazo zitaongeza mapato na kupunguza gharama za uendeshaji.
Mkataba huu utakuwa wa miaka 30 na utendaji kazi wa DPW utakuwa unapimwa kila baada ya miaka 5 na sio miaka 100.
Mwenye upeo anaelewa hayo maneno yanamaanisha kitu gani, asiye na upeo atakuita chawa.Tanzania inaelekewa kuwa ni "logistics solution" ya Afrika.
Nna uhakai huko mbeleni tutakuwa kitovu cha biashara kikubwa katika Afrika, lakini kwa leo tutazame tunayoyakabili sasa hivi.
Tunataka kujenga banadari kavu katika mipaka yote ya Tanzania.
Mazao yote ya Tanzania sasa yatakuwa kwenye soko la dunia kwa jina la Tanzania.
Hayo ni maneno ya Mwenyekiti wa DP World.
Sisi siyo bandari tu, sisi ni kituo cha UStawi wa Tanzania.
Mnaogola misikiti itakua mingi!?..Samia anajenga irrigation schemes nchi nzima, miundombinu ya afya,anaajiri,kaajiri walimu 30k,bandari mapato yataongezeka,huo u-worst wake ni upo!?..nyakati zimebadilikaSamia the worst president ever in the history of our country .