Uwanja wa Ndege Dar: Mapokezi ya Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu - Julai 27, 2020
Makosa yaleyale waliofanya mwanzo ndo yanajirudia kunakitu tunaita kutokuacha alama au ushahidi kwa lugha nyingine mfano Inshu ya J nassari kufukuzwa ubunge au la mbowe na ishu ya kuvunjika mguu usiku dodoma Sasa ndo hapa chadema wamefeli kuweka karata zao vizuri wanajua lisu anakesi mahakamani na wadhamini wake kila tarehe ya mahakamani wanaomba wajiondoe kumdhamini lisu sasa leo kaja ndo najiuliza hapa mahakamani haitatoa hati ya kumkamata lisu sababu anakesi mahakamani na wadhamini wake kila siku ya shauri uomba wajitoe kumdhamini?
Kumkamata Lissu kwa kosa lenye dhamana hakuna shida kabisa, muhimu apewe dhamana.
 
Makosa yaleyale waliofanya mwanzo ndo yanajirudia kunakitu tunaita kutokuacha alama au ushahidi kwa lugha nyingine mfano Inshu ya J nassari kufukuzwa ubunge au la mbowe na ishu ya kuvunjika mguu usiku dodoma Sasa ndo hapa chadema wamefeli kuweka karata zao vizuri wanajua lisu anakesi mahakamani na wadhamini wake kila tarehe ya mahakamani wanaomba wajiondoe kumdhamini lisu sasa leo kaja ndo najiuliza hapa mahakamani haitatoa hati ya kumkamata lisu sababu anakesi mahakamani na wadhamini wake kila siku ya shauri uomba wajitoe kumdhamini?
Ukute umeishia darasa la nne unajifanya unaijua sheria kuliko tundu lissu mwenyewe ambae amewahi kuwa raisi wa TANZANIA LAW SOCIETY (TLS )
 
Makosa yaleyale waliofanya mwanzo ndo yanajirudia kunakitu tunaita kutokuacha alama au ushahidi kwa lugha nyingine mfano Inshu ya J nassari kufukuzwa ubunge au la mbowe na ishu ya kuvunjika mguu usiku dodoma Sasa ndo hapa chadema wamefeli kuweka karata zao vizuri wanajua lisu anakesi mahakamani na wadhamini wake kila tarehe ya mahakamani wanaomba wajiondoe kumdhamini lisu sasa leo kaja ndo najiuliza hapa mahakamani haitatoa hati ya kumkamata lisu sababu anakesi mahakamani na wadhamini wake kila siku ya shauri uomba wajitoe kumdhamini?
Wewe tulia watu wamesha calculate hayo yote ndo mana anatua Tz
 
Usiulize majibu
Tupia picha tuone, lasivyo utakua unajitekenya kisha unacheka mwenyewe.
tapatalk_1595847570716.jpeg
 
Salaam Wakuu,

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tanzania Bara Tundu Lissu anatarajiwa kuwasili nchini leo saa saba na dakika ishirini saa za afrika Mashariki.

Lissu amekaa nje ya nchi miaka mitatu sasa baada ya kuondoka kwa shambulio la risasi lililotokea mjini Dodoma ,Septemba 7, mwaka 2017, saa 7 mchana, Area ‘D’, kwenye nyumba ya makazi ya viongozi wa Serikali mjini Dodoma.
Mkuu
“Lissu kwa sasa anatimiza mwaka wa tatu na anarejea hapa nchini baada ya kupona kikamilifu. Watanzania na wanachama wa Chadema wanakutana hapa uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA), kwa lengo la kumpokea makamu mwenyekiti wa chama chao Lissu.

Hivyo timu nzima tupo hapa kukuletea kile kitakachojiri kwenye mapokezi haya.

Stay tuned.

======

UPDATE (NOTE: Picha zipo post ya 2):



1105HRS: Hapa uwanjani pametulia, hakuna fujo wala dalili za fujo, Wanachama wachache wa CHADEMA wanaonekana wakipita pita huku na kule. Bado sijabahatika kuona gari la Polisi Wala Gari la CHADEMA.


Ratiba inaonesha muda wa ndege kufika ni saa saba na dakika Ishirini. Angalia kwenye chati

1121hrs: Saa moja iliyoisha Tundu Lissu ndo amepanda ndege ya Ethiopian Airlines ET 805 kutoka Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Bole Addis Ababa kuja hapa Dar Julius Kambarage Nyerere International Airport.

Safari inatazamiwa kuchukua masaa yasiyozidi Matatu kufika hapa tulipo.

1140hrs: Mwenyekiti Mkoa wa Iringa CHADEMA William Mungai, aliyekuwa Mbunge wa Tarime Vijijini John Heche na aliyekuwa Mbunge wa Mbeya Joseph Mbilinyi(Sugu) Wakiwa Wamefika hapa Uwanja wa ndege kumpokea Lissu

1156HRS: Kutoka kushoto: Hekima Mwasipu, Wakili wa Chadema, Sugu, Catherine Ruge(Simba Jike) Viti Maalum Mara na Mgombea wa Jimbo la Segerea CHADEMA

1230hrs: Polisi Magari Mawili ya Polisi wameshusha Wanausalama wa kulinda amani wapatao kama 30 nje ya Viunga vya Uwanja wa ndege. Wamekaa mstari kama Gwaride na wanapewa Maelekezo. Wameshusha njia Panda ya kuelekea Uwanja wandege. Kuna askari wanne walikuwepo tangu asubuhi Wakihoji kila anaye ingia.

Bodaboda kama 50 wapo hapo Askari Polisi Walipo, nadhani Wamekataliwa kuingia. Vilevile Magari ya CHADEMA maarufu kama Magari ya M4C, Yapo sehemu hiyo ya njiapanda yakizunguka huku na kule. Magari ya CHADEMA yapo Matano yamejaa watu waliovalia nguo za CHADEMA.

Polisi ukijielezea unapoelekea ndo Wanaruhusu. Lalikini kuna baadhi ya Wafanyakazi(Walinzi wa Uwanja, sio Polisi) ndo wanakataza watu kuingia.

1240: Baadhi ya Wanachama wa CHADEMA wameweza kupenya na kuongia ndani sehemu ya kusubiria Wageni

1300hrs: Baadhi ya Wanachama wa CHADEMA wameruhusiwa kuingia. Wengine wapo nje ya Uwanja wanaimba nyimbo.

Polisi Tanzania Wamewaruhusu Wanachama wote wa CHADEMA na Wafuasi wa Tundu Lissu. Muda wowote ndege itawasili

1357hrs: Abiria wameanza kutoka nje. Lissu bado hajaonekana

Mkuu nipo hapo arrivals mbona sikuoni
 
Back
Top Bottom