Waziri Mkuu: Bandari imepewa DP-World kwa kuwa utendaji wa TICTS ni mdogo
Ila hii nchi ina mambo ya ajabu!! Mtu mmempa mkataba wa miaka 20 akavurunda vibaya bado mnamuongezea wa miaka mitano!!!! No wonder huu mkataba mwingine umekaa ndivyo sivyo[emoji134][emoji134][emoji134]
TICS walikua watanzania wenzetu wapigaji wanawaza wizi tu ngoja tuwalete watu ambao wapo serious na kazi.
 
Maswali yote uliyouliza yana jibu moja tu ni kwamba DP WORLD anakidhi sifa miongoni mwa makampuni yote katika uendeshaji wa bandari.
Siyo kweli hata kidogo.
Unataka kuniambia kwamba bandari zote zilizopo hapa duniani ambazo zinafanya vizuri zinaendeshwa au kusimamiwa na kampuni ya DPW??
Kama ukweli ndio huo, Je, ni kwa nini Serikali isiwatume watu (Watanzania) kwenda kujifunza au kusomea namna bora ya kuendesha au kusimamua bandari katika kampuni hiyo ya DPW???
 
uyu ndo aliesema jpm ni mzima wa afya na anaendelea na majukumu yake tena alikua kuwa msikitini 😁😅😁
 
Wafanyabiashara wanakimbia shauri ya kodi kubwa, Mbona Hilo hawalishughulikii?

Hayo mengine danganya toto tu.
 
Waziri Mkuu, Kassimu Majaliwa amesema utendaji mbovu wa bandari unasababisha meli zitumie muda mwingi bandarini ambapo gharama ya meli kubaki bandarini huingia mfanya biashara hivyo bidhaa kuwa ghali mtaani. Amesema kwa sasa meli hutumia hadi siku saba kwa mzigo kupakuliwa.
Kwanini serikali isiwekeze yenyewe mitambo mikubwa ya kufanya kazi hiyo?
  1. Fikiria idadi ya magari ya kifahari yanayonunuliwa kwaajili ya viongozi
  2. Fikiria wingi wa wabunge butu wanaolipwa trillions for nothing
  3. Fikiria kodi wanazokwepa wafanyabiashara wakubwa
Vyote hivyo na vingine vingi vingefanyiwa saving huenda fedha ingetosha kuwekeza kwenye bandari na mapato yakawa 100% owned na serikali
 
2.Katika miaka yote hii ya Uhuru, Je, Serikali yenyewe imefanya juhudi gani za makusudi katika kuwawezesha Watanzania wazawa ili waweze kuendesha Bandari hiyo?? Kwa nini haikuunda Kampuni yake yenyewe ambayo ni strong and competent katika kufanya shughuli za Badari??
Ambayo mwisho wa siku ingekwenda kuwekeza kwenye nchi nyingine kama hao Dubai wanavyotaka kuja kufanya hapa
 
Hajajibu hoja zinazotiliwa shaka na wananchi.

Kwa ni wamepewa mkaba usio na Kikomo

Kwa nini wamepewa Bandari zoote, Anga, Reli na Barabara milele na milele.

Waziri Mkuu na yeye ni kama hajui kama sisi tu.
Uvivu wao na uwezo wao mdogo wa kufikiri na kutazama mbali ndiyo umetufikisha tulipo, they are really ceremonial leaders who never think of our future generations, wao wanaishi hand to mouth
 
1. Je, kuwapa hao DPW ndio suluhisho la kudumu la tatizo hilo??
2.Katika miaka yote hii ya Uhuru, Je, Serikali yenyewe imefanya juhudi gani za makusudi katika kuwawezesha Watanzania wazawa ili waweze kuendesha Bandari hiyo?? Kwa nini haikuunda Kampuni yake yenyewe ambayo ni strong and competent katika kufanya shughuli za Badari??
3. Je, kuuza au kubinafsisha wa wageni kila taasisi ya Serikali iliyoshindwa kujiendesha ndio suluhisho sahihi l a matatizo yetu??
4. Je, kampuni ya kitanzania yenye uwezo wa kufanya kazi za bandari ni TICTS tu peke yake??Zingine mbadala hakuna hadi wapewe DPW??
5. Kama utendaji usioridhisha wa Kampuni ya TICTS ndio kigezo kilichosababisha bandari kuuzwa kwa wageni, mbona kuna taasisi nyingi hapa nchini ( taasisi binafsi na taasisi za Serikali) ikiwamo na Ofisi yake ya Waziri Mkuu na Ikulu ya Rais pia, taasisi ambazo nazo utendaji wake si wa kuridhisha.Je, taasisi hizo (Ikulu na OWM nazo sasa tunatakiwa tuzibinafsishe kwa raia wa kigeni eti kisa zina utendaji usioridhisha???? Ndio anataka kutuambia hivi Watanzania??
6.Je, TPA itakuwa na Jukumu gani basi baada ya bandari zote kubinafsishwa hapa Tz???
7.Ni kwa nini Serikali isifikirie kuivunja Mamlaka ya Bandari (TPA), kuivunja TASAC pamoja na taasisi zingine zote zinazohusika na masuala ya Bandari hapa nchini ili kuunda kampuni moja kubwa itakayoshirikiana au kuingia ubia na taasisi binafsi za ndani ya nchi kama vile TICTS ili kufanya kazi za bandari kwa ufanisi zaidi badala ya kufikiria kubinafsisha bandari zote kwa kampuni ya kigeni ya DPW kwa Mkataba wa maisha/milele????????????

Ticts ndio imefanya kazi miaka yote alaf bdo tuwape hao hao tena [emoji853]ww ni mfanyakazi wa ticts xx imetosha utendaji wenu acha wengine wapige kazi
 
S

Sipingi DPW, ila huyu Waziri Mkuu anasema bidhaa zimekuwa ghari mtaani kwa sababu ya Customs na TRA au ushushaji mizigo polepole yaani procedure za TICS, huyu DPW atatatua hayo matatizo kwa technologia gani? Yaani meli zisushe mizigo haraka, zipunguze muda wa kungoja?
Maana yake , yeye kama waziri mkuu na mtendanji wa serikali- HATOSHI- kama utendaji kazi mdogo, kwa ni nini wasiongeze ufanisi kwa sisi wenyewe. kama utendaji kazi mdogo, chanzoi ne yeye. Longo longo tupu na kuzunguka mbuyu.
 
S

Sipingi DPW, ila huyu Waziri Mkuu anasema bidhaa zimekuwa ghari mtaani kwa sababu ya Customs na TRA au ushushaji mizigo polepole yaani procedure za TICS, huyu DPW atatatua hayo matatizo kwa technologia gani? Yaani meli zisushe mizigo haraka, zipunguze muda wa kungoja?

Tatizo hio ticts haina vifaa bora ndio maana ushushaji wa kimagumashi ila hao dp wanakuja wanaleta vifaa vipya na vya kisasa zaid.
 
Maana yake , yeye kama waziri mkuu na mtendanji wa serikali- HATOSHI- kama utendaji kazi mdogo, kwa ni nini wasiongeze ufanisi kwa sisi wenyewe. kama utendaji kazi mdogo, chanzoi ne yeye. Longo longo tupu na kuzunguka mbuyu.

Acha siasa mkuu miaka yote hakuna kitu hapo tukomae na kipengele cha muda tuh vingine ni fresh
 
Uzuri wake tumebakiza mwaka 1 kuingia kwenye Uchaguzi ujao hapo 2025.

Na kwa taarifa za ndani ile nguvu ya Ukawa ya 2015 itakuwa mara mbili zaidi maana ushawishi wa Chama Tawala upande wa Kanda ya ziwa umeshuka zaidi baada ya kifo cha JPM
Hiyo katiba manayo? Au bado mnategemea mkurugenzi atangaze matokeo ya jimbo na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi taifa atangaze matokeo ?
 
Hiyo katiba manayo? Au bado mnategemea mkurugenzi atangaze matokeo ya jimbo na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi taifa atangaze matokeo ?
Wakurugenzi wamepigwa marufuku kusimamia Chaguzi.

Hivyo nafasi ya Msimamizi wa Uchaguzi itakuwa ikitangazwa na wenye sifa watatikiwa kuomba.

Hopefully hii itaweza kusaidia
 
Back
Top Bottom