Kwa matokeo ya Mwibara, unapaswa ujitathimini; je, yale yote ufanyayo kudhalilisha watu na kuwatukana ukijifanya unamtetea Rais (bila kutumwa) na unaitetea CCM, je yanathaminiwa au unaonekana kituko tu?

Haiwezekani kwa juhudi zile zote lakini wanaCCM wenzako takribani 400 wakupatie kura sifuri, hata moja ya kudanganyia hakuna?

Hii ni dalili juhudi zile zote unaonekana mjinga tuu na bado kidogo wakuchoke.

AIBU KUBWA
 
Habibu Mchange Kibaha mjini kura 69 no 4 au 5 kama sikosei. Sylvester Koka ametetea kiti
 
Kuna kitu cha kujifunza hapo, yaani mtu anayemtetea mwenyekiti wao members wenzake wasimpe hata kura moja? ina maana members wanamchukia sana mwenyekiti pia ni vile tu hawajapata fursa ya kumchinjia mwenyekiti wao baharini kama hiyo waliyopata kumnyoosha Musiba!

If A=B and B=C it means A=C!!

Watu au Mungu au Shetani mmojawapo anamtaka Musiba akae hapo alipo na afanye kazi anayoifanya hiyo hiyo hawezi kutoka now mpaka akamilishe purpose! akitoka tutakosa fursa za udukuzi wa mazungumzo ya cm ya Kinana na Nape na Januari wakimwita Rais mshamba tu wa huko Mali Mali!!
 
Umemsahau na Lijualikali na Cecil Mwambe wote wameangukia pua zao chaaliiii
Yule dogo wa kigoma Elia aliyeunga juhudi toka chadema kachezea nae.
Siasa ni upepo na sio hesabu walitegemea kubebwa na mwenyekiti
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…