Kigoma Mijini waislam ni wengi kwa maana hiyo wao ndiyo waamuzi wa nani awe mbunge.

Ni Kama Zanzibar. Pale Mkristo akigombea hawezi kushinda.

Kwa hiyo usitoe povu sana wakati mwenzako kasema ukweli
Kwahiyo dini yenye wafuasi wengi ndio inaamua nani ashinde?

Mbona unatumia hoja dhaifu sana mkuu.

Hizi hoja za Ponda zinawaharibu sana ufahamu wenu
 
Huyu hata mke wake anamuona mjinga tu,nilikula nae break fast siku moja sehemu fulani alikuwa mbele yangu na watu Kama wawili wengine wakati tunanawa mikono,kabastola kake kakawa kamechomoza kiunoni upande wa kulia akaambiwa na mtu alie karibu nae,akamjibu " Bora waione wajue nimekamilika kwa mapambano" kila mtu mle restaurant alibaki mdomo wazi wakimshangaa
 
Hili ni funzo kwa wagombea wote wa CCM ambao wanatarajia kuwaambia wapiga kura kuhusu mambo makubwa yakiyofanywa na Serikali bila kuzingatia hali halisi ya maisha ya mpiga kura ya kila siku.
 
kuna kitu cha kujifunza hapo, yaani mtu anayemtetea mwenyekiti members wenzake wasimpe hata kura moja? ina maana members wanamchukia mwenyekiti?
Hili ni swali gumu... au wanawachukia wanaojipendekeza kwa Mwenyekiti? Au wanawachukia "waliojituma" kwa jina la Mwenyekiti?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…