Uchaguzi 2020 Yaliyojiri upigaji kura za maoni za wagombea wa Ubunge na ujumbe wa Baraza la Wawakilishi kupitia CCM - Julai 20-21, 2020
Yule ni mwanae sana tena saana,sidhani kama atamuacha hivi hivi tu mikono mitupu.
Sawa kiongozi nimekuelewa sana kwamba Mnyeti mtu wa familia ila Kitwanga kwa kuwa ni rafiki wa Jiwe na kwamba Ubunge ameukosa imani yangu ni kwamba baada ya uchaguzi wa 2020 atapewa uteuzi wowote ule hatamwacha hivi huvi
 
CCM imetengeneza 1,036,100,000 kupitia ada za fomu za ubunge na uwakilishi. kweli mwenye nacho huongezewa.
bado nasikia kuna michango mbalimbali isiyo rasmi wanatakiwa kulipia mbali na hiyo ada
Natumai panapimajaliwa mwaka 2025 hii ada lazima ipande..hata mwaka huu ingepanda sema hawajashtukia mchezo mapema kama watu watakua wengi kiasi hiki
 
Kama watanzania wa vyama vyote tungekuwa na Nia njema ya kuleta maendeleo ya nchi yetu Hawa wabunge ambao wamekaa bungeni zaidi ya miaka kumi tungewakataa katika uchaguzi huu. Haiwezekani mtu anakuwa Mbunge Hadi miaka ishirini na bado tu anautaka ubunge Tena utadhani Jimbo Hilo ni yeye tu mwenye sifa za kuwa mbunge.

Hii ingesaidia watu na hawa viongozi kutambua umuhimu wa katiba mpya na kuacha mawazo ya kudhani kuwa wao ni raia wa faraja la juu kuliko wengine, kwanza Hawa wabunge wa aina hii hawana jipya zaidi ya kujipendekeza na kupiga majungu kwa wenye mamlaka tu.

Wanayo majina yao eti maseneta wapishe wengine hao hata Kama watapishwa na upinzani wasichaguliwe, wakipitishwa na CCM wananchi tusiwachague.
 
Dr Kigwangalla anaomba dua zetu aweze kushinda!

Anaomba dua zetu huku anatutukana??

Si yeye mwenyewe ndo alikua anajifanya kutufundisha kujiajiri eti nje ya box😄😄
DA747316-C469-4FB9-80E4-1E0A6894EB4D.jpeg
 
Haya kumeshakucha tena La mgambo likilia ujue kuna jambo.


Kwa mujibu wa ratiba ya CCM, leo na kesho ni siku ya Mikutano Mikuu ya CCM ya Majimbo/Wilaya kupiga kura za maoni za wagombea wa ubunge na ujumbe wa baraza la wawakilishi

Kwa Mujibu wa Mwenyekiti wa CCM, Dkt. Magufuli waliochukua kugombea nafasi za Ubunge na uwakilishi ni 10,367. Waliokamilisha kujaza fomu na kurejesha ni 10,321.

Watanzania wataelekeza zaidi macho na masikio yao maeneo yenye upinzani mkali kama Kigamboni, Arusha mjini, Simanjiro, Kyela, Mbeya mjini, Mwibara, Misungwi, Same Mashariki, Tunduma, Tarime Vijijini na Ubungo ni baadhi ya maeneo yanayoangaliwa kwa jicho la tatu.

Ngoja tuone.

Up dates:

Jimbo la kinondoni jumla ya waliochukuwa fomu ni 81 na waliorejesha ni 79 ambao wanaendelea kujieleza .

Jimbo la Ubungo waliochukuwa fomu ni 113 na waliorejesha ni 111 na wanaendelea kujieleza, Mbarouk Masoud ambaye ni Katibu mwenezi anasema zege halilali.

Maendeleo hayana vyama!
Uwe unapandisha matokeo juu ,nimeona Jimbo la mwigulu tayari matokeo lakini kwenye update hakuna...Hatuna muda wa kusoma comments zote unless tagged.
 
Back
Top Bottom