acha wivu wa kikuda mkuu, hii simba sio yako wala ya babu yako, shabiki yoyote anaweza kuitumia kujitengenezea jina na hata kigonga madili wewe inakuuma nini kama sio chuki hizi
Duh we mwepesi kweli, unaelewa hapa kuna conflict of interest?

Hivi unafikiri media officer wa Man United angeruhusiwa na Glazers kuwa ambassador wa Abu Dhabi United Group na bidhaa zake?

Watu watahoji loyalty na commitment yako kwa klabu unayoitumikia.
 
Niguse ninuke
 
Wewe ni nani ndani ya Simba mpaka umpe masharti hayo mwenzako, ukute wewe ni chawa tu wa Barbara Gonzalez

Sent from my Infinix X683 using JamiiForums mobile app
 
Uzi bora kabisa wa kunywea na Wine wkend hii. Haji anadeka sana. Akiparuriwa kidogo tu huyooo Insta. Hatuwezi kuishi hivyo. Simba kama taasisi haiwezi kuwa imenyooka kama malaika wa mbinguni lazima kuwe na migongano ya hapa na pale. Mwanaume lazima usimame imara kukabili,sio unalia lia tu kama demu
 
Naunga mkono kila kitu hadi nukta.
 
Amepewa option ya kuchagua eidha awe mwakilishi wa Simba SC au Asas, GSM na Azam Ltd? Simple as that.

Hata mimi binafsi nilikuwa sipendezwi jinsi alivyotumia brand ya Simba kutengeneza brand yake ili kupata endorsements kama za Asas, GSM na Azam
Ila akiondoka Simba mjiandae kuoga shombo lake. Huyu jamaa kwa shombo hafai.
 
Unasema Manara hana adabu kwa CEO wake wakati huohuo na wewe unaonyesha utovu wa nidhamu kwa "kuipangia" SIMBA SC nini ifanye. Hiyo idea ya "kumuweka pembeni kwa siku 7" umeitoa wapi na ni kwa mujibu wa sheria ipi ya kazi ya SSC?
 
Si keshajitoa mwenyewe? Atuachie simba yetu!
 
Samahani Mkuu mimi bado sijaelewa MO ni Mmiliki au Mdhamini wa Simba SC?
 
Unasema Manara hana adabu kwa CEO wake wakati huohuo na wewe unaonyesha utovu wa nidhamu kwa "kuipangia" SIMBA SC nini ifanye. Hiyo idea ya "kumuweka pembeni kwa siku 7" umeitoa wapi na ni kwa mujibu wa sheria ipi ya kazi ya SSC?
Manara hana mkataba hivyo sheria za kazi hazitumiki hapo..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…