Hans Pope: Manara hataki kusaini mkataba ambao atalipwa milioni 4
Unasema Manara hana adabu kwa CEO wake wakati huohuo na wewe unaonyesha utovu wa nidhamu kwa "kuipangia" SIMBA SC nini ifanye. Hiyo idea ya "kumuweka pembeni kwa siku 7" umeitoa wapi na ni kwa mujibu wa sheria ipi ya kazi ya SSC?
Ametoa ushauri labda wewe utuambie ametenda kosa gani kutoa ushauri?

Manara ni disgrace kwa Simba
 
Iwe ni Mind game au iwe ni uhalisia, mimi nazungumza kama mdau wa michezo.

- Ukimsikiliza Haji kwenye audio inayozunguka mitandaoni, Moja ya malalamiko yake ni kwamba anashutumiwa kuihujumu Simba kutokana na ukaribu uliopo baina yake na uongozi wa GSM.

- Kama hoja ni hiyo, sioni kosa la Babra kumuita Manara na kumuuliza.
Leo hii wanayanga wanamshutumu mwenyekiti wa klabu ya Yanga kisa anafanya Kazi kwa Mohamed Dewji.

- Lakini pia kuelekea kwenye hizi mechi za watani wa jadi, kiongozi wa timu fulani kuwa karibu na viongozi au wadhamini wa timu nyingine, kiuhalisia inaondoa uaminifu KWA mashabiki na wanachama.

- Tukumbuke kuwa Haji huyu huyu aliwahi kumshutumu aliyewahi kuwa kocha wa Yanga Mwinyi Zahera kisa kukutana na Ibenge aliyekuwa kocha wa AS Vital KWA kile alichokisema anataka kuihujumu Simba. Alikwenda mbali mpaka akasema kuwa kama Simba itafungwa basi Zahera atakiona.

Alisahau kuwa Zahera alikuwa kocha msaidizi wa Ibenge kwenye majukumu ya National team.

- Hakuishia hapo Haji. Bado alikuja kumshutumu Senzo, kisa kukutana na kocha wa Al Ahly ya misri, KWA kile alichodai Senzo anataka kuihujumu Simba.

Alifikia hatua ya kumtisha Senzo mpaka juu ya uraia wake.

- Sasa ajabu ni nini yeye kushutumiwa juu ya hujuma za kuihujumu Simba?

- Ukichunguza Sana unagundua kuwa huu Ujinga waliufuga Simba wenyewe. Mashabiki na wanachama wa klabu ya Simba walimwamini Haji mpaka wakashindwa kumtofautisha Haji Manara na Afisa Habari wa Simba.

- Mashabiki na wanachama hawa ilifikia hatua hata ishu personal za Haji walizibeba kama ishu za Simba sc.

Na hapa ndipo Haji alipoanza kuota mapembe na kujiona yeye yupo sahihi kwa kila atakachokizungumza. Alijiona kuwa neno lake laweza kuwa sheria.

Haji alikuwa anaweza kuanzisha vita ya maneno na mtu, anapoona anakosa hoja anarudi kwa mashabiki na wanachama wa Simba kwa kisingizio cha kuitetea Simba. Na mashabiki nao bila kufikiri wanaingia mkumbo huo huo na kuwatukana watu hovyo.

Leo hii baada ya kuwachafua waliopo nnje ya Simba sasa anawachafua waliopo ndani ya Simba.

Akimaliza na Bara anakuja na Mo, na hapo ndipo mtakapokuja kujua ule msemo wa "MTOTO UMLEAVYO NDIVYO AKUAVYO" AND "WHAT GO AROUND, COMES AROUND"
 
Alichonikera ni kwenda kwenye mitandao ya kijamii yakati sisi mashabiki wala hatujui kama kuna ugomvi kati yake na bosi zake. Kwa ukweli hakukua na haja angemalizana huko huko tu. Nadhani timu ya simba inawafundisha ethics wachezaji tu bila ya kuwafundisha na hawa watendaje. Alichokifanya sio sahihi wala hakifuati misingi ya kisheria za kazi kwakweli. Sio mtu mzuri wa kufanya nae kazi au biashara ya aina yoyote kwakweli. Nna wasi wasi hata kuna siku atagombana na mkewe halafu aje huku mitandaoni kulalamika. Hata akiomba msamaha atafutiwe kazi nyengine ndogo ndogo afanye, zisizohusu moja kwa moja masuala ya uomgozi, amefeli sana
 
Mimi unachonishangaza unalalamika umeitumikia simba, kwani unapoitumikia simba faida kwako au kwetu. Sisi mashabiki tunaingia viwanjani na tunalipa kadi za chama kwa pesa zetu wala hatufaidiki na chochote zaidi ya furaha. Wewe simba inakulipa, sasa nani anaitumikia simba ni sisi au wewe. Haji aache upuuzi bhana, atolewe haraka ni kirusi mbaya sana
 
Manara hawezi kufanya kitu chochote kile kitachoiathiri Simba SC technically.
Yaani azisome mbinu za Gomez halafu akamwambie Nabi?
Au awaambie Yanga Simba wanapanga kuwachezesha kina nani? Formation gani? Au wanakula chakula gani?
Au atawaambia yanga nini kitakachowafanya Simba wapoteze mechi?
Acheni mambo yenu ya kienyeji. Endesheni timu professionally.
 
Umeandika vizuri sana mkuu, ila nawe ni mnifiki tu kama huyo Haji umsemaye.. Mbona Siku zote hukuja kusema hapa,, wewe ni CCM kama Manara na kama Mimi tu,, Basi kama CCM ni ya Wanafiki, Sisi wote ni wanafiki.
We unadhan ungekuwa Manara unalipwa 700k kwa club kama simba ungeshindwa kuihujumu hali ya kuwa GSM unapiga nao dili dogo tu unakula millions 5.
 
Mimi unachonishangaza unalalamika umeitumikia simba, kwani unapoitumikia simba faida kwako au kwetu. Sisi mashabiki tunaingia viwanjani na tunalipa kadi za chama kwa pesa zetu wala hatufaidiki na chochote zaidi ya furaha. Wewe simba inakulipa, sasa nani anaitumikia simba ni sisi au wewe. Haji aache upuuzi bhana, atolewe haraka ni kirusi mbaya sana
Simba imejaza uwanja wa taifa toka wnzi za mtani jembe na hakukua na hamasa ya manara leo anatokeza mtu anasema manara ndio sababu ya kujaza uwanja...
Tunamshukuru kwa mchango wake ila muda wake wa kuondoka umefika..
 
Manara hawezi kufanya kitu chochote kile kitachoiathiri Simba SC technically.
Yaani azisome mbinu za Gomez halafu akamwambie Nabi?
Au awaambie Yanga Simba wanapanga kuwachezesha kina nani? Formation gani? Au wanakula chakula gani?
Au atawaambia yanga nini kitakachowafanya Simba wapoteze mechi?
Acheni mambo yenu ya kienyeji. Endesheni timu professionally.
Hata kama hana madhara technically, bado huo ni uhaini. Haipo ktk maadili ya kazi.
 
Kwa muda mrefu Haji amekuwa akijihusisha na GSM kama one of the brand ambassador na pia amekuwa brand ambassador wa wafadhili wa azam. Tatizo ni kwamba kuwa ambassador huko kwingine kunamnyima yeye nafasi ya kutangaza bidhaa za mtu ambaye amewekeza pesa nyingi pale Simba kwa sababu za kimikataba na hao wengine.

Sasa haiingii akilini, muajiriwa wasimba anashindwa kutangaza bidhaa za mdhamini wa Simba, ila anaenda kutangaza bidhaa za madhamini wa Yanga!

Hivi ishawahi kufikiria leo Hasan bumbuli awe na mkataba wa kibiashara na Mo dewji kutangaza bidhaa zake na mashabiki wa yanga wamuangalie tu?

Linapokuja swala la mshahara, Simba wanampa laki Saba huku hao wengine wanampa wakimpa zaidi ya million 5 Sasa unafikiri huyo anayempa million 5 akija kumuomba taarifa za huyu anayetoa laki 7 atakataa?? Ni halali viongozi wa Simba kuwa na mashaka na haji manara.
 
Haji Manara ameonesha utovu wa nidhamu wa hali ya juu! Anamwambia CEO akome!! Kwenye taasisi yoyote CEO ndo kila kitu! Unamtukana CEO hadharani unategemea nini?

Manara ameifedhehesha sana simba!! Hata kama CEO akiwa na makosa hiyo siyo namna ya kushughulika naye. Siwezi kushangaa kama Manara akimtukana baba yake! Hana adabu!! Ni aibu kwa baba yake pia!

Nashauri awekwe pembeni kwa siku 7 apate muda wa kutafakari! Asiambatane na timu kigoma!! Baada ya siku saba 7, amwombe radhi Barbara hadharani.

Kisha kama ana malalamiko yoyote ayawasilishe kwa uongozi. Akishi dwa hilo aende zake!! Mchango wa,e kwa simba tunautambua lakini ameamua kunyea kambi!
Hajji inabidi akamatwe na kutiwa ndani kwa kumtishia CEO (Boss wake), afungwe hata mwaka tu na akitoka afungiwe na TFF kutojihusisha na mpira hapa Tanzania.
 
Alichonikera ni kwenda kwenye mitandao ya kijamii yakati sisi mashabiki wala hatujui kama kuna ugomvi kati yake na bosi zake. Kwa ukweli hakukua na haja angemalizana huko huko tu. Nadhani timu ya simba inawafundisha ethics wachezaji tu bila ya kuwafundisha na hawa watendaje. Alichokifanya sio sahihi wala hakifuati misingi ya kisheria za kazi kwakweli. Sio mtu mzuri wa kufanya nae kazi au biashara ya aina yoyote kwakweli. Nna wasi wasi hata kuna siku atagombana na mkewe halafu aje huku mitandaoni kulalamika. Hata akiomba msamaha atafutiwe kazi nyengine ndogo ndogo afanye, zisizohusu moja kwa moja masuala ya uomgozi, amefeli sana
Aliisha leta mtandaoni baada ya kukosana na mke wa kwanza.
 
Simba imejaza uwanja wa taifa toka wnzi za mtani jembe na hakukua na hamasa ya manara leo anatokeza mtu anasema manara ndio sababu ya kujaza uwanja...
Tunamshukuru kwa mchango wake ila muda wake wa kuondoka umefika..
Kabisa.
Hanspope kamjibu vizuri sana.
 
Ametoa ushauri labda wewe utuambie ametenda kosa gani kutoa ushauri?

Manara ni disgrace kwa Simba
Anafanya "kosa" lilelile kama la Manara. 🙂

Manara sio disgrace. Ametoa frustrations zake tu. Kumbe mtu analipwa ujira wa kibarua wa 700K, hana Mkataba (no bima ya afya, no NSSF) na yupo tagged kama mfungwa ambaye movements zake zipo monitored. Kama Manara anafanyiwa hivi, how about walinzi, wapishi na cleaners??

Akina Barbara ndio disgrace kwa Simba
 
Back
Top Bottom