MITHALI 22:6
Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.
Maombolezo 5:7
Baba zetu walitenda dhambi hata hawako; Na sisi tumeyachukua maovu yao.
MITHALI 10:1
Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye; Bali mwana mpumbavu ni mzigo wa mamaye.
ISAYA 54:12-13
Nami nitaifanya minara yako ya akiki nyekundu, na malango yako ya almasi, na mipaka yako yote ya mawe yapendezayo.
Na watoto wako wote watafundishwa na Bwana; na amani ya watoto wako itakuwa nyingi.
YEREMIA 22: 29-30
Ee nchi, nchi, nchi, lisikie neno la Bwana.
Bwana asema hivi, Andikeni habari za mtu huyu kwamba hana watoto, kwamba mtu huyu hatafanikiwa siku zake zote; maana hapana mtu katika wazao wake atakayefanikiwa, akiketi katika kiti cha enzi cha Daudi, na kutawala tena katika Yuda.