Manyara UPDATE: Waliofariki kwa Mafuriko Wilayani Hanang wafikia 80 na Majeruhii 133
Vifo vilivyotokana na maafa yaliyotokea wilayani Hanang, mkoani Manyara, na kusababisha uharibifu mkubwa ikiwemo baadhi ya nyumba na mali, vimeongezeka na kufikia 47 na majeruhi 85.

Tuzidi kuwaimbea ndugu zetu hali ni mbaya niliona video mchana hali inatisha nikiipata nitawetea hapa
 
Ule mlima kuna kitu watu hawakijui vizuri, iko hivi mlima hanang upo kama kilimanjaro una-crater kwa juu ambamo panamaji kwa miaka mingi hivyo ilipopiga mvua kubwa ngoma ilifurika nakusababisha mpasuko chinikwachini pressure ilipoongezeka nakusababisha landslide/mudflows
Au kuna Bwawa la Maji kama la Libya? Source ya Maji ya Bomba I mean.
 
MANYARA: Idadi ya Watu waliopoteza maisha kutokana na Mafuriko yaliyosababishwa na Mvua zilizonyesha kuanzia Desemba 2 huko Hananga imefikia 47 na Majeruhi 85

Taarifa zaidi zimeeleza kuwa Mvua hizo zimeathiri Miundombinu ikiwemo kuvunja baadhi ya Nyumba, kukata Mawasiliano ya Barabara na Umeme.

============

===========

Watu watano wamefariki dunia na wengine 12 wamejeruhiwa wilayani Hanang mkoani Manyara baada ya mvua iliyonyesha usiku wa Desemba 2, 2023 kusababisha mafuriko.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga akizungumza na Mwananchi Digital leo Jumapili Desemba 3, 2023 amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo na madhara katika mali za watu.

Fuatilia mitandao ya kijamii ya Mwananchi na tovuti kwa taarifa zaidi

--

UPDATE: WALIOFARIKI DUNIA WAFIKIA 17

Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Janeth Mayanja amesema Watu 17 wamefariki dunia katika Wilaya ya Hanang Mkoani Manyara kufuatia mafuriko yaliyoambatana na mawe makubwa na miti kuingia katika makazi ya Watu ambapo imepelekea nyumba kadhaa kuanguka.

“Leo asubuhi tumepata changamoto hapa Hanang toka jana usiku zilikuwa zikinyesha mvua za kawaida lakini maji yakawa yameporomoka kutoka Mlima Hanang yakiwa na mawe na miti kuja katika Mji wa Kateshi yakiwa na nguvu, ambapo mpaka sasa tumepata vifo vya Watu 17 pamoja na majeruhi ambapo maiti zimehifadhiwa katika Hospitali ya Tumaini lakini pia uharibifu wa miundombinu ya barabara kati ya Sindiga na Babati yamesimama kwa muda ila TANROADs na TARURA wapo hapa kuhakikisha mawasiliano yanarejea”

“Pia niwaombe Wananchi kuendelea kuwa watulivu wakati jitihada za uokoaji zikiendelea”

====

HANANG, Manyara: At least 20 people have been confirmed dead and several others missing following heavy rains that triggered flash floods in northeastern town of Hanang in Manyara region on Sunday.

Manyara Regional Commissioner, Queen Sendiga, confirmed the incident, saying 70 people have suffered minor and serious injuries. The leader described the incident as “fatality and a tragedy” in the region.

Sendiga said the rescue teams were swiftly deployed to the affected areas to provide support and aid in the search for the missing.
Ilaa taarifaa sio sahihi sisi uku tumeshuhudia watu said 100. wakifariki mnasema 17.
 
Watu walikebehi watalaamu humu ndani. Watu wanajua kuwa watalaamu ama watu kwenye vitengo vyao wanalala na kuamka ama kuota wanajiropokea tu Kama wanasiasa wanavyoongeaga Kama utongazavyo unaongea ahadi ambazo huwezi timiza
 
Poleni sana sana Kwa msiba huu mkubwa, so far ni 47 confirmed dead! Ila Kuna Mambo mengine yanaleta ukakasi!

FFU wako juu ya Paa wakilinda mafuriko Kwa bunduki na bullet proof jackets na virungu

IMG-20231203-WA0036.jpg
 
Poleni sana sana Kwa msiba huu mkubwa, so far ni 47 confirmed dead! Ila Kuna Mambo mengine yanaleta ukakasi!

FFU wako juu ya Paa wakilinda mafuriko Kwa bunduki na bullet proof jackets na virungu

View attachment 2832497
Vilevile, itakuwa sawa kabisa kusema hao Askari walio pichani wapo hapo kama Advance team ya Usalama wa Raisi.

Na sio kila kitu ni kuzodoana na kukashifiana tu.

Hatahivyo ni kawaida katika majanga yeyote yale duniani kuwepo askari wanaolinda maeneo na mali wakati waathirika wakiwa katika mkiki mkaka wa janga linalowasibu.

Poleni wafiwa na waathirika wote. Muumba awalinde na kuwapitisha nyakatinhii ngumu.
 
Vilevile, itakuwa sawa kabisa kusema hao Askari walio pichani wapo hapo kama Advance team ya Usalama wa Raisi.

Na sio kila kitu ni kuzodoana na kukashifiana tu.

Hatahivyo ni kawaida katika majanga yeyote yale duniani kuwepo askari wanaolinda maeneo na mali wakati waathirika wakiwa katika mkiki mkaka wa janga linalowasibu.
Maelezo safi sana. Reasoning ya wanajf inazidi kushuka kila uchwao.
 
Back
Top Bottom