MANYARA: Idadi ya Watu waliopoteza maisha kutokana na Mafuriko yaliyosababishwa na Mvua zilizonyesha kuanzia Desemba 2 huko Hananga imefikia 47 na Majeruhi 85
Taarifa zaidi zimeeleza kuwa Mvua hizo zimeathiri Miundombinu ikiwemo kuvunja baadhi ya Nyumba, kukata Mawasiliano ya Barabara na Umeme.
============
===========
Watu watano wamefariki dunia na wengine 12 wamejeruhiwa wilayani Hanang mkoani Manyara baada ya mvua iliyonyesha usiku wa Desemba 2, 2023 kusababisha mafuriko.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga akizungumza na Mwananchi Digital leo Jumapili Desemba 3, 2023 amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo na madhara katika mali za watu.
Fuatilia mitandao ya kijamii ya Mwananchi na tovuti kwa taarifa zaidi
--
UPDATE: WALIOFARIKI DUNIA WAFIKIA 17
Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Janeth Mayanja amesema Watu 17 wamefariki dunia katika Wilaya ya Hanang Mkoani Manyara kufuatia mafuriko yaliyoambatana na mawe makubwa na miti kuingia katika makazi ya Watu ambapo imepelekea nyumba kadhaa kuanguka.
“Leo asubuhi tumepata changamoto hapa Hanang toka jana usiku zilikuwa zikinyesha mvua za kawaida lakini maji yakawa yameporomoka kutoka Mlima Hanang yakiwa na mawe na miti kuja katika Mji wa Kateshi yakiwa na nguvu, ambapo mpaka sasa tumepata vifo vya Watu 17 pamoja na majeruhi ambapo maiti zimehifadhiwa katika Hospitali ya Tumaini lakini pia uharibifu wa miundombinu ya barabara kati ya Sindiga na Babati yamesimama kwa muda ila TANROADs na TARURA wapo hapa kuhakikisha mawasiliano yanarejea”
“Pia niwaombe Wananchi kuendelea kuwa watulivu wakati jitihada za uokoaji zikiendelea”
====
HANANG, Manyara: At least 20 people have been confirmed dead and several others missing following heavy rains that triggered flash floods in northeastern town of Hanang in Manyara region on Sunday.
Manyara Regional Commissioner, Queen Sendiga, confirmed the incident, saying 70 people have suffered minor and serious injuries. The leader described the incident as “fatality and a tragedy” in the region.
Sendiga said the rescue teams were swiftly deployed to the affected areas to provide support and aid in the search for the missing.