Mwigulu: Tumesikia malalamiko ya Watanzania kuhusu tozo za miamala na Rais ametoa maelekezo ya kuzitazama upya
Ukitaka maendeleo ni Kodi. Kwenye hili hakuna mbadala wake.

Bila kufanya hivi Hawa machinga ambao ndio wanamiliki uchumi siku hizi na Kodi hawalipi unategemea utawapata wapi
 
Yaani huduma za mobile money zilikuwa zimekaa poa sana hadi pale serekali imeamua kuharibu kila kitu kama kawaida. Tamaa, Mimi nadhani wabunge hawa wakatwe kodi maana wanaenjoy wakaati sisi maskini tunapigika. Inshort tunafanya kazi kwa nguvu kulish familia na viongozi wa serekali.
 
Kwa nini miamala ya bank hakuna tozo na ukaamua kung'ang'ana na miamala ya walala hoi watu wa chini kabisa ,je wenye akaunti banki sio watanzania ,onyesha hekima na siyo kiburi kwa kufuta hilo hata kama sheria imepitisha uliwauliza wananchi
 
Mwanasiasa yeyeto ambae mtoto wake wa primary analipa ada milioni 10 na apandi daladala Katu hawezi panga bajeti rafiki kulingana na maisha ya mtza
 
Mhe. Rais naye ameguswa na jambo hili, amesikia maoni ya Watanzania wote, ameshatoa maelekezo kwamba tuyafanyie kazi haya malalamiko ambayo wananchi wanayatoa." - Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Nchemba.....
Huyu rais hawezi toboa sababu hana msimamo.
 
Lazima usome chochote ambacho kinahusu kuweka sahihi
Yaani unaamini kabisa Rais wa nchi atakaa na kuanza kusoma mikataba, na miswada?! Atasoma mikataba na miswada mingapi?! Na nimekuuliza, wakati Rais anakaa kusoma mikataba na miswada, wakati huo Mwanasheria Mkuu wa Serikali anafanya kazi nini, na ameajiriwa kwa kazi ipi?
 
Mhe. Rais naye ameguswa na jambo hili, amesikia maoni ya Watanzania wote, ameshatoa maelekezo kwamba tuyafanyie kazi haya malalamiko ambayo wananchi wanayatoa." - Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Nchemba.

Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Mwigulu Nchemba, amesema jambo hilo tayari limefika kwa viongozi wakuu wa nchi na tayari Majaliwa ameitisha kikao na wizara ya fedha na Ile ya mawasiliano kwa ajili ya kulipatia ufumbuzi.

Dk. Nchemba amesema kikao hicho kitafanyika kesho na hivyo ameowaomba Watanzania kuendelea kuwa watulivu na kuisikiliza serikali yao na siyo kusikiliza maneno ya watu ambao wamekua wakifanya upotoshaji mitandaoni.

"Niwaombe Watanzania muwe watulivu, jambo hili limeshafika kwa viongozi wetu wakuu na Rais wetu Samia Suluhu Hassan ameguswa nalo na amesikia maoni ya Watanzania, hivyo tayari ameshatoa maelekezo kwetu ya kufanyia kazi hoja zote zinazotolewa na wananchi," amesema.

"Tunaamini kupitia kikao na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kesho tutatoka tukiwa na muelekeo wa pamoja, kwa hatua ya Sasa niwasihi Watanzania kuendelea kuwa na imani na serikali yao na kumuunga mkono Rais Samia katika utekelezaji wa majukumu ya kuijenga Nchi yetu," amesema Dk. Nchemba.

Ametoa rai kwa wale wote wenye nia ovu kuacha kufanya upotoshaji kwa wananchi na badala yake amewaomba Watanzania kusikiliza maelekezo yote yanayotolewa na viongozi na kuahidi kuyatolea ufafanuzi na maelekezo mambo yote ya kikanuni.
"Rais Samia ana nia njema ya kuijenga Nchi yetu, ni jukumu letu kama wananchi kuendelea kumuunga mkono na siyo kusikiliza wababaishaji wanaofanya upotoshaji," amesema.

Waziri wa Habari na Mawasiliano, Dk. Faustine Ndugulile, amesema wizara yake itaendelea kushirikiana na wizara ya fedha katika kutolea ufafanuzi sheria hiyo, huku akiwaondoa hofu wananchi na kuwahakikishia kuwa serikali yao ni sikivu na inajali wananchi.
Jamani Mama atafanya mangapi? Musaidieni kuondoa kodi mzigo kwa wananchi sio mpaka watu waandamane.
 
Back
Top Bottom