Uchaguzi 2020 NEC yamuita Tundu Lissu kufika mbele ya Kamati ya Maadili ya Taifa

Uchaguzi 2020 NEC yamuita Tundu Lissu kufika mbele ya Kamati ya Maadili ya Taifa

Sisi wananchi tunataka kampeni za kistaarabu za wagombea kunadi sera tuwasilikilize tufanye maamuzi Sasa Kama wagombea watakuja majukwaani na matusi na lugha za kashfa tutawapimaje?

Tume mmepewa mamlaka ya kusimamia uchaguzi nchi hii Kama mgombea yoyote kafanya kosa la kiaadili achukuliwe hatua bila kujali ukubwa wake walal ukubwa wa chama chake. Tume simamieni sheria
 
Lisu ni debe tupu!

Ukiona mtu anakutaja sana ujue umemzidi.

Lakini pia mwacheni Lisu aropoke atakavyo maana ni sehemu ya tiba kwa yaliyomkuta.

Lisu ni debu tupu.
Nani kakudanganya? Kama ni debe tupu mbona mmeacha kunadi ilani yenu mmebaki kusubiri atasema nini ili mujibu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaha mnamuombea poo?!

Anamshambulia mgombea mwenzake, sasa ataanzaje kuishambulia serikali?!

Serikali ni sote watanzania we vipi?!

Umeoa wapi mchezaji anakabana namashabiki na kuacha kukaba wachezaji wa team pinzani?!
Pia timu ikifanya vibaya anaeshambuliwa na kufurumushwa ni kocha, kwanini serikali iwe ya Magufuli, flaiova za Magufuli, Tanzania ya Magufuli, barabara za Magufuli alafu huyo Magufuli mwenye mali zake akishambuliwa wanalia lia?
Watulie kama walivokua wakitulia Magufuli alipokua anashangiliwa na kusifiwa.

Sent from my TECNO K9 using JamiiForums mobile app
 
Si Gumu kwani hata huyo kiongozi wa CCM , Mkapa alisema kuwa tunahitaji tume huru . Yaani yeye hajui maana ya Tume huru??

Hivi Bashiru aliposema ikiwepo Tume huru , CCM haiwezi kushinda , hivi haelewi maana ya Tume huru ??

Ni wewe tu unayejifanya huelewi ndio unakuja na story mpya

Hivi wale wanaosimamia mechi za Yanga na Simba hutoka mbinguni ??
Sipo hapa kumuuliza Mkapaau Bashiru,ninakuuliza wewe uliekuja na hoja ya time huru hapa.
Ikiwa wewe mwenyewe hauwezi kusimamaia hoja unazozianzisha mpaka nimtafute mkapa(RIP) au Bashiru, nataka nikushauri uache mkumbo wa kubeba hoja sehemu bila kuelewa misingi yake ni nini.
 
Unaweza vipi kuitenga serikali ya awamu ya 5 na Magufuli.

Magufuli mwenyewe na wanaccm wenzake wanaaiita serikali ya Magufuli.

Wewe ni nani useme asielekezewe lawama yeye wakati toka mwanzo amejinasibisha na serikali kuwa mali yake.

Wacha apewe stahili yake
Malalamiko ya Tundu Lisu anapaswa kuyaelekeza ama kwa serikali au kwa bunge linaloisimamia serikali lakini siyo kwa Dr Magufuli kama mgombea.

Lisu anapaswa kuzilalamikia sera za CCM kama anaona zimefeli maana kinachoshindanishwa sera za vyama siyo watu.

Huu mtindo wa kushambulia watu binafsi tusipoukemea utatufikisha pabaya.
Yuko wapi Sadiffa aliyekuwa anamzushia Lowassa kila aina ya uzushi?
Siasa siyo uadui wagombea mnapaswa kuheshimiana.

Johnthebaptist leo Iringa mjini.

Maendeleo hayana vyama!
Sifa zilizokuwa zinamwagika mfululizo kwa jenzi za mabarabara si kwa serikali ya chama cha mapinduzi bali zilienda kwa Rais magufuli vumilieni na lawama ziende kwake pia
 
Mkuu umejibu vizuri kuliko wote waliojaribu kuikabili hoja yangu hapo 🖕 juu.
Ingawa tukubaliane kwamba hakuna sehemu unaweza kupata watu wasiofungamana na upande wowote wa kisiasa.Hata Sasa time inalalamikiwa na CDM kwasababu watu wake wamelalia upande wa CCM, laiti kama watu wa tume wangekuwa upande wa CDM,Amini kwamba walalamikaji wangekuwa ni CCM.
SWALI LANGU:Tunawezaje kupata time Yenye watu wasiofungamana na upande wowote wa kisiasa,hata Kama hawatateuliwa na Rais aliepo madarakani?
Pamoja na kusifu jibu ulilopewa, ambalo ni sahihi kabisa, bado unakomaza shingo tu?
Ina maana hukuelewa jibu au unazi umekuzidi kimo kiasi huwezi kuona kitu chochote kilicho tofauti na yaliyomo akilini mwako?
 
Ngoja nikusaidie kidogo, pamoja na kuona uwezo wako wa fikra ulivyo chini sana. Tume inaweza kuundwa kwa njia mbalimbali na bila ya kutegemea manazi wa chama kimoja pekee.
Kama bado huelewi hiki, wewe huwezi kuelewa chochote.
Uwezo wangu wa kufikiri utaonekana ni mdogo kutona na udogo wa ubongo wa mtu anaetaka kujibu hoja zangu.Subiri hoja za hoyehoye userereke nazo.
 
Sipo hapa kumuuliza Mkapaau Bashiru,ninakuuliza wewe uliekuja na hoja ya time huru hapa...
Wapi nilikuambia ukamuulize Mkapa na Bashiru? soma nini nimeandika bila jaziba . usipindishe hoja please
 
CCM mmeanza lini siasa za kuheshimiana hasa huyu mgombea wenu asie na breki mdomoni...
Kuliko kujifariji ni afadhari mkaendelea na maisha yenu tu kutafutia watoto wenu unafuu wa maisha,ni bora zaidi kuwa huna chama kuliko kushabikia upinzani huu wa kipuuzi tu
 
Mkuu umejibu vizuri kuliko wote waliojaribu kuikabili hoja yangu hapo 🖕 juu. Ingawa tukubaliane kwamba hakuna sehemu unaweza kupata watu wasiofungamana na upande wowote wa kisiasa.Hata Sasa time inalalamikiwa na CDM kwasababu watu wake wamelalia upande wa CCM....

Suala la kuwa na mahaba na chama fulani sio dhambi,shida ni kuonesha hayo mahaba hadharani!Swali lilipaswa kuwa watumishi wa tume wanapata wapi ujasiri wa kuonesha mahaba yao au kupendelea bila woga?

Na hapa ndio linakuja suala la msimamizi wa sheria ndio huyo ambaye amewateua viongozi wa tume!Hivyo hawana woga wa kuwajibishwa kwa maana wanampendelea huyo mwenye mamlaka!

Majibu ya haya yote ni katiba mpya itakayopunguza mamlaka ya Rais na kuzipa taasis nguvu zaidi kutekeleza majukumu yao kwa uhuru!
Kwanini marekani wameweza?

Sisi hatujashindwa ila kwasababu mfumo unawabeba watawala basi wanaukumbatia!
 
Hatimaye kamati ya maadili Nec yamuita mgombea Uras kupitia chama Cha demokrasia na maendeleo "chadema" kwa ajili ya mahojiano zaidi.
 
Pamoja na kusifu jibu ulilopewa, ambalo ni sahihi kabisa, bado unakomaza shingo tu?
Ina maana hukuelewa jibu au unazi umekuzidi kimo kiasi huwezi kuona kitu chochote kilicho tofauti na yaliyomo akilini mwako?
Hutapata mtu asifungamana na chama chochote,zaidi ya kufanya balancing kama ilivyo sasa.Tatizo lenu mmeshajijengea mawazo kuwa kila anaeteuliwa na Rais Basi lazima ataunga juhudi 😂, na ndio maana kelele za tume huru kwenu hazitaisha.
 
Inatosha kushughulika na mtu kama wewe.
😂😂😂😂 huna hoja.
Suala la kuwa na mahaba na chama fulani sio dhambi,shida ni kuonesha hayo mahaba hadharani!Swali lilipaswa kuwa watumishi wa tume wanapata wapi ujasiri wa kuonesha mahaba yao au kupendelea bila woga?Na hapa ndio linakuja suala la msimamizi wa sheria ndio huyo ambaye amewateua viongozi wa tume!Hivyo hawana woga wa kuwajibishwa kwa maana wanampendelea huyo mwenye mamlaka!
Majibu ya haya yote ni katiba mpya itakayopunguza mamlaka ya Rais na kuzipa taasis nguvu zaidi kutekeleza majukumu yao kwa uhuru!
Kwanini marekani wameweza?

Sisi hatujashindwa ila kwasababu mfumo unawabeba watawala basi wanaukumbatia!
Nimekuelewa 🙏🙏
 
Malalamiko ya Tundu Lisu anapaswa kuyaelekeza ama kwa serikali au kwa bunge linaloisimamia serikali lakini siyo kwa Dr Magufuli kama mgombea...
Ila yeye MagufuLi akisema “mtu kashiba ugali anakuja kusema ndege hazina faida kwani alikuja kutoka nje kwa bajaji?” Hii siyo persanal?
 
Sipo hapa kumuuliza Mkapaau Bashiru,ninakuuliza wewe uliekuja na hoja ya time huru hapa.
Ikiwa wewe mwenyewe hauwezi kusimamaia hoja unazozianzisha mpaka nimtafute mkapa(RIP) au Bashiru, nataka nikushauri uache mkumbo wa kubeba hoja sehemu bila kuelewa misingi yake ni nini.


Tume ya Jaji Fransic Nyalali iliyoundwa mwaka 1991 ilipendekeza mfumo wa vyama vingi na tume huru ya uchaguzi.

Aidha Tume ya Jaji Ropbert Kisanga iliyoundwa mwaka 1999 ilisema hatua ya wajumbe wa tume kuteuliwa na rais ambaye anaweza kuwa kiongozi wa chama kinachotawala katika utendaji wao ama watakuwa na upendeleo kwa chama husika ama watalipa fadhila kwa aliyewateua.

Mapendekezo mengine ni yale ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba ya Jaji Joseph Warioba ambayo iliona umuhimu wa kubadili muundo wa tume ya uchaguzi na kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi.

Katika kitabu chake cha My Life, My Purpose, Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, anashauri kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi ili kuimarisha demokrasia barani Afrika.

Anasema muundo wa tume umekuwa ukilalamikiwa kutokana na upatikanaji wa viongozi wake hivyo, kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi itakayokubalika na vyama vyote vya siasa ndiyo chachu ya kulea na kukuza demokrasia nchini.
 
Back
Top Bottom