Uchaguzi 2020 NEC yamuita Tundu Lissu kufika mbele ya Kamati ya Maadili ya Taifa

Uchaguzi 2020 NEC yamuita Tundu Lissu kufika mbele ya Kamati ya Maadili ya Taifa

Vipi wajumbe wa hiyo kamati ni wa vyama gani?
Je huyu mahera ni mjumbe?
 
Tume isiyo huru ya CCM inaenda kuwahoji chadema wapi na wapi?
 
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imemuandikia barua mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu ya kumuita katika kikao cha kamati ya maadili ya Taifa...
Taarifa za ukweli ndio zipi?

Alafu alivyoongea leo ni kama vile alikuwa anapiga kampeni kupitia chama chake cha CCM.
 
Sasa Kama Hamna Imani na tume inayosimamia uchaguzi,Kuna haja gani ya kushiriki uchaguzi?
Sasa ulitaka wajitowe mpate kupeta kirahisi? Hamtaki Tume huru, tumeamua kumchinja kondoo atavyoelekea . Mwaka huu tutagawana mbao au muondoke tu
 
Mimi hata nashangaa huyo Lissu wanamsumbua wanini wakati wingi wa watu siyo hoja ya ushindi, Mimi naona Membe ndo tishio maana akibebwa na chadema na wapambe wa CCM waliokaa kimya lazima CCM itikisike Tena dakika hizi za majeruhi Bora wamuache Lissu na kampeni zake.
 
Mbona kawajibu teyar, nanukuu kasema haendi na amerudia kusema atayevuruga uchaguzi atashughulikiwa
 
Labda Phd ya kemikali za kuua mbu... Pamoja na phd yake haimsaidii kitu... Hoja yako hii ya KIPUUZI sana mkuu, ficha aibu hata kidogo..

Sent using Jamii Forums mobile app

angalia tu usije ukazimia kwa chuki, vumilia bana! hapa ndo tunajua walioenda shule kweli na waliokua wanajifunza kutunga IMLA shuleni., si mmemskia jamaa ana akili kuliko nyerere maaana alimtukana matusi ya kutosha
 
alielewa nn sasa wakati amesoma HGE? ana diploma ya HGE, mwenzake ana PHD ya chemistry! sasa nan mbuzi apa
Post hii inakutambulisha Kama mtu mwenye Elimu ndogo kabisa. Enzi zile tukiwa chuo,kijana mmoja mtanashati alikamatwaa akiiba,ili kuepuka kichapo alijitete kuwa yeye ni mwanafunzi mwenzetu anaomba tusimzuru,alipoulizwa kozi anayosoma akasema anasoma PCM
 
Aliongelea mgombea individual na kumtaja jina lake? Akamtaja Labda Tundu Lisu kwa jina? Ulishamsikia Magufuli akimtaja Lisu kwa jina lake?
Mwoga ssna yule hayawahi kutaja jina hata pm au vp
 
Post hii inakutambulisha Kama mtu mwenye Elimu ndogo kabisa.Enzi zile tukiwa chuo,kijana mmoja mtanashati alikamatwaa akiiba,ili kuepuka kichapo alijitete kuwa yeye ni mwanafunzi mwenzetu anaomba tusimzuru,alipoulizwa kozi anayosoma akasema anasoma PCM

sasa kwan ni uongo? lissu hajasoma HGE? magufuli hajasoma phd ya kemia? kwamba mnataka mmtetee hajasoma HGE ama? 😂 😂 😂
diploma ya kuandika imla😂 na mipasho
 
Mwoga ssna yule hayawahi kutaja jina hata pm au vp

zile ndo sheria sister, ndo maaana wanasema fanyeni kampeni za kistarabu, ukifanya kampeni unatakiwa uwe na adabu pia! tumia lugha nzuri kunadi sera zako na pia jitahidi kushawishi wananchi kwa uwezo wako wote ukitumia staha

sasa jamaa ana mdomo mchafu alafu anajiona kama ndo anajua sheria peke yake nchi nzima, ona yanayomkuta sasa, aende kujibu nec, akimaliza akikosa uraisi kuna kesi znamsubiri, kule wananchi wanataka kumpiga mawe uku kwingine wasiojulikana wanamweka target
 
Back
Top Bottom