Ongea ya Rais Samia imebadilika tangu sakata la bandari lianze

Ongea ya Rais Samia imebadilika tangu sakata la bandari lianze

Amegundua kuwa kumbe watanzania wanaweza kuamua kufuatilia mambo yao, kuyaelewa vizuri na hata kuyakomalia kwa hoja.
Haya mambo ni kelele za kwenye mitandao tu, lakini mtaani watu wako bize na mambo yao. Na huu ni upepo utapita, Raisi ni taasisi inayopima mambo, kufeli kwa maandamano ni dalili kua hizi ni kelele za mitandaoni tu.
 
Haya mambo ni kelele za kwenye mitandao tu, lakini mtaani watu wako bize na mambo yao. Na huu ni upepo utapita, Raisi ni taasisi inayopima mambo, kufeli kwa maandamano ni dalili kua hizi ni kelele za mitandaoni tu.
Hujui kuwa mitandao ndio njia ya kisasa ya kutoa hoja bila kuhitaji kundamana mitaani na inafanya kazi kubwa mno? Ona Samia alivyonyong’onyea kwa maandamano ya mitandaoni pekee.
 
4. Anahisi kupoteza uungwaji mkono na heshima aliyojijengea (loss of trust).
 
Wabongo baada ya kushtuka bandari zao zinauzwa kwa mwarabu, mazeri sauti ya ujasiri na kujiamini imeondoka kabisa mdomoni kwake wakati wa kuhutubia,Pengine anapisha upepo mbaya upite.
 
Sauti ya ngapi anatumia sasa baada ya kelele zetu?
 
Spana zinazopigwa kuhusu bandari lazima ajisikie siyo poa.
 
Kwa anayefuatilia hotuba za Rais Samia atagundua kuwa namna yake ya kuzungumza na hulka yake vimebadilika kwa kiasi flani tangu sakata la bandari lianze. Ile sauti yake ya kurelax na kujiamini imetetereka kidogo. Sina uhakika kama ni hali ya hewa na kibaridi hiki.

Lakini hii yaweza kumaanisha nini?

1. Kwamba ameguswa na yanayoendelea kuhusu bandari

2. Hakutegemea yanayoendelea kufika mbali hivyo

3. Ni dadili ya kusutwa dhamiri

4. Anahisi kupoteza uungwaji mkono na heshima aliyojijengea (loss of trust).

5. Amekuwa kwenye shinikizo (stress) kubwa kipindi hiki

6. Amegundua kuwa kumbe watanzania wanaweza kuamua kufuatilia mambo yao, kuyaelewa vizuri na hata kuyakomalia kwa hoja.

7. Amekuwa defensive na mwenye mipasho kinyume na tunavyomjua.

Ama kwa hakika hiki ni kipindi kigumu kwa rais wetu.

Sasa;

Anapaswa kuwa mkweli kwa nafsi yake na kwa nchi yake.

Anapaswa kuruhusu mchakato wa wazi na wa kizalendo juu ya bandari zetu.

Anapaswa kuepuka wasaidizi wake wanaomsifia kupita kiasi na kumshauri kinafiki.

Tunamwomba rais wetu asibweteke na kuanza siasa za kibabe kama anavyoshauriwa na wanafiki wengi waliomzunguka kwani mkakati huu utakuwa na madhara makubwa kwake na kwa wananchi.

NB: Suala la kupuuzia marekebisho ya katiba litamletea fedheha kubwa zaidi siku zijazo.
Mda si mrefu zomea zomea ya enzi za mzee wa Msoga itaanza., ukikatiza tu unamavazi ya kijani jamii inaanza kukuzomea.
 
Anaongea kama anataka kulia

Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
 
Amesema ameweka vizibo masikioni .hasikii wala hataki kusikia
Utaweka vizibo baada ya kwanza kukisikia kinachoongelewa. Mara moja moja lazima utatoa hivyo vizibo Ili kunyonya nondo za wazalendo wa Kitanganyika.
 
Huwa najiuliza hivi wakati wa kutuomba kura 2025 atakuwa na ujasiri wa kutoka wapi kama sasa hivi hawajali wamama na wananchi wanyonge (wa hali ya chini) ambao ndo maskini ya Mungu huwa wanapiga kura kwa uaminifu kulinganisha na matajiri ambao kwanza ni wachache na pili wengi wao hawanaga muda mchafu wa kwenda kupiga kura!
Hivi unadhani anaweza kupata kura ngapi kutoka Tanganyika? Nadhani Chama chetu kitatumia njia yoyote Ili asisimame.
 
Amalizie urithi wake apite hivi
2025 nahamasisha maandamano ya katiba mpya badala ya kampeni za uchaguzi ni kuhamasisha watu kadai katiba kabla ya kuingia uchaguzi

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom