Picha: Tupatie update ya eneo lako husika- El nino 2023/2024
Bahari ina kupwa na kujaa. Bahari ikijaa unahisi maji yataenda wapi?

Kwanza Bamvua limekaribia, walijua weye?
Kwa hiyo unaona ni Sawa Jiji la Dar Salaam kujaa Maji Kwa Mvua ya Siku moja Wakati jiji liko kwanye ukingo Wa Bahari ambako Maji na mito yote Duniani inaishia hiku.

Maji kujaa na Maji kupwa hakujawahi kusababisa mafurika .Tukio la Maji kujaa na Maji kupwa halisababishwi na mvua Mkuu.

Mbona mnatetea Viti Vya kijinga Badala ya kuwaambia watendaji wanaosimamia Kodi Zenú watumie akili kushughulikia majanga madogo yanayohitaji akili na maarifa ya binadamu Badala ya kusingizia Vitu visivyo na maana.

Jiji la Dodoma lipo kwenye Bonde la ufa pakijaa Maji ni Sawa Lakini sio jiji la Dar es Salaam ,Tanga,Mtwara na Lindi au mji wa Kilwa.

Tatizo watu Wa mipango miji wanawaza starehe zao na Serikali haisimamii watendaji wake ipasavyo.
Waliohamishiwa Mabwe pande waliishia wapi mpaka Leo Bonde la mto msimbazi Bado wamejenga na wanaishi.

Kwa nini baada ya kuwahamisha hatukuona magereda yakichimba mitaro mikubwa ya Maji na kuzuia ujenzi holea Wa kuzuia mikondo ya Maji.

Maji yanazuiwa Kwa ama kujenga malambo ya kupunguza Kasi yake na kukontro uelekeo au kuwejenga mifereji ya kuyapitisha Moja Kwa moja bila kukwama.
 
Wakuu, tujuzane huko ulipo hali ikoje kwa picha na video, na kama kuna sehemu ina changamoto toa taarifa haraka kwa mamlaka husika kuepusha athari kubwa.

Bila kusahau, tuchukue tahadhari kipindi hiki chote cha mvua.

Mzazi, kama mtoto wako anasoma mbali na miundombinu ni mibovu ni bora ukaacha leo apumzike, asije kukutana na majanga ukaishia kujuta.

Wengine wamekutana na majanga asubuhi asubuhi, jamaa kanasa kwenye mtaro maeneo ya Tegeta

Tunashukuru kwa picha na taarifa
 
FB_IMG_1699002110882.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mvua ni ya kawaida tu, ila miundo mbinu yetu ni mibovu, tumejenga kiholela holela.
Ila dar mji una laana sana, mvua ikikatika tu joto liko pale pale.. 😂🤣
 
Amani kwako.

Jiji la Dar Es Salaam na Zanzibar ni kati ya mikoa iliyotajwa kuwa na mvua kubwa zitakazopelekea mafuriko na hali ya sintofaham.

Mvua ya toka jana jioni hadi leo imepelekea baadhi ya sehemu kadhaa kukubwa na mafuriko katika mini hii iliyotajwa hapo juu Dar Es Salaam na Zanzibar.



Picha hii hapa ni kutoka darajani Zanzibar.
Screenshot_2023_1105_175652.jpg


Na hii hapa chini ni jijini Dar Es Salaam.
Screenshot_2023_1105_175555.jpg


Update: 06.11.2023
📍Zanzibar.
Leo wana nafuu ila wingu limetanda, so wanaweza kununua vyakula na kufanya daily works kupata kipato.

📍Dar Es Salaam.
Kuna uwezekano eneo moja inakunya na kwingine hainyi ila bado hali ya hewa maeneo mengi ni ya kufirika.

Picha kwenye komenti 😄!.
 
Back
Top Bottom