..watolee ufafanuzi kwanini Rsisi akisafiri huagwa na kupokewa uwanja wa ndege na utitiri wa viongozi wanaoendeshwa kwenye ma-V8.

.. Kwanini viongozi hao wasipande basi maalum kwenda kumuaga au kumpokea Raisi uwanja wa ndege?
Kwani wana muaga amekufa?
 
Kazana baba yasiwe ni maneno tu kumbuka bado tunatawaliwa sijui huyo mtoto wako utamfundishaje labda ujenge shule yako na mitaala isiwe hii tuliyonayo hapo utafanikiwa.
 
Lete picha ya Rais wa ufaransa au waziri mkuu wa Canada au viongozi wa G7 waliopanda yutong Acha kutetea haya madharau.usitete ukoloni mamboleo.usiwe kipingamizi wa afrika mpya.
Usikute hata chakula cha msibani wamewekewe kwenye masinia mkao wa wanne wanne. [emoji1787][emoji1787]

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
Tatizo letu ni kudharau vya kwetu na kuona baadhi ya tamaduni zetu ni primitive mfano mwenge.

Hawa wenzetu symbolism na mambo ya traditions wanachukulia serious pamoja na kuwa wameendelea.

Huko kwao leo TV zote hakuna kuonyesha matangazo ya biashara kwa sababu leo ni siku ya msiba sio ya kibiashara (imagine hela ambazo TV zimekosa leo).

Heathrow Terminal zote sasa hivi kuna cancellation ya ndege kupaa na kutua wakati Queen anaingia Windsor sio mbali na uwanja wa ndege; awataki marehemu apigiwe kelele wakati anaingia kulazwa nyumba ya milele (imagine stress za wasafiri, Heathrow ndege inatua na kupaa kila dakika 5). Uzuie ndege kutua na kupaa kwa masaa kadhaa si unatengeneza backlog ya kufa mtu.

Kuingiza viongozi na mabasi aina uhusiano wowote na dharau ni kwenye ku focus na tukio lao na eneo ni sehemu ya maombolezi awataki ghasia zingine ziwatoe nje ya tukio kwa heshima ya Queen.

Isitoshe viongozi wote walienda na ulinzi wao binafsi ni nje tu ya kuingia eneo la kanisa barabara ambayo waombolezaji wamejipanga (wengine wamelala hapo siku kadhaa ili wawe mbele ya fence) ndipo waliposhuka na kuingia na basi kwa pamoja kumalizia safari kwa heshima ya waombolezaji. Focus ni msiba sio wao.

A fuss about nothing
 
Aibu!

Huko London kwenye msiba wa Queen Elizabeth II, Rais Samia wa Tanzania ni mmoja wa Viongozi waliopandishwa kwenye basi.

Nb: Kuna kila dalili Rais wa bongo alikuwa ana mind mpiga picha πŸ˜„.

View attachment 2361396
Loo!.Naona kila mmoja anaona haya.Siku nyengine wakilikwa kwenye mambo kama haya watajiuliza.
Mtaka nyingi nasaba hupata mingi misiba.
 
Aibu!

Huko London kwenye msiba wa Queen Elizabeth II, Rais Samia wa Tanzania ni mmoja wa Viongozi waliopandishwa kwenye basi.

Nb: Kuna kila dalili Rais wa bongo alikuwa ana mind mpiga picha πŸ˜„.

View attachment 2361396
kwani Rais Samia Suluhu amepanda basi peke yake acheni maneo maneno mama katuwakilisha vyema na anaimarisha Diplomasia Tanzania
 
Tunaweza kuokoa gharama kubwa ya usafiri wa viongozi wetu na tukaepukana na hizo tuzo ambazo zinazalishwa kila siku.

Mfano Rais Samia akiwa Dar ana anatakiwa kwenda Dodoma.Asubuhi anawahi stand anapanda Kimbinyiko na maafisa wake wote.

Waziri Mkuu anaweza kupanda Dar Express from Dar to Arusha hizi tozo tusingezisikia hata kidogo.
 
Inaonekana wewe na mwenyekiti wa EFF ya South Africa Hon Julius Malema mko na same school of thought kuhusu ubeberu
 
Wewe ndiyo usiyekuwa na ufahamu kuhusu kitu kinaitwa "Power Relations" kwenye nyanja mbalimbali na hasa linapokuja kati ya taifa na taifa na athari zake.

Kuna siku Obama alienda Saudi Arabia halafu akajiinamisha chini ya mfalme wa Saudia, wamarekani waling'aka hapana mfano.

Kuna stori (sijui kama ni kweli maana sikuwepo) kwamba Malkia wa Uingereza alimsalimia Nyerere huku mikono yake kavaa gloves, Nyerere kuona hivyo naye akareciprocate kwa kumgea kifimbo chake.

Hizi folklore zote zinatengeneza jambo moja la msingi: kutawaliwa kimwili na kiuchumi kunaanza kwa mtu kutawaliwa akili na roho. Msipende kuchukulia vitu poa kudunishwa kwa Rais wa nchi. Ripple effect yake kwa watu wa taifa analoliwakilisha ina nguvu sana.

Kwangu binafsi Rais Samia haniwakilishi mimi huko alikokwenda sijui kuhudhuria msiba wa nani vile. Hilo basi alilopandishwa kapandishwa yeye kama Samia na wala hawajapandishwa watu wa taifa analoliongoza. Watanzania tuna legacy ya taifa kubwa lililowahi kuongozwa na Nyerere na Magufuli na hatuna uduni uduni wa dizaini hizo. Tunaweza kuwa hatuna uchumi mkubwa wa vitu lakini tuna hazina kubwa ya akili na ufahamu na hatukubali uduni wa akili wa wanasiasa walioangukiwa na bahati nasibu ya kutuongoza.
 
Jiheshimu na uache uongo Frace, Germany,Japan,Canada,na USA hawajapanda basi

Sent from my CPH1823 using JamiiForums mobile app
 
Hamnaga argument based on hearsay & conspiracy mkuu. Argument inajengwa na facts.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…