ras jeff kapita
JF-Expert Member
- Jan 4, 2015
- 22,152
- 33,899
Wakati wananchi na wafuatiliaji wa mambo wakianza kujengewa imani ya kuwa Taifa letu linarudi kwenye utawala bora lakini pia tukielekea kwenye utawala wa sheria na Uwajibikaji kwa viongozi wetu mfano ni kufikishwa Mahakamani kwa aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Hai , Ndugu Lengai Ole Sabaya.
View attachment 1808395View attachment 1808396
Katika kumbukumbu zetu wakati taifa la Marekani wakimpiga marufuku RC Paul Makonda kuingia nchini kwao kwa tuhuma mbalimbali walisema sababu kubwa ilikuwa wana taarifa na ushahidi wa uhakika kutoka vyanzo vyao kuwa kuna mambo ya kihalifu dhidi ya binadamu aliyokuwa akiyatenda. kwa kutumia nafasi yake ya ukuu wa mkoa.
Tunavyojua sisi kuwa vyanzo vyao ni CIA ikishirikiana na taasisi zingine kama MOSAD, MI6 na taasisi zao zingine kama NSA,FBI, n.k. Sasa Taarifa hizi na Ushahidi(INTEL) dhidi ya Makonda wanazo hawa ndugu zetu na tunadhani wako tayari kuzitoa kwa hatua zaidi. Ni wakati sasa wa vyombo vyetu vya Ulinzi na Usalama kuwasiliana na wenzetu wa USA na kupata hizi taarifa na ushahidi wao na kuzichunguza ili kuthibitisha au kumsafisha.
Yeye mwenyewe alijitetea na kusema sababu ni kupambana na ushoga lakini ikumbukwe Musevene alifosi kutunga sheria dhidi ya mashoga, Bingu wa Mutharika alishawishi mashoga wakafungwa jela,Waziri Mkuu wa Cambodia, Hun Sen aliwahi kuchochea raia kuua mashoga lakini wote hawa hawakuzuiwa kwenda USA, hivyo tusiwapuuze MABEBERU hili, tusiwadharau CIA kiasi hiki kwani lisemwalo lipo.
"Wizara ina taarifa za uhakika kuwa Makonda amehusika katika uvunjifu huo wa haki kupitia nafasi yake kama mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam. Katika nafasi yake hiyo, pia amelaumiwa kwa kukandamiza upinzani wa kisiasa, kukandamiza haki ya kujieleza, na kushambulia makundi yasiyo na sauti," imeeleza sehemu ya taarifa hiyo ya wizara.
Pia Bwana Pompeo alisema ,"Leo tumetangaza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Christian Makonda kuwa hataruhusiwa kuingia Marekani kwa kushiriki kwake katika ukiukwaji mkubwa wa haki za binaadamu. Tuna wasiwasi mkubwa juu ya kuporomoka kwa heshima ya haki za binadamu na utawala wa sheria nchini Tanzania," ameeleza aliyekuwa Secretary of state Ndugu Pompeo katika ujumbe wake huo.
Matamko ya jumuiya ya kimataifa kuhusu uhalifu dhidi ya binadamu yalikuwa mengi sana, ni wakati wa kujisafisha sasa na kujenga mahusiano na jumuiya hii, mfano haya hapa chini:
Paul Makonda awa kiongozi wa kwanza kuzuiwa kuingia Marekani kwa kuwanyima watanzania HAKI YA KUISHI
Serikali ya Marekani imemzuia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuingi nchini humo kutokana na kuhusika kwake kwenye uvunjifu wa Haki za Binadamu unaohusisha kunyima haki ya kuishi, uhuru na ulinzi wa watu. Katika uongozi wake, Makonda ameonesha uonevu kwa wapinzani, kuminya uhuru wa...www.jamiiforums.com
![]()
Tamko la Umoja wa Ulaya (EU) kufuatia ongezeko la matukio ya kisiasa yenye viashiria vya ukatili na vitisho Tanzania
Tamko la Umoja wa Ulaya (EU) kufuatia ongezeko la matukio ya kisiasa yenye viashiria vya ukatili na vitisho Tanzaniaeeas.europa.eu
![]()
Bunge la Ulaya laijadili Tanzania, upi mustakabali wake? – DW – 20.11.2020
Kamati ya mambo ya nchi za nje ya Umoja wa Ulaya ilijadili uchaguzi uliopita wa Tanzania na kutaja kuwa ulikiuka misingi ya kidemokrasia, na suala la kutokuwepo maambukizi ya virusi vya corona. Hakuna uamuzi wowote uliotolewa hadi sasa. Dotto Bulendu ni mwandishi habari na mchambuzi wamasuala...www.dw.com
Unaweza weka na mengine mdau tujikumbushe malalamiko kadhaa ya hawa wateule awamu iliyopita
Na majizi yanayoiba kwa kalamu myapigie kelele yadakwe.....
sio kina Manji mnapiga kelele waachiwe
alafu kina mako... Wadakwe mtakuwa kumbafu nyie