Uchaguzi 2020 Samia Suluhu Hassan: Askari wa Serikali ya CCM akipiga mtu risasi 3 akamkosa atawajibika

Uchaguzi 2020 Samia Suluhu Hassan: Askari wa Serikali ya CCM akipiga mtu risasi 3 akamkosa atawajibika

Ni vyema wakina mama tujiweke kwenye hali ya kuaminika mbele ya jamii hasa linapokuja suala la vijana wa watu - wakike na wakiume. Sisi tukiwa mstari wa mbele kuharibu ‘tamaduni’ na ‘maadili’ haipendezi. Swali pendwa kwa Lissu wamuulize Bi Mkubwa sasa. Haya mambo bwana! Yani Mataga wanafanya mambo wenyewe huko ndani ya chama chao halafu wanakazi ya kusingizia wengine na wazungu, kumbe wao ndio wenyewe wataalamu.
 
Hii kauli ita muumiza sana huyu mama muda wote huwa ni mstaarabu siyo rahisi kutoa kauli tata namna hii na hakuwa na sababu ya kufanya hivyo. Kwa njia hii wanajishitaki bila kujua.

Walio karibu naye wamshauri kuepuka kauli za vijembe ambazo huwa zinaweza kumfanya ajikute anatangaza uhusika wa serekale katika shambulio lile la kinyama kabisa
Itakua alimaanisha waliotaka kumuuwa siyo askar wa CCm lakn sijui kama chama kinakuaga na askar au kamaanisha Hawa askari wanaolipwa kwa kod zetu
 
Alichosema mh.Samia makamu wa Raisi JMT sio sawa au labda sijasikia hotuba yake ndo maana inakua rahisi kutoa hukumu. Ukweli ni kwamba HAKUNA ASKARI BILA MAFUNZO, hii ina maana lszima wajue majukumu yao iwapo wahusika wa tukio la mh.Lissu ni watumishi wa majeshi yetu niamini nikisema mh.Lissu angekua marehemu leo hii labda niwaze kua walikua wanacheza long game kwa faida yao baadae hivyo amri zao hazikua kufanya mauaji au si kweli hawakua wana usalama wa vyombo vyetu vya ulinzi.
 
Mama Samia umenena vyema. Na Lissu aendelee kuwashukuru Polisi kimya kimya maana wanajua kile wafuasi wake hawakijui kuhusu risasi 16!
 
Mbona ipo wazi waliompiga lissu risasi ni kikundi fulani kilichomo ndani ya chadema na ishu yote ni kufifisha nguvu ya Lissu dhidi ya Mwenyekiti Mbowe...
 
Kuna jamaa yangu mmoja alishazoea kusema pumbache...
 
Mama Samia Yuko sahihi, hata Lissu hajasema kuwa police ndio waliomshambulia na anasema wazi alimwona aliyemshambulia na anamfahamu, anacholaumu kwanini police hawamkamati?

Inawezekana aliyeenda kumshambulia hakupaswa kwenda Ni keherehere chake tu, au aliyepaswa kwenda alipuuza mjinga mwingine akaamua kujichukulia amri mkononi.

Anachosema mama kuwa ile Ni dhambi ya mmoja na sio ya chama au serikali na ingelikuwa ya chama au ya serikali wangetumwa wataalamu wa hiyo kazi

Nakubaliana kabisa na wewe mkuu kuwa ingekuwa State operation basi isingeweza kufail Swala la Lissu na relate na Inshu ya Chacha Wangwe. Lissu alishakuwa threat hata ndani ya Chama chake na ivo hana hela amekuja tu kuwa Mzigo kwa sasa ila Chair man hana Jinsi mana Lissu ana influence kiasi fulani.
Freeman alipenda zaidi aende na Lazaro ila influence ya TAL imefanya akose option zaidi kumruhusu Lissu avie for CDM, Shambulio la Lissu naliona kabisa kuwa limekuwa organized na watu wake wa Karibu tu na sio state
 
Huyu mama kipindi cha bunge la katiba nilikuwa nasikiaga vituko vyake na mimi karibu ningeenda kuosha rungu. Dah aliichafua Dodoma hatareeeee
cc Victoire
Mawaziri wa kike wote files zao tunazo. Wakijichanganya wanalipuliwa tyuuuh
 
..kuna comment alitoa kuhusu wabunge wa vyama vya upinzani wakati wa bunge maalum.

..nadhani kulitokea mzozo na wabunge hao wakaamua kutoka nje ya ukumbi, sasa kuna kauli aliitoa ndio ilinifanya nijue kwamba iko siku tabia zake zitakuja kujulikana/kujitokeza waziwazi.

..Mama Samia alimtembelea Tundu Lissu akiwa hospitali Nairobi na alimkuta katika hali mbaya sana akiwa bado kitandani.

..Na waTz wengi tulimpongeza kuwa amefanya jambo la kiungwana. Sasa imekuwaje mtu ambaye alimuona TL akiwa kitandani ni mgonjwa, leo aanze kumtolea maneno ya kashfa? Kwa maoni yangu ni afadhali maneno hayo yangesemwa na mtu ambaye hakumuona TL kule hospitali.

..Na kibaya zaidi yamesemwa na mwanamke ambaye tunajua ana uchungu wa kuzaa,na anajua machungu ya kuuguza kwani kwa mila zetu wanawake ndiyo wanaouguza na wafariji ktk familia zetu.
Huyu mama alipokuwa bunge la katiba yani alikuwa mwingi balaa
 
Kipindi cha kampeni za mwaka 2015 akajichagulia kina Ummy, Kairuki, Wolper, Aunt Ezekiel na Wema akawa nao kwenye kampeni eti mama ongea na mwanao yani ilikuwa ni laana tupu! Emb niishie hapo ila lazima nimuite Victoire
Saivi ataanikwa hadharani tyuuuh. Hakuna namna lol
 
Nchi yenye jina kubwa katika ukombozi wa bara la Afrika, tumewafundisha Afrika Kusini, Msumbiji, Namibia, Congo, Uganda, nk....tumewaandaa kuanzia mistuni hadi wakawa marais viongozi wengi...hadi kuna wakati Tanzania ilikuwa kama Islael ya Afrika kwa intelgensia! Tuseme kama kweli Lissu alikuwa "adui" wa nchi na sio mchumia tumbo kama wenzake waliopita kumuua Lissu ingechukua dk ngapi? mbinu na medani zote kuanzia "anhtrax", kiharusi, sumu, ajali ,nk, zote ziligoma hadi kumpiga risasi za miguu tu na kuacha kichwa na kifua au "sniper" wetu wote waliotumikia na wanaoendelea kutumikia nchi hii walikuwa likizo?
Endeleeni kuidhalilisha "system" yetu kuwa inapanga mashambulizi ambayo hata wezi wa kawaida ukiwakodi hawawezi kufanya ujinga kama huo!
 
Back
Top Bottom