Serikali: Walimu sasa kufanya mtihani wa kupima uwezo kabla ya kuajiriwa

Msimlaumu mkwezi nazi imeliwa na mwezi !

Msimlaumu Mkenda bure maana hilo ni hitaji la nyakati hata angekuwepo mtu mwingine kwenye hicho cheo angeamua Kwa namna hiyo hiyo.

Mabadiliko hayanabudi kuja.
 
Kwanza ingefaa ualimu waende wale walofaulu kwa ufaulu wa juu sana (Top Cream) ili wanafunzi wapate elimu bora zaidi kwa maendeleo ya Taifa letu badala ya hali ilivyo sasa.
 
Watu wafanye mtihani, Kuna wengi wamefundishwa blablaaa na Wana GPA kubwa lakini kichwani empty kabisa. Mwl lazima awe ameiva hasa, hata vyuoni Kuna walimu bure kabisa. Yaani mtu anaingia lecture anasoma kitini mwanzo mwisho anatoka, huyu si wakufukuza kabisa huyu. Mwalimu lazima awe na uwezo wakufundisha siyo kusoma shairi. Piga mtihani kabisa Kuna wahuni wanaharibu kada ya ualimu. Hapa degree halali na za chupi au pesa zitajipambanua.
 
Kwanza ingefaa ualimu waende wale walofaulu kwa ufaulu wa juu sana (Top Cream) ili wanafunzi wapate elimu bora zaidi kwa maendeleo ya Taifa letu badala ya hali ilivyo sasa.
Kuna wale wenye GPA za guesthouse, hao wakafundishe watoto wetu siyo.
 
Ameseme ualimu ni chaguo la mwisho baada ya kufeli sehemu zote. Waziri wa elimu kayasema hao dar Es salaam View attachment 2660431View attachment 2660432

Mpwayungu Village
Siwabezi walimu na ndio wote tunaoweza kuandika na kusoma tumepitia kwao, huo ndio ukweli aliosema Waziri lakini sio wote wanaochagua Ualimu ni kuwa walikwama kupata machaguo mengine.

Kipindi kabla mfumo wa kuajiriwa moja kwa moja haujaharibiwa, baadhi ya Watu waliamua kusoma Ualimu ili pindi wakimaliza masomo waweze kuajiriwa moja kwa moja ili wakidhi haja zao za kimaisha, na wengine waliamua kusoma ualimu kwa mapenzi ya kufundisha.
 
Aina gani ya mtihani watapewa kupima uwezo wao...?
 
We kweli ndo ujui kitu ungejua hakuna madarasa magumu kufundisha kama hayo uliyoyataja apo
 
Safi kabisa na isiishie hapo tu wapimwe na vipimo vya kijinsia kwa walimu wa kiume ijulikanwe ni mashoga au laa na walimu wa kike kadhalika, na sekta nyingine zote iwe namna hii kutokana na hali na zama hizi tulizopo mambo yamekuwa mengi.
 
Hadi Afya wapitie usaili wa kazi.
 
Ukiona hivyo ujue kuna watoto wa wakubwa wameoshalamba vitengo.....hii ni njia ya kuwabana na kuwaminya watoto wa walalahoi.....hongera sana bwana mkenda kwa kuanzisha utaratibu mzuri
Hata hao wakubwa wanaowapa connection za ualimu vijana wao watakuwa wendawazi Bora wawape mitaji midogo tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…