Spika Tulia Ackson: Mtu akimsema vibaya Rais nyooka naye, akinisema vibaya Nyooka naye
Awamu hii ndio imetuonyesha kwa mwanamke hapaswi kuwa Kiongozi, wametuangusha pakubwa Sana natumai hatutarudia Tena huu ujinga
 
20221003_153234.jpg
 
hapa sio rwqnda sasa.
Yani uyu analeta Mambo ya rwanda na tz? Taifa tutalipeleka pabaya , Kama ambavyo vijana wa ccm ,Wana viongozi , au watalala nao vijana wengine mbele nao Wana viongozi nao watalala nao mbele,

SA ,kenya Rais wananangwa na wajiri wao na maisha yanaenda sie wa kwetu amekua Mungu,

Tulia jiuzulu Mara MOJA na sio Ombi nasema Kama Bwana anenavyo hapa ,ni lazima hustahili kaa kwenye kiti hicho ,
 
Unadhan anaweza kukata mkono unaomlisha????yule andunje alipojaribu kujipapatua kilichomkuta imebaki historia
Dk tulia anasimamia mhimili mkubwa unao Tunga Sheria na kuisimamia serikali!! Kasema watakaomsema rais .
Washughulikiwe!! Mimi najua rais hajawa mungu kwamba asisemwe! Akiifanya vizuri tutampongeza ila akidemka tutamsema bila kuchoka Wala kuogopa kauli ya tulia!! Kama tulia amefikia Mahali pa kutaka rais asisemwe huku uraiani vipi bungeni nako wataruhusiwa kumsema rais akikosea? Rais sio mungu na kamwe hatakuwa mungu !! Kwa nini tulia anamuwekea kinga rais ! Kuna nini? Tutamsema ,tutamsema na tutamsema tena!!! Tulia anaona watanzania wote ni sawa na familia yake !! Asali imemlewesha anzeni kuwashughulikia !! Watanzania sio waoga ila ni wavumilivu!
 
Ndivyo ilivyo huwezi kukubali boss wako asemwe vibaya all in all mkubwa lazima aheshimiwe kwa gharama yoyote na sio utamaduni wetu sisi watanzania kumsema rais vibaya japo kuna wachache miongoni mwetu wanakengeuka na kujitoa ufahamu
 
Yupo sahihi ikiwa anawaambia Vijana wake wa CCM.
Ila hayuko sahihi Kama atakuwa anamaanisha vijana wa nchi nzima.

Kama ndio Katiba ya ccm ndivyo isemavyo yupo sahihi
Haijalishi anawaambia kwa msingi gani. Nani hasemwi nchi hii, kusema vibaya ndio nini kwa watu wenye low level ya understanding na tolerance anything short of kusifia ni kusema vibaya ni matusi. Hii inachochea vurugu na mbaya zaidi huyu mama ni speaker, ni msomi na lawyer kiwango cha PhD. Huu ni ushenzi wa hali ya juu. Mola tuokoe na wajinga kama hawa..
 
speaker wa bunge la jamhuri ya Tanzania Dr Tulia Akson, leo tarehe 3. 10. 2022 alipokuwa anaongea katika kikao na vijana wa CCM amewasisitiza kwamba ikiwa kuna mtu yeyote atakaye msema raisi Samia Suluh vibaya basi wana wajibu wa kudeal naye sambamba.

speaker tulia kauli hii ni ya uchochezi na kauli kama za kwako yalipelekea mauaji ya kimbari, hivyo unachokitafuta utakipata
kama kweli katamka hayo nalaani kauli yake na Mungu adili na yeye kabla ya hao anaotaka yawakute
 
TULIA nyege sinamsumbua tupigane wenyewe Kwa wenyewe CCM wamekata pumzi hawanahoja tena
 
Back
Top Bottom