Tundu Lissu: Watekaji wanataka wanimalize wamsingizie Mbowe
Unajua hiki alichokiandika Lissu haraka sana mimi nilikijua kwamba kitatokea, unaambiwa mbwa ukimjua jina hakung'ati.

CCM iko transparent mno kwenye mambo ya Utekaji na mauaji, ila kwa kukosa maarifa wao wanadhani wamejificha!

Huwezi kuwa na nchi inayowaza kuua tu raia wake halafu ikaendelea
Well said Mwamba
 
Kutoka X Lissu anaandika,

Enyi watu wabaya mjulikanao kama 'watu wasiojulikana,' nimezisikia njama zenu. Mnataka kuniumiza halafu mumsingizie Mwenyekiti wetu wa chama, Freeman Mbowe.

Ndivyo mlivyofanya wakati wa kifo cha marehemu Chacha Wangwe. Ndivyo mlivyofanya tena wakati mliponishambulia tarehe 7 Sept '17. Na ndivyo mlivyofanya miezi michache iliyopita mlipomteka nyara na kumuua Mzee Ali Mohamed Kibao.

Ndivyo mnavyofanya kila mnapoua watu wasio na hatia. Mnasingizia watu wengine ili nyie mnaohusika msiwajibike na udhalimu wenu.

Huyo mnayedhani mnamtumikia alitoa ahadi hadharani kuwa nitakuwa salama nikirudi nyumbani. Waziri wake Masauni alirudia ahadi hiyo bungeni.

Mkiniumiza kama mnavyopanga mjue lawama yote itaangukia kwa Samia Suluhu Hassan. Badala ya kumlinda mtamchafua zaidi. Na kama ilivyokuwa kwa Magufuli baada ya 7 Sept '17, ndivyo itakavyokuwa kwa Samia.
Hahaha naona anaanza kuelewa sasa mchezo. Hiyo September 7, 2017 Mh. Mbowe aka kengeza kwa kushirikiana na mabeberu waliotaka kuona Dkt Magufuli anasingiziwa ndiyo waliotumwa na mbowe wamuue yeye lisu. Ndiyo maana mbowe mpaka leo anakinyongo na huu ndiyo wakati atammalizia kwa sababu ya uenyekiti hahah amuulize ayatola zito alikimbia chama kisa uenyekiti.
 
Wajaribu tukinukishe, maana tumechoka!! Hii nchi ni yetu sote!!wasituchukulie poa!!kisa tuna vyeo vidogo jeshini! hao wanaowaumiza ni ndugu zetu!!
Mkuu jeshi likiamua hata leo mtashangaa jinsi wananchi tutawaunga mkono. Ili nchi yetu ianze upya ni aidha machafuko, ama mapinduzi ya kijeshi. Jeshi pekee ndio nguzo yetu, wananchi wengi tutawaunga mkono.
 
Kumekucha
Screenshot_20241216-203852.png
 
Hahaha naona anaanza kuelewa sasa mchezo. Hiyo September 7, 2017 Mh. Mbowe aka kengeza kwa kushirikiana na mabeberu waliotaka kuona Dkt Magufuli anasingiziwa ndiyo waliotumwa na mbowe wamuue yeye lisu. Ndiyo maana mbowe mpaka leo anakinyongo na huu ndiyo wakati atammalizia kwa sababu ya uenyekiti hahah amuulize ayatola zito alikimbia chama kisa uenyekiti.
Hapo ndio unaona umecheza mindgame la hatari.
 
Katika andiko lake hilo la X ameweka ushahidi wa tuhuma zake? Unaweza kusaidia kuweka hapa jukwaani? Alisema kwenye chama chake yameingizwa manilioni ya rushwa je amewahi kuthibitisha tuhuma hizo? Je unaweza kutuwekea hapa majina ya hao watoa na wapokea rushwa wa CHADEMA? Yeye kama makamu Mwenyekiti alishughulikia vipi masuala hayo? Lissu alisema kuwa alitaka kuhongwa mapesa na mtoto wa Rais je amewahi kuweka ushahidi wa hata CCTV camera? Unaweza kutusaidia kuweka hapa?
Mwashambwa , wewe bado mwepesi sana katika mambo mengi.

Fahamu kuanzia leo: Tuhuma huwa hazina ushahidi wala vielelezo vya ushahidi. Ukiviweka vielelezo au ushahidi wazi kwenye tuhuma, waovu wanaweza kuvichezea au kujipanga kupambana na tuhuma dhidi yao.

Ushahidi na vielelezo hutolewa mahakamani au mamlaka maalum kama kamati za uchunguzi.

Kwa sasa Lisu ametoa tuhuma dhidi ya vyombo vya dola, hivyo vyombo vya dola vilivyotuhumiwa haviwezi kumhoji. Ila Rais ana uwezo wa kuunda kamati maalum huru kufanya uchunguzi ambapo Lisu atalazimika kutoa ushahidi wa tuhuma, ambao kwa ujumla ni mwingi. Ameeleza tangu kifo cha Chacha, kuoigwa kwake risasi na hii mipango yao miovu ya sasa.
 
Kutoka X Lissu anaandika,

Enyi watu wabaya mjulikanao kama 'watu wasiojulikana,' nimezisikia njama zenu. Mnataka kuniumiza halafu mumsingizie Mwenyekiti wetu wa chama, Freeman Mbowe.

Ndivyo mlivyofanya wakati wa kifo cha marehemu Chacha Wangwe. Ndivyo mlivyofanya tena wakati mliponishambulia tarehe 7 Sept '17. Na ndivyo mlivyofanya miezi michache iliyopita mlipomteka nyara na kumuua Mzee Ali Mohamed Kibao.

Ndivyo mnavyofanya kila mnapoua watu wasio na hatia. Mnasingizia watu wengine ili nyie mnaohusika msiwajibike na udhalimu wenu.

Huyo mnayedhani mnamtumikia alitoa ahadi hadharani kuwa nitakuwa salama nikirudi nyumbani. Waziri wake Masauni alirudia ahadi hiyo bungeni.

Mkiniumiza kama mnavyopanga mjue lawama yote itaangukia kwa Samia Suluhu Hassan. Badala ya kumlinda mtamchafua zaidi. Na kama ilivyokuwa kwa Magufuli baada ya 7 Sept '17, ndivyo itakavyokuwa kwa Samia.
Hii ndiyo mbinu maarufu na iliyozoeleka kwa chama chenye mavazi ya rangi ya kinyesi cha wanyama walao nyasi mbichi.
 
Mwashambwa , wewe bado mwepesi sana katika mambo mengi.

Fahamu kuanzia leo: Tuhuma huwa hazina ushahidi wala vielelezo vya ushahidi. Ukiviweka vielelezo au ushahidi wazi kwenye tuhuma, waovu wanaweza kuvichezea au kujipanga kupambana na tuhuma dhidi yao.

Ushahidi na vielelezo hutolewa mahakamani au mamlaka maalum kama kamati za uchunguzi.

Kwa sasa Lisu ametoa tuhuma dhidi ya vyombo vya dola, hivyo vyombo vya dola vilivyotuhumiwa haviwezi kumhoji. Ila Rais ana uwezo wa kuunda kamati maalum huru kufanya uchunguzi ambapo Lisu atalazimika kutoa ushahidi wa tuhuma, ambao kwa ujumla ni mwingi. Ameeleza tangu kifo cha Chacha, kuoigwa kwake risasi na hii mipango yao miovu ya sasa.
Aache ujinga wa kuropoka mambo bila kuwa na ushahidi.sasa kwanini akae na ushahidi wa tuhuma nzito za kuhatarisha uhai wake? Au na wewe umejitungia tu ngonjera zako kama kawaida yako.
 
Takataka wewe akili zako ziko kwenye MNDUKU, kuna siku hao wahalifu wenzio wa serikali ya ccm wataifikia familia yako ili tuongee lugha moja.
Wewe endelea kutukana matusi utafikiri kichaa au mwendawazimu.mimi naendelea kushusha NONDO tu
 
Unawafahamu waliomuua kibao? Unaweza kusaidia jeshi la polisi ?
Waliomwua Ali Kibao walijitambulisha wazi kuwa wao ni nani. Japo walijitambulisha kuwa ni polisi, lakini siyo hawa polisi wa kawaida.

Hawa wanaofanya mauaji yote ya kisiasa, kwa habari za ndani kabisa kwenye vyombo husika, ni wale wanaojiita kikosi kazi. Ndani yake wapo waajiriwa wa polisi, TISS, UWTZ, Greenguards na TRA. Ndiyo maana uliona yule aliyeadhibiwa na wananchi, akitambulishwa kama mwajiriwa wa TRA.
 
Mkuu jeshi likiamua hata leo mtashangaa jinsi wananchi tutawaunga mkono. Ili nchi yetu ianze upya ni aidha machafuko, ama mapinduzi ya kijeshi. Jeshi pekee ndio nguzo yetu, wananchi wengi tutawaunga mkono.
😆😆😆😆😆
 
Huyo mnayedhani mnamtumikia alitoa ahadi hadharani kuwa nitakuwa salama nikirudi nyumbani.

Ingawa idara husika imejitangaza kama mlezi jasiri wa masilahi ya usalama ya Tanzania , historia yake inaonyesha jukumu lake kuu kuanzia hasa 2016 limekuwa kushiriki kuziteka siasa za nchi kwa manufaa ya chama dola kongwe na kuumiza viongozi wa upinzani wa kisiasa.

Mkuu wa zamani mchungaji aliyetupwa kwenda kuwa balozi aliyehudumu Namibia, na vilevile waliomrithi cheo wameshiriki kuvuruga uchaguzi na kuwatia hofu wapinzani wa kisiasa kwa kuwaumiza, kuwateka na hata kuwapoteza wapinzani .

Tahadhari ni kuwa michezo hii inamwisho na ipo siku mkuu wao wa juu kabisa atawakana, na ndipo mtajuta kufanya kazi haramu.


View: https://m.youtube.com/watch?v=CWWzPw0Pv4Y
 
Ee Mungu mkuu uzidiye mamlaka na uweza wote, uliyewahi kuyaangamiza majeshi ya wakuu walioaminika kuwa na mamlaka yasiyoweza kufanywa chochote, Ee Yesu ambaye kwa upendo mkuu ulikubali kuteseka, kuimwaga damu yako, na hata kufa msalabani, ambaye hatimaye uliyashinda mauti ya mwili na Roho, ukamshinda shetani na ufalme wake, ukapewa mamlaka yote Duniani na Mbinguni, kwa mkono wako wenye nguvu, umtazame mtumishi wako Tundu Lisu kwa jicho la huruma na ushindi, tunaomba umshirikishe katika ule ushindi wako dhidi ya mauti kama ulivyomfanyia hapo mwanzo dhidi ya yeyote anayepanga uovu wowote juu ya uhai wake. Kwa sababu ya ile sadaka aitoayo kwa watu wako, kwa kuunena uovu wa watawala wautendao dhidi ya watu wako wasio na uwezo wa kunena wala kujitetea, ukampe ulinzi wako usiopenyeka wala kwa risasi, sumu, kisu au kingine chochote. Na kwa mkono wakp wenye nguvu, hao waupangao huo uovu na waliopangwa kuwa watekelezaji wa uovu huo, matokeo ya uovu walioupanga, yakawarudie wenyewe na watu wao, na washiriki wao, hata mara 3 zaidi.

Yeyote atakaye ulinzi juu ya Lisu na adhabu dhidi ya waovu, kila siku baada ya kufanya toba jwa Bwana, aisali sala hii mfululuzo kwa siku 7 au 3. Kumbukeni kuwa 3 7 na 40 ni namba za ukamilifu.

NB: Sala siyo mbadala ya kutimiza wajibu wetu kama wanadamu kwa kutumia zile nguvu na mamlaka zote aluzotujalia. Wakati tukiomba mkono wenye nguvu wa Mungu dhidi ya waovu, tuendelee kupambana kupinga mifumo na matendo yoyote ya dhuluma dhidi yetu na wengine wote wanaoonewa na mifumo ya utawala na watawala.
 
Ee Mungu mkuu uzidiye mamlaka na uweza wote, uliyewahi kuyaangamiza majeshi ya wakuu walioaminika kuwa na mamlaka yasiyoweza kufanywa chochote, Ee Yesu ambaye kwa upendo mkuu ulikubali kuteseka, kuimwaga damu yako, na hata kufa msalabani, ambaye hatimaye uliyashinda mauti ya mwili na Roho, ukamshinda shetani na ufalme wake, ukapewa mamlaka yote Duniani na Mbinguni, kwa mkono wako wenye nguvu, umtazame mtumishi wako Tundu Lisu kwa jicho la huruma na ushindi, tunaomba umshirikishe katika ule ushindi wako dhidi ya mauti kama ulivyomfanyia hapo mwanzo dhidi ya yeyote anayepanga uovu wowote juu ya uhai wake. Kwa sababu ya ile sadaka aitoayo kwa watu wako, kwa kuunena uovu wa watawala wautendao dhidi ya watu wako wasio na uwezo wa kunena wala kujitetea, ukampe ulinzi wako usiopenyeka wala kwa risasi, sumu, kisu au kingine chochote. Na kwa mkono wakp wenye nguvu, hao waupangao huo uovu na waliopangwa kuwa watekelezaji wa uovu huo, matokeo ya uovu walioupanga, yakawarudie wenyewe na watu wao, na washiriki wao, hata mara 3 zaidi.

Yeyote atakaye ulinzi juu ya Lisu na adhabu dhidi ya waovu, kila siku baada ya kufanya toba jwa Bwana, aisali sala hii mfululuzo kwa siku 7 au 3. Kumbukeni kuwa 3 7 na 40 ni namba za ukamilifu.

NB: Sala siyo mbadala ya kutimiza wajibu wetu kama wanadamu kwa kutumia zile nguvu na mamlaka zote aluzotujalia. Wakati tukiomba mkono wenye nguvu wa Mungu dhidi ya waovu, tuendelee kupambana kupinga mifumo na matendo yoyote ya dhuluma dhidi yetu na wengine wote wanaoonewa na mifumo ya utawala na watawala.
Ameeni mtumishi
 
Back
Top Bottom