Tunduma: Wakuu wa shule wavuliwa nyadhifa kisa wimbo wa Zuchu (Honey)

Tunduma: Wakuu wa shule wavuliwa nyadhifa kisa wimbo wa Zuchu (Honey)

Aisee nilidhani unatania kumbe kweli bhana, tena mwanzoni tu mwa video.. nchi ngumu sana hii..
Acha tu, nilibaki mdomo wazi wakati naangalia hicho kipande uzuri nilikua peke yangu.... halafu bora kingekua kifupi ila wameweka scene nzima ya verse ya Mbosso iwe hivyo
 
Hao walimu ilitakiwa wachapwe na viboko unaachaje watoto wakate vibuno
 
Huo ni uonevu.. matumizi mabaya ya madaraka....
Warudishe hao walimu
 
Mbona kwenye mbio za mwenge walimu hao hao huwakusanya wanafunzi na kuomba mapambio ya kusifu CCM, lakini hamuwachukulii hatua?
 
Huyu prof nae kichwani sifuri kabisa. Ukiangalia ule wimbo watoto walikua wanaimba kwa ufasaha kabisa sasa swali ni Je! hao walimu ndio waliwakalilisha huo wimbo? NO.. Kwahiyo prof kama angekua na akili angeshajua wapi pa kuanzia na sio kufukuza kazi wazazi wenzie ambao wanatumikia nchi kwa mishahara midogo na wana familia zinawategemea.
 
Unamsema zuchu Maudhui yake wakati anayoyaimba ndio unayoyafanya.. unafiki mkubwa
Nafikiri wewe ndio Mnafiki siujui Huo wimbo ndio kwanza nimeona kwenye hiyo clip.Usifikiri humu Kuna wapuuzi wenzio wanaosikiliza hizo takataka.Kwa Tanzania nyimbo nazosikiliza ni Gospel tu hakuna Cha zaidi.
 
Leo nimeona video ya wimbo wa Whozu ft Billnass na Mbosso unaitwa Umeyatimba,
Kipande anachoimba Mbosso kuna sehemu anasema "Nyoooo na Nyokoooo", pia ile video inaonesha anambaka Mwanamke chumbani huku Wanaume wapo sitting room wanashangilia, anampaka hadi mafuta ya nazi....

Nimeshindwa kuelewa mamlaka husika hawajaona haya lakini na hawa wasanii kwanini wanafanya hivi, lengo lao hasa ni nini kutoa nyimbo za namna hii huku wakijua wahanga wakubwa ni watoto na vijana wadogo!??
Nimekuelewa sana,hawa batata sijui wapo kwa ajiri gn? Kuna upumbavu mwingi sana unafanyika kwenye nchi hii,lkn mamlaka zipo kimya kbs.
 
Kwa kweli viongozi wa Tanzani ni sufuri brain, hizo nyimbo zimezaga mitaani watoto wanazimba kila siku hajui maanake, kwahiyo wanalikuza ili wawafundishe maana yake?.......kua mualimu ni laana katika nchi hi

cc@Mpwayungu Village na kusapoti saana unamaono
[emoji1360]
 
Leo nimeona video ya wimbo wa Whozu ft Billnass na Mbosso unaitwa Umeyatimba,
Kipande anachoimba Mbosso kuna sehemu anasema "Nyoooo na Nyokoooo", pia ile video inaonesha anambaka Mwanamke chumbani huku Wanaume wapo sitting room wanashangilia, anampaka hadi mafuta ya nazi....

Nimeshindwa kuelewa mamlaka husika hawajaona haya lakini na hawa wasanii kwanini wanafanya hivi, lengo lao hasa ni nini kutoa nyimbo za namna hii huku wakijua wahanga wakubwa ni watoto na vijana wadogo!??

Kabisa nimebidi kwenda kuutazama, nakubaliana na wewe zile scene hazifai kbs. Zinahamasisha kuwafanyia ubaya wanawake kwa kisingizio kisicho na mantiki.
 
Hakuna sababu yoyote ya MSINGI inayoweza kukubalika ya KUWASHUSHA VYEO, tuache tabia za viongozi wa juu kujiona wao HAWAKOSEI .

Waalimu hao kuwapigia simu na kuwaonya INATOSHA KABISA. mambo mangapi MAGUMU wanayopambana nayo katika mazingira yao ya KAZI lkn kwa dhiki iliyogubikwa na UZALENDO KWA TAIFA LAO wanapambana bila ma ung'uniko.

Kwa HESHIMA NA TAADHIMA walimu hao WASAMEHEWE waliamini wanawasahaulisha wanafunzi wao shida walizonazo.
 
Mmh najaribu kutafakari na kuona kosa la walimu mpaka kuvuliwa nyadhifa zao sioni.

Tujiulize haya!

1.Je kosa ni kurekodiwa na kuwekwa katika social media au

2. Mziki kupigwa maeneo ya shule na watoto kucheza.

3. Je ingekuwa siku ya mahafali ya Darasa la saba na wimbo huo ukapigwa na wanafunzi wakaucheza je mwalimu angevuliwa nyadhifa yake?

Kiukweli tunakemea mmomonyoko wa maadili katika jamii yetu lakini mpaka wimbo umepita basata walichuja wapi na kuona utatumika kwaajili ya wakubwa tu na watoto hawata sikiza wimbo huo?

Watoto wanavyoimba inaonesha wanaujua wimbo tangu awali, this means kwamba kwa siku hiyo tu mwalimu mkuu hajasababisha mmomonyoko wa maadili kwa wanafunzi.

Kumvua cheo mwalimu mkuu ni Kuiambia BASATA kuwa walikosea kuruhusu wimbo huo.
Kwa maoni yangu mwalimu mkuu hana makosa ya kumvua cheo chake.

Yani Kiukweli mawaziri hukurupuka sana katika maamuzi, sijui ni poor kantiri ndo maana na mindset zetu zipo kama hali yetu ya uchumi.

Honeeey.
Madaraka ya kulevya🤣🤣🤣🤣🤣🪑💺
 
Zuchu sijui Chuchu ni mwanaccm wameshindwa kufungia wimbo wake wanaenda kuwavua walimu vyeo.

Mbona kuna majizi ya pesa za umma hayavuliwi vyeo ndio kwanza yanaitwa waheshimiwa.
 
Huyu profesa kichwani ni sifuri kama baadhi ya members JF.

I don't want peace[emoji3577], I want a problems.
 
Back
Top Bottom