Ummy Mwalimu: Kuanzia sasa matibabu ya Joseph Haule(Prof. Jay) yatagharamiwa na Serikali
hii sio sawa, anatibiwa kama nani..

gharama za wagonjwa wengine hapo muhimbili wasio na mbele wala nyuma nazo Serikali itazibeba? tuwe serious kidogo.
Aliyenacho huongezewa, na asiyekuwa nacho hunyang'anywa hata kile kidogo alichonacho. Kumbuka kuwa huyu nae ni mfaidika wa kiinua mgongo cha Tshs. 200m+ alichopata mwishoni mwa 2020.
 
HuYu alikuwa Kiongozi na mwakilishi Rasmi wa Wananchi kwa miaka 5. Alifanya Mengi kwa maendeleo ya Wananchi wa Jimbo lake.(Mbunge).
Kwani alifanya bure, alilipwa zaidi ya bilioni moja kwa kazi hiyo ukijumlisha mishahara,posho za vikao,marupurupu pamoja na pension.
Serikali inatakiwa iwe serious iache cheap popularity kuna watu wa kusaidiwa matibabu wamekosa msaada
 
Anatibiwa kama Mbuge mstaafu we kama hutaki andamana!
Mbunge lisu hakutibiwa ndio useme mbunge mstaafu anatibiwa acheni kutetea matumizi ya hovyo ya fedha za umma ndio maana inahitajika katiba mpya haiwezekani rais ajikurupukie tu aseme fedha za serikali zitumike kumtibu mr flani.
Tunahitaji katiba mpya itakayowezesha kupatikana kwa viongozi wenye weledi wa kuweka mifumo mizuri ya matibabu kwa wananchi wake wote bila ubaguzi
 
Hii ni aibu pia kwa serikali, maana ikiwa mtu kama Prof jay matibabu inakua ngumu kuyamudu. Vipi kwa wale maelfu ambao hata buku mbili tu ya kula hawana uhakika?
Nadhan suluhisho ni bima kwa wote, kama ilivyowahi kufikiriwa iwe namna hyo, pengine inaweza kuwa na uhafadhali.
 
Chadema wala familia ya J haikushindwa kumtibu mtu wao , Kujichomeka kwa serikali ili ipate huruma ya wananchi kusikupumbaze .

Tumenyamaza kwa sababu maalum
Siyo huruma prof alikuwa mtu safi sana Hana siasa za maji taka
 
Total failure ya serikali. Kuficha aibu serikalini angeenda waziri wa sanaa na michezo angalau tungejua wanamtibu mwana sanaa mwenzao. Kwa huyu waziri anatakiwa aseme kuanzia leo watu wote watibiwe bure vinginevyo........

Sent from my SM-A022F using JamiiForums mobile app
 
Jay anapaswa kusaidiwa ikiwa kakwama, Ila wanachohoji hao pia kina mantiki kwa maana Kuna maelfu ya watu ambao wamekufa kutokana na kushindwa kumudu gharama za matibabu.
Kusema tusubiri apone ndio raisi aambiwe, nadhani huu ni ujinga.
Ina maana raisi hajui watanzania wengi hawawezi kumudu matibabu?
Hizi ni roho mbaya.

Wewe Unaona ni sawa Serikali kukaa kimya watu wanashika mabango kuchangishana ili Mbunge Mstaafu apate Matibabu?

Ni mara nyingi TU serikali imesaidia watu wanaojitokeza kuomba michango ya kusaidia wahitaji.

Tusikosoe kila kitu Kwa sababu TU ya roho Mbaya.

Mbona Kuna wapinzani walichangiwa ili walipe faini za mil 30 wakati walikua na uwezo wa kulipa wenyewe.?
Kwani wasingelipiwa wangekufa?

Suala la Matibabu ni suala la kisera sio jambo la kukurupuka na kuanza kulaumu Kwa sababu TU serikali imeona ijaribu kuokoa maisha ya Prof. Jay.

Matibabu Duniani kote ni ghali sana.
Serikali Kwa hili naipongeza. Kuna watu wanatumia matatizo ya watu kama mitaji bila huruma.

Serikali itagharamikia na ukurasa wa michango na vibango vya kuchangia imefungwa.

Anayetaka michango achange akawatibu wengine nao wanahitaji michango.

Kwa Nini hao wanaofanya makongamano ya michango wasifanye ili walipe Matibabu ya wahitaji wengine? Hili la Jay serikali imelibeba . Waendelee na michango ,mbona wapo wengi wanaohitaji tena wanachama wao?
 
Kwani serikali haijui kuna hao 'wengine' wakikata roho kila kukicha hapo hapo Muhimbili (na kwengineko) huku wakikosa hata 10k ya matibabu ?
Endeleeni michango ili mkawalipie hao wengine hili la Prof. Jay mama yetu kipenzi amelibeba.
Changeni msaidie wengine nao mkiweka mabango atawatuma watendaji wao watajirisha kuwa Kuna tatizo Hilo atalibeba pia.

Huu ni mwanzo mzuri ,naipongeza serikali.
Walikataa kumtibu Lisu mkapiga kelele na Sasa Mbunge Mstaafu anatibiwa mnapifa kelele.
Sio ustarabu huo ni kujenga Taifa la watu wenye roho mbaya wasiojua jema na baya.
 
Tuna Safari ndefu Kama nchi,tunaweza kuchukua miaka Mia Tisa na hamsini ili kufika pale tunapoota kila siku...
 
Asante sana Mh. Raisi kwa upendo wako. Prof. J ameitumikia nchi kwa sanaa ilivyotukuka, nyimbo zake na mashairi yake yamekuwa chachu ya mapinduzi makubwa kifikra na kiutendaji wa watu wengi. Serikali haiwezi kugharamia wagonjwa wote, il ni busara kumuokoa Prof kutoka kwenye mauti na fedhea ya kutembeza bakuli. Asante mama kwa upendo ulioonesha.
 
Upo sahihi, lakini vipi kwa wale wasio na uwezo hata wa kulipa elfu 10 kumuona daktari? Wao wanasaidiwa na nani?
Wewe uko wapi ?
Mbona wanatibiwa ! Na kama Hana Elfu kumi si akamuone hata Diwani wake wa CCM au Mtendaji ili aseme kuwa hawezi kulipa?

Ukumbuke kuwa Matibabu ya Jay. bila kumsaidia ujue atafilisika kabisa.

Matibabu madogo madogo watu wanapewa dawa na serikali Kwa kiwango kidogo Cha magonjwa madogo. Lakini magonjwa makubwa hasa magonjwa yanayotokana na tabia za kimaisha hua Matibabu yake ni ghali sana. Na Kwa Karne hii magonjwa yasiyoambukizwa / yanayotokana na hali ya kimaisha yanawakuta watu wengi sana.

Ndio maana hata Mabeberu hawajajitokeza Afrika kufadhili Matibabu ya magonjwa yatokanayo na tabia za kimaisha mana yanagharama kubwa sana.
 
Maneno Makali sana lakini nakuhakikishia ungepewa hiyo wizara usingeweza kuiendesha hata miezi miwili . Maamuzi yake ni sahihi sana na zipo sababu zilizofanya seeikali Kuingilia hili Suala. Utakakatishaji fedha una njia nyingi sana na fedha za kufanya Uhalifu zina njia nyingi. Serikali ina macho kama imeshaamua kuingilia hili Suala wananchi tukae kimya tufanye mambo mengine mf. Kuhudumia familia yake n.k
Serikali imetumia busara kubwa sana .
Nampongeza sana mama yetu Kipenzi Mh. Samia Suluhu Hasani Kwa utu wake.
Prof. Jay ni mtu maarufu sana. Haikua busara kuacha watu wapitishe mabango ya michango kwenye mitandao ndani na nje ya nchi Kwa mtu aliyelitumikia Taifa hili Kwa uamunifu. Watu wangeishangaa sana serikali kuwa imemtenga Kwa sababu ni Mpinzani. Na Kwa watu wenye roho mbaya kwao waliona watafanikiwa kuonyesha Dunia kuwa serikali haiwajali wapinzani.

Na pia kama walishachanga Kwa Nini hizo walizochanga na wanazoendelea kuchanga wasiende kuwalipia watu wengine pale muhimbili ili wapatiwe Matibabu? Wote ni watanzania ! Au palikua na agenda nyingine?
 
Watanzania hatuna jema kwa kweli, kama hadi hili la Prof J kusaidiwa inakuwa nongwa?
Kumbuka kuna maskini wanakufa kwa kushindwa kulipia huduma ya matibabu.

Kumbuka kuna maiti zinazuiwa hospitali kwa kukosa pesa ya kulipia matibabu.

Je kuna umuhimu wa professor J kulipiwa matibabu wakati kiasi fulani ana uwezo?

Wao hao wanaokufa kwa kukosa uwezo wa kulipia matibabu wao ni halali kufa? Fikilia kabla ya kushabikia ujinga.

Huyo anasaidiwa kwa sababu alikuwa ni chawa wa CCM. Kumbuka enzi za JPM huyo mgonjwa alikuwa akihudhulia mikutano ya JPM Morogoro na kupewa fursa ya kuimba wakati viongozi wa CDM hawakuwa wakihudhulia mikutano hiyo. Na hata akihudhulia hapewa ruhusa ya kusalimia.
 
Kila mtu hupewa kulingana na mchango wake katika jamii..ukizieoewa kanuni za maisha na ikazifata favors zitakuwa upande wako...huyu mtu Ana mcnago mkubwa na chanya katika jamii..
Huyo mwingine ambae hapati favors Kama hizi maana yake mchango wake katika jamii ni mdogo...masikini kabisa atapata kidoogo Sana na pengine asipate kabisa..ni kanuni za maisha jaman...
 
Ukisikia ule msemo wenye akili hawana power na wenye power hawana akili ndio hiii.

Hivi Serikali inawezaje kutoa statement kama hiyo mbele ya jamii-bora wangemlipia kimya kimya.
Tuna viongozi ambao hawatumii akili kabisa,by the way sisi Wananchi ndio matahira kabisa -acha mambo yaende.
Wangemlipia kimya kimya matapeli wangeendea kupitisha michango na kuwaibia watu bila huruma.

Tuachae kupinga kila kitu.
Michango ilikua ni ya wazi na serikali imetoka wazi kusitisha zoezi Hilo Kwa kulipia Matibabu yake hata kama yatagharimu mabilion ya fedha.

Suala la Lisu limewafundisha mengi. Na mama Samia Hana roho ya Kwa Nini kwake wote ni binadamu sawa.

Waliotegemea kutafuta kiki za michango Bado wananafasi ya kuchangia michango ya wagonjwa wengine ili watibiwe. Tena wengine wanahitaji michango kidogo TU.
 
Back
Top Bottom