Ummy Mwalimu: Kuanzia sasa matibabu ya Joseph Haule(Prof. Jay) yatagharamiwa na Serikali
hili lipo toka enzi na enzi, hata kwa Mungu hakuna usawa,hata Yesu aliwahaidi pepo wale jamaa aliosurubiwa nao, utauliza kwanini wale aliwakubalia kuwa nao katika ufalme wa mbinguni huku akiacha wengine wajipiganie wao ?
hata Mungu alimsifu Ayubu,je watu wengine wangelalamika kwanini hajawasifu ?

Unachohitaji kuelewa ni kwamba sio vitu vyote vinalinganishika. Vitu vingine havilinganishiki!

Haya, tuambie ni kitabu gani kwenye Biblia kinamzuia Mungu (akiwemo Mwanae wa pekee) kufanya discrimination?
 
[emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji120][emoji120][emoji120]
 
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amesema kuanzia sasa Serikali itagharamia matibabu ya aliyekuwa Mbunge wa Mikumi Joseph Haule Profesa J anayetibiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili hadi hapo atakaporuhusiwa kurudi nyumbani.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu alipofika Muhimbili leo kumjulia hali Msanii huyo.



Pia soma:
Tumuombee sana Profesa J
Mke wa Profesa Jay afunguka, familia yaomba msaada wa matibabu
Hii naona kama ubaguzi mbona aliokuwa naibu waziri Wa nishati na madini pia Mkuu Wa wilaya mbalimbali nchini bila kusaha mbunge Wa kigoma kusini hali yake mbaya mgonjwa serekali hawaendi kumuona wala nini wamemtelekeza wanasubiri afe wamsifie nakumpamba kwakuwa hatokuwa na uwezo wakuwajibu au kwakuwa alitetea mahakama ya kadhi ?
 
Waseme vizuri atatibiwa nakodi zetu wananchi!!
Serikali haina helazake hata rais hanahela zakugawa maendeleo kama mnavyoaminisha watu, muachage uongo ni dhambi!!
Nionavyo serikali inatafutia umaarufu kupitia ugonjwa wa mtu huyu maarufu Nigga J... Maskini kibaaao wanatesekea matibabu hawana ndugu wala marafiki!!!
kama tungekea na serikali unbiased inayojali watuwake woote basi wamfidie na Tundu Lissu alopigwa risasi akiwa kazini kulijenga taifa lkn akajitibia mwenyewe...
Basi wamwachie Freeman na waifute hiikesi isiyo na "kichwawalamiguu"!!!
Kuonesha upendo kwa kubagua ni unafiki na uzandiki wahali yajuu.
Nigga ataponywa na Mungu tunamuombea heri kuu.
 
Jambo jema sana, serikali iwaone na makapuku wengine wanaokufa kwa maumivu sana kwa kukosa support ya matibabu.

#HAKIKWAWOTE.
Umeshasema makapuku.hivi huoni hata kwenye msafara wa rais makapuku hawathaminiwi??
 
Hii naona kama ubaguzi mbona aliokuwa naibu waziri Wa nishati na madini pia Mkuu Wa wilaya mbalimbali nchini bila kusaha mbunge Wa kigoma kusini hali yake mbaya mgonjwa serekali hawaendi kumuona wala nini wamemtelekeza wanasubiri afe wamsifie nakumpamba kwakuwa hatokuwa na uwezo wakuwajibu au kwakuwa alitetea mahakama ya kadhi ?
Nani huyo Mkuu Kwa jina?
 
Ni unafiki tu hakuna chochote huyo wasanii na wanasiasa wenzako wako tayari kumtibu tunataka serikali itowe matibabu kwa watu wote bila ya kuangalia wasfu wa mtu tunataka universal health care kuanzia maradhi madogo mpaka makubwa.

Unachanganya mambo na unaleta mada tofauti kabisa . Hili serikali ililofanya ni jambo sahihi sana kwa mtu kama Prof Jay , huyu ni mtu aliibadirisha bongo fleva kutoka kwenye uhuni mpaka kuwa mziki rasmi na sasa si ajira tu bali ni mziki unaitangaza Tanzania nje . Jay ni game change ni watu wanaleta turning point katika mambo mbali mbali , watu wa namna hii ni wachache sana Duniani.

Turudi kwenye suala lako la matibabu bure kwa kila mwananchi , Serikali yako ina uwezo huo ? Mko tayari kulipia (Angalia tozo tu zinavyopigiwa kelele angalia ukwepaji kodi ulivyokithiri). Achana na hiyo je unajua Bima NHIF ni minimum sh ngapi kwa mwaka ? Unajua ni pesa ndogo sana. kijana wa Kitanzania anayebeti kila siku ana uwezo wa kubadili mtazamo na kupeleka pesa yake kwenye bima ikamsaidia yeye na wazazi au watoto wake, unalijua hili ? It is easy to blame policy makers lakini na sisi tujiangalie tuna mchango gani kwenye suala tunalolalamikia …
 
Wanasiasa na fursa za kutafuta popularity.

Hapo hapo MNH kutakuwa na wagonjwa makapuku kwelikweli wanashindwa kufanya dialysis kwa kukosa tu fedha but no one will care,lakini kwa mtu maarufu huyu ambaye kashaanza kuomba michango kwa umma serikali inasema italipia full,so michango i-stop.
 
Nani huyo Mkuu Kwa jina?
Huyu siwezi kumtaja kwasababu hajanituma nawala hanijui lakini nikwambie tu aliwahi kuwa naibu waziri Wa nishati awam ya 3 baadae Mkuu wa wilaya tofauti akitokea kigoma kusini kwasasa uvinza ccm wanamtambua vizuri amewahi kutetea mahakama yakadhi nadhani hii ndio ilikuwa Zambi yake kubwa na kuchukiwa kwa uaminifu Hanna mfano wakumzidi ni mitume tu
 
Makada Chadema tumechanga mil 22, safi sana.
20220214_052827.jpg
 
Back
Top Bottom